Pages

Ads 468x60px

Friday, June 27, 2014

IMMANUELI MGOGO AWACHEFUA MAPRODUCER WA MKOA WA MBEYA,


WAMEDAI  AME WADHARAU NA KUWADHALILISHA  SANA, BITI ZA NYIMBO ZAKE AMETENGENEZA KATIKA STUDIO ZA MBEYA ADAI NI DAR-ES-SALAM
                               EMMANUELI MGOGO KATIKA ALBAM YA MSIKILIZE MUNGU
 NAMBA YA MAWASILIANO NA IMAIL YAKE VINAVYO ONESHA SI ALBAM  SI YA SAYUNI BAND BALI NA YAKE BINFSI
     TASWILA NDANI YA DVD YAKE INAVYO ONESHA VEDEO NA OUDIO  IMEREKODIWA WAPI 

KWA UNDANI WA HABARI HII SOMA HAPA CHINI


IMMANUELI MGOGO AWACHEFUA  MAPRODUCER WA MKOA WA MBEYA,

WAMEDAI  AME WADHARAU NA KUWADHALILISHA  SANA, BITI ZA NYIMBO ZAKE AMETENGENEZA KATIKA STUDIO ZA MBEYA ADAI NI DAR-ES-SALAM

Baadhi ya wamiliki wa studio  na waandaaji wa nyimbo za injili mkoani hapa wamemlalamikia mwambaji anae chipukia wa njimbo za injili EMMANUELI MGOGO kwa kitendo alicho kifanya cha  kuandika jina la Studio  ECK PRODUCTION ya jijini Dar-es-salaam  kwamba ndiyo iliyorekodi nyimbo zilizomo katika albam yake ya MSIKILIZE MUNGU wakati sikweli  nyimba hizo zimerekodiwakatika Studio za  hapa jijini Mbeya.

Hayo yamebainishwa na Produser wa Studio ya Braju Baraka Mwasambamba iliopo Airpot jijini hapa alipokua akiongea na mwandishi wa habari hizi, amekiita kitendo alichokifanya mwimbaji huyo si cha uungwana na hakina ustaarabu na hekima  ndani yake kwani ni kuudharau mkoa wa mbeya.

“Mwandishi kwanza ninasikitika sana kwa jinsi alivyo tudhalilisha Immanueli Mgogo  sisi waandaaji wa nyimbi mkoani hapa, mimi nimetengeneza Bit ya wimbo wa Msikilize Mungu, alikuja hapa na kwaya moja kwa lengo la kuwasaidia kurekodi  nilipotengeneza hiyo Biti kwa lengo la kuitengenezea hiyo kwaya yeye akasema naomba usiwape hawa ninaitaka niitungie maneno nikamkubalia” alibainisha Mwasambamba

Ameongeza kua baadae alikuja na kuaanza kuingiza maneno tukiwa wote hapa Studioni kwangu, tulipo maliza aliniomba aichukue data apelike Dar es salaam ampelekee mpiga kinanda amjazie maeneo yaliyo acha wazi mimi nilikubali nikampa hizo data nashangaa sana kuona ndani ya hiyo DVD  yake ameandika OUDIO imetengenezwa na ECK  PRODUCTION huu ni udhalilishaji.

Baraka amehoji kwamba kama kweli nyimbo hizo zomerekodiwa Dar es salaama anaweza kudhibitisha?, je wale waimbaji wanao mwitikia alikwenda nao huko ECK? Alihoji huku akiwa na jazba kwa jinsi alivyolipokea swala hilo, tunajua waimbaji wengi wa huku Mbeya wakiisha pata majini kidogo tu  hupenda kuhamia huko lakini si kututukana matusi watu wa mkoa huu kama huyu.

Kwa upande wake Producer  Peter Mbuba wa H Studio iyopo maeneo ya Isanga jijini hapa yeye kasema anamuachia Mungu kwa kitendo alichokifanyiwa na mwimbaji huyo kwani amesikitishwa sana baada ya kuona wimbo alioutunga Producer huyo na kuutengenezea Bit yake  anakuta anatukuzwa mtu mwingine.

“Mimi ndiye niliyetengeneza biti na maneno ya wimbo wa Niko ulieko nimeiga kutoka kwa mwimbaji wa Afrika kusini Rebeka Marope nashangaa leo hii naona katika cd yake kwamba imetengenezwa Dar es salaam na Studio ya ECK hii si sawa hata kama ameona Mbeya hakuna watengezaji bola angetengeneza huko”

Bwana, Mbuba ameongeza kwamba hata kama Mgogo atapinga haya yeye anao ushahidi wa nyimbo hizo ikiwa ni pamoja na biti za kinanda chake hakiingiliani na vinanda vingine anaweza kutoa ili kilinganishwe na huyo anaemwita ECK, wa Da es salaam  kwamba ndiye alie recod nyimbo hizo, kwakufanya hivyo ni sawa na kuukataa mkoa wake ulio mtoa.

