VIJANA WAKICHIMBUA KABURI ALIMOZIKWA ALIYEKUWA HAI
KWANZA
KABISA WANAANZA TOA JENEZA LA ALIEKUFA KWA UGONJWA NA KUZANIWA AMEROGWA
NA ALIYEZIKWA AKIWA HAI MAANA KATIKA KABURI HILO WALIZIWA WATU WAWILI
KATIKA KABURI MOJA ALIE HAI NA MFU
JENEZA LA ALIEKUFA KWA UGONJWA TAYARI LIMETOLEWA HILO PEMBENI SASA ANAFUKULIWAALIEZIKWA HAI
MWILI WA ALIEZIKWA AKIWA HAI SASA UNATOLEWA KABURINI
HII
MITI NDIYO ILIYOTENGANISHA JENEZA NA ALIEZIKWA AKIWA HAI KWANZA ALIANZA
ALIE HAI KUZIKWA IKAFUATIA MITI HIYO NDIYO LIKAFUATA JENEZA LA ALIEKUFA
KWA UGONJWA
MWILI WA ALIEZIKWA AKIWA HAI BAADA YA KUTOLEWA KABURINI
MDOGO WA MAREHEMU ALIEZIKWA AKIWA HAI
MWILI WA ALIEKUFA KWA UGONJWA ULIZIKWA TENA NA WANAUSALAMA KUONDOKA NA MWILI ALIEZIKWA AKIWA HAI
WANANCHI HAO HAIKUTOSHA BAADA YA KUMZIKA MWENZAO AKIWA HAI WALIKWENDA KUCHOMA NYUMBA YAKE
NA KUHARIBU MAZAO YAKE SHAMBANI
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida wananchi wa
kijiji na kata ya Mkwajuni Wilaya ya Chunya Mkoani hapa wamemzika Mwanakijiji
mwenzao akiwa hai wakimtuhumu kusababisha kifo cha Mkazi mmoja kijijini hapo.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea Apri 26
mwaka huu majira ya Saa Nane Mchana katika Kitongoji cha Maweni
Makaburini baada ya Mhanga aliyefahamika kwa jina la Victory Mwachirui(68)
kuhudhuria mazishi ya Pita Barton(28)aliyefariki baada ya kuugua kwa muda
mrefu.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Thobias
Ismail amesema marehemu alipatwa na umauti akiwa anapatiwa matibabu kwa mganga
wa jadi ambaye jina lake halikuweza kujulikana maramoja.
Amesema wakati taratibu za mazishi zikiendelea
Ndugu wa marehemu walidai kuwa kifo cha Marehemu kilisababishwa na Mwachirui
ambaye ni Katekista mstaafu kwa imani za kishirikina.
Ameongeza kuwa wakati kaburi likichimbwa kwa
ajili ya kumzika marehemu ndipo vijana waliokuwa wakichimba waliagiza
Wazee wa Mila wafike makaburini kwa ajili ya kuangalia utaratibu wa mazishi na
kukagua ukubwa wa Kaburi ambalo lilikuwa limekwisha chimbwa.
Kutokana na mwito huo walifika wazee wanne
akiwemo Mzee Mwachirui ambaye walimsisitiza kusogea jirani na kaburi ambapo
baada ya kusogea alipigwa na Sururu kichwani na kuangukia kaburini huku
akisindikizwa na marungu.
Baada ya Mzee huyo kupoteza fahamu Vijana
hao walianza kutandika fito ndani ya kaburi kisha kufukia kwa udongo kiasi kwa
lengo la kutenganisha na Mwili wa Marehemu Pita uliokuwa kwenye jeneza baada ya
kuwazika kwenye kaburi moja.
Baada ya kukamilika kwa zoezi la mazishi kundi
la vijana lilielekea hadi nyumbani kwa Mzee aliyezikwa akiwa hai na kuiteketeza
nyumba yake huku wakiapa kutotoa siri wakidai Siri ya Jeshi.
