Pages

Ads 468x60px

Thursday, May 29, 2014

Mtu mmoja amekutwa ndani ya maji akiwa amekufa sokomatola barabara ya saba katika mto Mbata


Mtu alie julikana kwa jina la Jofrey Mwambeja anae kadiliwa kuwa na umli wa miaka 30-35 amekutwa amekufa ndani ya maji ya mto mbata uliopo sokomatola kata ya maendeleo jijini mbeya
 Kaka wa marehemu Fredy Mwambeja akiwa katika majonzi mazito ya kuondokewa na mdogo wake 


Mwaili wa marehemu Jofrey Mwambenja baada ya kumtoka ndani ya maji maeneo ya sokomatola


                              Wasamalia wema wakijaribu kuweka sawa mwili wa marehemu
                       Askali kanzu wakipata maelezo kutoka kwa diwani wa kata hiyo Pantareo Shio




                                      Baadhi ya watu waliofika kushuhudia tukio hilo

             Kaka wa marehem akiwa ndani ya gari la polisi tayari kuelekea Hospitali a Rufaa mbeya


KIZAZI HIKI KIMEKWA AKIBA KWA MOTO WA MILELE

Wale wote walioasi hawatafika mbinguni kwa baba


Viongozi wa mbeya moraviani Town Choir wakimtembelea Askofu Conradi Nguvumali Nyumbani kwake Sumbawanga


Mbeya moraviani Town Choir wakiimba na Mkuu wa mkoa wa Sumbawanga Stella Manyanya wakimpokea Waziri Mkuu Pinda



Viongozi Mbalimbali akishikana mikono na  Viongozi Baada ya kuwasili Ikulu ya Mijini Sumbawanga

Wachungaji wakiwa katika hali ya kumsikiliza waziri mkuu katika ukumbi wa mikutano katika ikulu ya Sumbawanga


Mbeya moraviani Town Choir wakonesha umahili wao katika uimbaji uliofanyika katika kanisa la moraviani Sumbawanga




Maandamano ya waumini na wachungaji kuelekea uwanja wa kumbukumbu ya Nelesoni Mandela kwa ajili ya ibaada ya kumsimika Askofu nguvumali







Askofu Nguvu Mali akiwasili na kusalimiana na maaskofu na viongozi katika viwanja vya Neleson Mandela

Mgeni Rasmi Waziri Mkuu Pinda akiwasili Kiwanjani hapo akipokelewa na maaskofu Mbalimbali



 Mbeya Moravian Town choir Wakitumbuiza mara baada ya kuwasili Mgeni Rasmi waziri mkuu Pinda kiwanjani hapo






              Kwaya mbalimbai zimeshiriki kuimba katika ibaada ya kumsimika Askofu Nguvu mali
 Katibu wa jimbo la Sumbawanga akitambulisha wageni mbalimbali waliofika kushudia ibaada ya mbaraka wa Askofu

                                                  Baba na mama wa Askofu nguvumali




Watu mbalimbali waliofika kushuhudia Mbaraka wa Askofu Nguvumali wakiwa katika uwanja wa mandela
               Mjumbe wa bodi ya kanisa aCharle Mwakipesile akiteta jambo na Askofu Kiongozi




                   Maasikofu wakisoma masomo katika ibaada ya mbaraka wa Askofu Nguvumali

             Askofu Aizack Nikodemu wa jimbo la Magharibi Tabora akihubiri katika ibaada hiyo











                        Matukio mbalimbali ya shughuri nzima ya mbaraka wa Askofu Nguvu mali
                                                 Wachungajiwaki andaa kiti cha kiuaskofu
                             Askofu Nguvumali paoja na mke wake baada ya kubarikiwa

 Mc Charles Mwakipesile akiongoza utaratibu wa mkutano huo na alikua kivutio sana katika ibaada hiyo










                                                                   
                                                                      HABARI KAMILI




Charles Mwaipopo

Askofu wa Kanisa la Moraviani Tanzania Jimbo la Magharibi Tabora  AIZACK NIKODEMU ameya sema hayo katika Ibaada ya  kumsimika Askofu wa Kanisa la Moraviani Jimbo la Rukwa CONRAD NGUVUMALI iliyofanyika katika uwanja wa NELSON MANDELA Sumbawanga na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa na madhehebu mengine ya kikristo nchini.