Nao baadhi ya waimbaji aliokua akiimba nao katika albam ya kwanza iliyokua ikiitwa Iko wapi njia ya Sayuni Band kwa kutotaka kutajwa majina wamesema wao katika albam ya Msikilize mungu hawajahusishwa na kwamba hawajui imerecodiwa lini wapi na kwa gharama gani na hata mapato yake hatuyajui.

“Ukweli ni kwamba Mgogo katika Sayun bandi ni mwalimu tu na atabaki kua mwalimu sisi albam ya Msikilize mungu Hatujashilikiswa kwa hiyo si ya Sayuni Bandi hiyo ni yake kama mgogo na ndio mana ukiangali  Imeandikwa Immanueli mgaga hilo neon Sayun Bandi ameliweka tu wala si Sayuni Badi” Hyo yamesemwa na baadhi ya waimbaji wa Sayuni Bandi.

Awali mwambaji Immanueli mgogo amekua akijipatia umaarufu katika uimbaji wa nyimbo za injili ambapo mwanzoni mwa safari yake ya uimbaji ilianzaia katika Albam ya kwanza iliyoitwa Iko wapi njia iliyo kua chini ya Sayuni Band, albam hii ilitokea kutamba sana katika vymbo vya habari na hata katika matamasha mbalimbali, na kitu ambacho kimemfanya  atambulike ndani na nje ya mkoa wa Mbeya

Kama ilivyo kawaida ya baadhi ya watu wanapo pata nafasi ya kupata umaarufu kidogo husahau aliko toka na kujiona mafanikio hayo yamekuja kwa nguvu na juhudi za akili zake na kusahau msemo wa wahenge uliokua ukisema ukimuona kobe juu ya mti ujue kapandishwa.

Thursday, June 26, 2014

WAJUMBE WA BARAZA KUU NA MKUTANO MKUU WA CHADEMA WAENDA KWA MSAJIRI WA VYAMA VYA SIASA NA KWA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA UBADHIRIFU WA FEDHA ZA CHAMA UNAO WAHUSISHISHA VIONGOZI WA CHAMA HICHO.


 Wanachama na Viongozi wa Chadema wakiwemo wa Baraza Kuu la chama hicho, wakipiga kwata kuelekea Ofisi za Msajili wa Vyama vya Siasa, jijini Dar es Salaam, leo, kupeleka barua ya kumuomba Msajili huyo wa vyama, kuwataka viongozi wa ngazi ya juu wa Chadema kuzingatia Katiba ikiwemo kuitisha kikao cha Baraza Kuu na kuzingatia matumizi bora ya fedha za Chama.
 Mjumbe wa Baraza Kuu Chadema ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya Temeke Joseph Yona (kushoto) akiongoza wenzake kuingia Ofisi ya Msajili wa Vyama leo kuwashitaki viongozi wa ngazi ya juu wa chama hicho kwa kudaiwa kutotekeleza Demokrasia na kufuata Katiba ndani ya Chama
 Yona akisaini kitabu cha wageni kwenye kwenye mapokezi ya Ofisi ya Msajili wa Vyama Jijini Dar es Salaam, alipowasili ya ujumbe wake. Kulia kwa Yona ni Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kaliua mkoani Tabora ambaye ni Mjumbe wa  Baraza Kuu na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Chadema, Jorum Mbogo
 Naibu Msajili wa vyama vya Siasa Nchini akimkaribisha Yona na msafara wake.