Hata hivyo baadhi ya wananchi walitoa taarifa
kwa Mwenyekiti wa Kijiji hicho aliyefahamika kwa jina la Credo Kayanza ambaye
pia alitoa taarifa kwa Diwani wa Kata hiyo Chesco Ngairo ambao kwa pamoja
walitoa taarifa Jeshi la Polisi ambao baada ya taarifa hiyo walifika eneo la
tukio huku wakidhani lililotokea ni kuchomwa kwa nyumba pekee.
Jeshi la Polisi baada ya kufanya upelelezi na
kubaini kitendo hicho waliwaamuru baadhi ya Vijana kufukua kaburi hilo zoezi
ambalo lilifanyika baada ya Vijana hao kulipwa.
Baada ya kufukuliwa kwa kaburi hilo Mwili wa
Marehemu Mzee Mwachirui ulichukuliwa na kupelekwa katika Hospitali ya Misheni
ya Mkwajuni kwa ajili ya Uchunguzi huku Mwili wa Pita ukizikwa upya palepale.
Baada ya kukamilika kwa uchunguzi mwili wa
marehemu ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya mazishi ambapo Marehemu alizikwa
katika eneo tofauti na alipokuwa amefukiwa awali.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani
amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo pia ametoa wito na kuwaasa
wananchi na jamii kuacha tabia ya kuamini mambo ya ushirikina na uchawi
kwa madai kuwa hauna faida kwao bali huchochea migogoro katika jamii zao.
Aidha ameongeza kuwa wakumbuke kitendo cha
kujichukulia sheria mkononi ni kosa kisheria ambapo pia amewaomba wenye
taarifa za walipo waliohusika na mauaji hayo kuzifikisha polisi haraka ili
hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao ingawa hakuna aliyekamatwa kuhusika na
tukio hilo.
Marais wa jumuiya ya Afrika Mashariki wakisimama kwa dakika moja
kumkumbuka laiyekuwa Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka Uganda
Marehemu Eriya Kategaya wakati wa ufunguzi wa kikao cha kumi na moja
cha Jumuiya hiyo jijini Arusha leo mchan. Katika Hoteli ya
Ngurdoto.Kutoka kushoto Rais Wa Burundu Pierre Nkurunzinza,Mwenyekiti wa
Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda,Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Rais Dkt.Jakaya
Mrisho Kikwete akiteta jambo na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya wakati wa
ufunguzi wa kikao cha juu cha kumi na moja cha Wakuu wa nchi wa jumuiya
ya Afrika Mashariki kilichofaniyka jijini Arusha.
Marais Wa jumuiya ya Afrika Mashariki waliohudhuria Mkutano wa Wakuu
wa jumuiya hiyo katika hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha leo.Kutoka
kushoto ni Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi,Mwenyekiti wa jumuiya hiyo
Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda,Mwenyeji wa mkutano Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Mpya wa Kenya,Uhuru Kenyatta(picha na
Freddy Maro)
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Mkewe
Margareth Kenyatta wakifurahia ngoma za utamaduni muda mfupi bbada ya
kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro kuhudhuria
Mkutano wa Wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika
jijijini Arusha(picha na Freddy Maro)
Rais .Jakaya Kikwete akimkaribisha Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta katika
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowasili juzi jioni
kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuia ya Afrika ya Mashariki
unaofanyika jijini Arusha. (PICHA NA FREDDY MARO)
Hayo yamebainishwa na ofisi
ya mganga mkuu mkoa wa mbeya kitengo cha huduma za afya ya uzazi na mtoto kwa
kushirikiana na shirika la UJERUMANI (GIZ).
Akiongea na waandishi wa
habari ofisini kwake mratibu wa huduma hiyo PRISCA BUTUYUYU amesema kumekua na
upungufu mkubwa kwa baadhi ya wanaume kutoshiriki katika huduma za afya ya
uzazi.
“Katika tafiti zilizofanywa
kwa wilaya nane za mkoa wa mbeya tangu mwaka 2009 hadi 2011 zimeonyesha idadi za wanawake wanaokwenda
klinic wakiwa na wenzi wao imendelea kuporomoka kila wakati hivyo ofisi yetu
imeliona hilo na umuhimu wake hivyo kuchukua jukumu la kuhamasisha wanaume kushiriki
katika hupata huduma za afya wakiwa na wenzi wao” BUTUYUYU amesema.