“Biblia imesema wazi kwamba kizazi hiki chote kimewekwa akiba kwa moto wa milele kwani Yesu anasema nikifananishe na nini kizazi hiki, watu wake hawambiliki hawasikii wameingiza siasa kanisani watu  wame jaa unafiki wanacheka nawe kumbe hawakutakii mema katika maisha yako” Amesema Nikodem.

Ameongeza kua dunia ina wacheka wale wote waliopitwana wakati, kwakua wakati ni wakati tu wengi wao hutenda dhambi zilizopitwa na wakati huko ni kupitwa na wakati kwakua mungu alikifutilia mbali kwa maji kizi kilichopita na kumuokoa Nuhu kwa sababu ya dhambi.

“Hakuna dhambi iliyo mpya katika dunia hii wewe uliyepitwa na wakiti unatenda dhambi zilizopitwa na wakati Mungu alikifutilia mbali kizazi cha Nuhu kwasababu ya dhambi akaaanza kizazi kipya nacho kikaasi akakakichoma moto enzi za Sodoma na Gomola, Nawaambia wale wote walioasi hawataingia mbinguni” Ameongeza  Nikodemu.

Akiongea kwa Msisitizo mkubwa juu ya ubaya wa dhambi amesema Dhambi inalitesa kanisa, Taifa la Tanzania limegawanyika katika makundi kwa sababu ya ambi na koo zimetengana, na maisha yamekua magumu, Mungu anakusumbiria urudi kwake akupumzishe na kukuongoza katika maisha ya kumpendeza yeye.

Kwa upande wao waumini waliohudhuria ibaada hiyo wamempongeza mkuu wa mko wa Rukwa Stella Manyanya kwa kitendo chake cha ujasili katika kutafuta suru kati mwasiasa mkongwe Dr Chrisent Mzinda kaya na Mbunge wa Sumbawanga Mjini (ccm) Aeshi Hilaly Ambao wamekua wakitofautiana tangu uchaguzi upite.

Pamoja na juhudi hizo haziku zaa matunda baada ya Mzindakaya kukataa kusemehe mpaka pale watakapofuata taratibu na mashalti aliyowapa wakati waziri mkuu alipojaribu kuwapatanisha kwamba zitumike taratibu za vikao vya chama na si katika mikutano ya dini kwani haihusiani na siasa

Nae Aeshi Hilaly alikili kuwepo kwa tofauti kati yake na na mkongwe huyo katika siasa na kusababisha kuwepo kwa makundi katika chama chao na kumuomba msamaha mzee huyo akisema hakuna marefu yasiyo na ncha naomba nisamehewe ili tuweze kuijenga Rukwa yetu.

Waziri mkuu Peter Pinda Amewataka wa viongozi kuto kimbilia wala kufurahia kazi za kuwaongoza watu kwakua ni mzigo mkubwa ambao hautakiwi kuona raha endapo unachaguliwa kuwa kiongozi wa kuongoza watu kwakua ni vigumu sana kuwaongazo watu

Akinuukuu baadhi ya vifungu kutoka katika Biblia kwamba aitakae kazi ya uasikofu ataka kazi njema lakini asiwe ni mtu mwenye kulaumiwa na wengine uongozi si jambo jepesi hivyo ni vema kuhubili amani ili kanisa liwe na amani na nchi pia iwe na amani

Pinda ameongeza kuwa Nchi hii wala Serikali yake havina dini na itaeendelea hivyo japo wananchi wake wana dini wanazotaka kuzitumikia hivyo basi amewataka viongozi wa dini kutoingiza siasa katika dini zao ila wasiwakataze waumini wao kuwa na vyama wanavyopenda kushabikia