Kunafaida kubwa kwa wenzi
kushiriki pamoja katika huduma za afya
ya uzazi kama vile kupima pamoja,
hususani maambukizi ya VVU kwani kwa kufanya hivyo mnaweza kujitambua na kuishi
maisha ya kumlinda mtoto pamoja na mwenzi wake endapo mmoja wao atagundulika
ana maambukizi, BUTUYUYU amesea
Ameongeza kua mbali na kupima
magonjwa pia kunaelimu mbalimbali ikiwemo kujifunza namana ya kupanga uzazi,
jinsi ya kulea mimba kujiandaa kupokea
mtoto atakapozaliwa pamoja na jinsi ya
kumlea.
Kwakuona umuhimu wa swala
hilo kwa wananchi wa TANZANIA, ENGENDER HEALTH kwa kushirikiana na shirika
la FHI 360 limetoa mradi wa champion wa kuhamasisha
vyombo mbalimbali vya habari kushiriki katika kampeni hii ili kuandika habari pamoja na vipindi vyenye kutoa ujumbe
wenye kuhamasisha wenza kushiriki katika huduma za afya ya uzazi,
Akiongea katika semina ya
waandishi wa habari iliyofanyika katika ukumbi wa IFISICOMMUNITY CENTER
afisa mratibu mwandamizi wa mradi wa champion MUGANYIZI MUTTA amewataka
waandishi kushiriki katika kampeni hizi.
“Mradi huu upo katika mikoa
kumi yenye maambukizi ya juu ya VVu, kwa hiyo tumelenga katika kuhamasisha wanaume
kupunguza kuwa na mahusiano ya wanawake wengi, kupambana na mila na desturi
katika jamii, Kuweka sera mahari pa kazi kuhusu swala la wanaume na maambukizi
ya VVU” amesema MUGANYIZI.
Ameongeza kuwa habari zilenge
kuhamasisha mambo hayo muhimu na mwandishi
atakaye andika habari na ikatumika
katika chombo chake itakuwa imeinga katika shindano la Champion ambalo zaidi ya
Tshs milioni mbili kushindaniwa.
NILITEMBELE KITO CHA AFYA CHA RUANDA KILICHOPO MWANJELWA JIJI MBEYA KUJIONEA HUDUMA ZINAVYOENDLEA HUSUSANU HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO
SELINA KOMBANI MRAIBU WA HUDUA ZA AFYA YA UZAZO NA MTOTO ALIE UPANDE WA KULIA AKIONGEA NA MASHAKA BONIFAS PAMOJA NA MKEWE SEKELA MWASONYA WALIPOHUDHURIA KLINIKI PAMOJA
BAADA YA MAHOJIANO SELINA ANAMPATIA HUDUMA HARAKA KWAKUA AMEONGOZANA NA MWENZI WAKAKE
BAADA YA KUWAHUDUMIA WALE WALIONGOZANA NA WENZI WAO KATIKA KUPATA HUDUMA NDIPO SERINI HUAANZA KUTOA ELIMU KWA WALE AMBAO HAWAKUONGOZANA NA WENZI
BAADA YA MAFUNZO NDIPO SHUGHURI ZA UPIMAJI ZINAENDELEA
BAADHI YAO WAKISUBILIA HUDUMA ZA DAKRALI WAKIWA KATIKA FORENI TOFAUTI NA WALE WALIKWENDA NA WENZI WAO HUPEWA KIPAU MBELE
JESTINA LUHANGA AKICHEKA JAPO KWA MAUMIVU MAKALI KUTOKANA NA MAUMIVU YA KUJIFUNGUA KWA UPASUAJI BAADA YA KUFARIJIWA NA MWENZI WAKE KWA KULETEA ZAWADI YA KITOTO CHA KIKE
BAADHI YA NDUGU JAMAA NA MARAFIKI WAKIWA KATIKA WAD YA MAMA WAJA WAZITO WAKIMTAKIA HARI BI, JESTINA
Huenda Rais Uhuru Kenyatta akalitangaza Baraza la Baraza la mawaziri wiki hii.
Nairobi.Baraza
la mawaziri nchini Kenya linangojewa kwa hamu na wananchi ambapo wangi
wanatarajia liwe la mseto kama ilivyo Katiba ya Kenya.
Taarifa kutoka Kenya ambazo ni za kuaminika
zimesema kwamba kuna uwezekano mkubwa kutangazwa kwa Baraza hilo kati
kati ya wiki hii.
Pia Taarifa zilifichua kwamba washirika kwenye
muungano wa Jubilee bado wanajadiliana kuhusu ni upande upi utatoa
nafasi kwa baadhi ya vyama vidogo vilivyotia sahihi mkataba wa maelewano
baada ya uchaguzi mkuu kwa lengo la kuimarisha utawala wa Jubielee.
Kutokana na hali hiyo raia wa Kenya wamekuwa wakisubiri kwa hamu kusikia baraza jipya la mawaziri likitangazwa .
Taarifa ziliendeela kudodosa kwamba mahojiano na
washirika wa karibu wa viongozi yalionyesha kuwa viongozi hao wameamua
kubadilisha kabisa muundo wa utawala.
Kwa sasa anachokifanya rais wa Kenya Uhuru
Kenyatta akiwa na timu yake ,anaandaa majina ya baraza lake la Mawaziri
na pia makatibu,wakuu wa mashirika pamoja na nyadhifa zingine za juu
wakiwemo wakurugenzi wa Wizara na Idara.
Hiyo ina maana kuwa Wakenya watajionea baraza
jipya kabisa la mawaziri, makatibu wapya, mabalozi, maofisa wakuu wa
mashirika ya serikali na wakurugenzi wa wizara na idara mbalimbali.
Hata hivyo awali Rais Kenyatta alishatoa ahadi ya
kulitangaza baraza lake la mawaziri wapya huku akizingatia taaluma,
utendaji wa kazi, uwakilishi wa kimaeneo na jinsia. Kutokana na hali hii, baadhi ya mabalozi walioagizwa warejee nyumbani huenda wasirudi katika nafasi zao za awali.
Marehemu Bi Kidude alikuwa ni gwiji wa
muziki katika Bara la Afrika. Jina lake halisi ni Fatuma binti Baraka. Bi Kidude
ni msanii mkongwe na mahiri sana katika fani ya muziki wa mwambao ambao
hujulikana kwa jina la Taarabu.
Muziki huu ambao ni mchanganyiko wa muziki toka nchi
za Kiarabu na vionjo vya muziki wa Kiafrikaumekita sana katika mwambao wa Afrika
Mashariki yaani Zanzibar, Mombasa, Lamu na
kwingineko.
Leo hii ni Marehemu! Nguli na Mtunukiwa wa Nishani
ya Uhuru wa Tanganyika/Tanzania 2012, Fatuma binti Baraka au Bi Kidude,
alizaliwa katika kijiji cha Mfagimarigo Zanzibar katika familia ya watoto saba
(7). Baba yake Mzee Baraka alikuwa ni mfanyabiashara wa nazi, zao ambalo ni la
kutumainiwa sana Zanzibar.
Bi Kidude aliwahi kusimulia kuwa hafahamu tarehe
halisi aliyozaliwa, isipokuwa anachojua ni kwamba alizaliwa
wakati rupia ikitumika kama fedha, na vilevile ana hakika ni kabla ya Vita Kuu
ya Kwanza ya Ulaya. Wataalamu wa mahesabu baada ya kupata taarifa hizo
wakampigia mahesabu na kumkabidhi miaka yake kwamba ni zaidi ya miaka
90.
Bi Kidude aliendelea kusema uimbaji aliuanza tangu
alipokuwa na umri wa miaka kumi na alijifunza kutoka kwa msanii mkongwe na
aliyetamba sana enzi hizo Sitti binti Saad. Anasema wageni wengi kutoka sehemu
mbalimbali walikuwa wakifika Zanzibar kuja kumwona Sitti, na kwa vile Bi Kidude
na Sitti walikuwa wako karibu basi yeye alikuwa akiwapeleka wageni wale nyumbani
kwa Bi Sitti, wakifika huko wageni walikuwa wakiingia ndani na yeye kubakia nje,
kule ndani Bi Sitti alikuwa akiwaimbia wale wageni, na yeye huku nje alikuwa
akimsikiliza kwa makini na kumfuatiza jinsi alivyokuwa akiimba. Aliendelea hivyo
hadi akawa mahiri sana katika uimbaji.
Alipokuwa na miaka 13, kwa mara ya kwanza alitoroka
nyumbani kwao Zanzibar na kukimbilia Tanzania Bara, baada ya kulazimishwa
kuolewa. Lakini alipokuwa kigoli wa kutosha kuolewa aliolewa ingawa ndoa hiyo
nayo haikudumu kutokana na manyanyaso aliyokuwa akiyapata, hivyo aliamua
kukimbilia kaskazini mwa Misri ikiwa ni katika miaka ya 1930, huko aling'ara
sana katika fani yake ya uimbaji na uchezaji ngoma. Lakini ilipofika miaka ya
1940 aliamua kurudi nyumbani Zanzibar ambako aliendelea na shughuli zake
uimbaji.
Bi Kidude hategemei kazi moja tu ya kuimba, kwani
pia ni mfanyabiashara ya 'wanja' na 'hina' ambavyo anavitengeneza yeye mwenyewe,
pia ni mtaalamu wa matibabu kwa dawa za mitishamba na zaidi ya hayo ni mwalimu
mzuri sana wa 'Unyago' na ameanzisha chuo chake mwenyewe na anasema katika
wanafunzi wake wote hakuna aliyepata talaka kutoka kwa
mumewe.
Watu wanasema 'Utu uzima dawa' Bi Kidude ana upeo
mkubwa sana wa akili kwani pamoja na kukulia katika mazingira yaliyogubikwa na
tamaduni za kiarabu ambapo mwanamke anatakiwa wakati wote akiwa hadharani
ajifunike, Bi Kidude aliliona hili katika upeo mwingine kwamba ni sheria tu ya
kitamaduni toka Uarabuni, hivyo aliamua kuvunja sheria hiyo na
kuondoa hijabu mwilini mwake, na sasa hivi anavaa kama Mtanzania na si
kama Mwarabu. Lakini hakubakia hapo alivunja na miiko mingine zaidi ya
kutokunywa na kuvuta, kwani Bi Kidude anakunywa pombe na kuvuta sigara jambo
ambalo si kawaida kwa wanawake Zanzibar.
Bi Kidude amekwisha tembelea nchi nyingi sana ikiwa
ni pamoja
na Oman, Ufaransa, Hispania, Ufini, Ujerumani na Uingereza.
Amekwisha pata tuzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na
ile ya Tamasha la Filamu la Nchi za Jahazi (ZIFF) mwaka 1999 tuzo ni ya maisha.
Pia mwaka jana tuzo ya WOMAX ilienda kwake.
Nyimbo alizowahi kuimba ni pamoja na Muhogo wa
Jang'ombe, na anaimba kwa Kiswahili na Kiarabu. Hakuwahi kupata elimu nyingine
zaidi ya Kurani.
Bi Kidude pia amekuwa akishirikishwa na wasanii
wengi wakongwe na chipukizi katika nyimbo zao. Miongoni mwa nyimbo zinazotamba
sana siku hizi ambazo Bi Kifude ameimba na vijana wa kisasa ni za Msanii Ali
Toll maarufu AT.
Mbali na AT lakini pia Bi Kidude amewika na kung'ara
zaidi katika wimbo mwingine wa vijana wa Ahmada Umelewa wa Msanii Offside Trick
ambao umepigwa marufuku kupigwa kwa sasa visiwani
Zanzibar.