 Wanachama waliofuatana na wajumbe wa Baraza Kuu Chadema wakisubiri kuwasisha barua yao kwa Mkuu wa Masijala wa Ofisi ya Msajili wa vyama.
 Yona akionyesha abarua ambayo baadaye aliikabidhi masijala kwa ajili ya kumfikia Msajili wa vyama
 Yona akikabidhi barua yao, kwa Mtunza kumbukumbu Mkuu wa Ofisi ya Msajili wa vyama, Jihadhari Saidi.
 Yona akizungumza nje ya Ofisi ya Msajili baada ya kuacha barua yao kwa Msajili wa Vyama
  Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kaliua mkoani Tabora ambaye ni Mjumbe wa  Baraza Kuu na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Chadema, Jorum Mbogo akisoma taarifa yao kabla ya kwenda kwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali baadaya ya kutoka kwa Msajili ya vyama
 Baadhi ya wanachama wanaodaiwa kuwa wa Chadema wakiwa na mabango nje ya Ofisi ya Msajili wa vyama
 Mamilioni ya ruzuku yanayeyukia wapi? Bango linauliza
 Eti Bora Chadema ife kuliko Mbowe kutapeli?
 Chadema wakiomba msaada kwa Msajili wa vyama
 Ujumbe mzito kwa Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe
   Wanachama na Viongozi wa Chadema wakiwemo wa Baraza Kuu la chama hicho, wakiwa nje ya Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali leo kupeleka maombi ya kutaka Mkaguzi huyo wa Hesabu za serikali kufanya ukaguzi wa hesabu wa Chadema kwa madai kwamba viongozi wa ngazi za juu wanazitafuna


Friday, June 20, 2014

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI DEBORA SAID AFARIKI DUNIA

Kwa kupitia Facebook Accout, Rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania Addo Novemba amepost habari za kifo cha mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania Debora Said na hivi ndivyo alivyoandika, "Pigo Tena kwa Tasnia ya Muziki wa Injili, ninayo huzuni kubwa kuwatangazia Kifo cha Mwenzetu Deborah Said aliyefariki Muhimbili..naomba ushirikiano katika kipindi kigumu, kwa kuwa nipo nje ya Dar nikijiandaa kurudi nimeshamtuma Mhe Cosmas Chidumule aunganishe wanamuziki wote..Bwana Ametwaa, Tuonane Milele Tuonane Bandarini Pale!"
Marehem Debora Said enzi za uhai wake
Rumafrica imepokea kwa masikitiko makubwa sana juu ya kifo cha Debora, tunawapa pole wafiwa na Watanzania wote na kupotelewa na mtumishi wa Mungu ambaye amefanya kazi yake kwa upendo na uaminifu. Mungu azidi kuipigania familia yake na wale wote waliokuwa wakimtegemea kiroho na kimwili. Kazi ya Mungu daima haina makosa, tuzidi kumtumikia Mungu sisi tuliobaki kwani hatujui vilivyombele yetu.
 Huu ni wakati wa kuungama na kutubu makosa tunayoyafanya katika maisha yetu hapa dunia, siku ya mwisho tutatupwa jehanamu kama tukizidi kumsahau Mungu. Mungu amekupa kipaji fulani kwa kazi yake basi kitumia na usiache. Debora amefanya kazi ya Mungu kwa njia ya uimbaji na sasa Mungu amemchukua akampongezi kwa kile amekifanya duniani.

Dada Debora baada ya oparesheni



Hapa mama mchungaji, Debora John akimsifu Mungu, huku akienda sambamba na Mch. John Bagenyeka

SOO LA MUMEWE KUPANDISHWA MAHAKANI...FLORA MBASHA APATWA NA AIBU

 Shetani ukimtumikia kwa sili ipo siku atakuumbua tu,

wakati jana mumewe Emmanuel Mbasha (32) akipandishwa kizimbani kwa mara ya pili kwa soo la ubakaji wa shemejiye, mwimba Injili kinara Bongo, Flora Mbasha (31) amepitia katika hatua tatu za aibu, Ijumaa lina ripoti kamili.

Mwimba Injili kinara Bongo, Flora Mbasha akiwa na mumewe Emmanuel Mbasha.
Mbasha ambaye naye ni mwimba Injili na mfanyabiashara alitarajiwa kupandishwa kizimbani jana kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Ilala, Dar akitokea mahabusu Keko akikabiliwa na mashtaka mawili ya ubakaji wa shemejiye mwenye umri wa miaka 17.
Habari kutoka kwa mtu wa karibu wa Flora ambaye alihama nyumbani na kwenda kuishi hotelini maeneo ya Sinza, Dar, kitendo hicho kilimuingiza staa huyo kwenye hatua ya tatu ya aibu na kujikuta akiwa katika masikitiko makubwa.
AIBU YA KWANZA
Kwa mujibu wa mtu huyo wa karibu aliyeomba hifadhi ya jina, aibu ya kwanza inayomuuma Flora ni ile ya ndoa yake kuingia kwenye gogoro kisha kudaiwa kutengana na mumewe kinyume na kile anachokihubiri kupitia nyimbo zake zinazopendwa na wengi ndani na nje ya Bongo.



Binti wa miaka 17 anayedaiwa kubakwa na mume wa mwimbaji wa nyimbo za injili Bongo Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha.
“Unajua lile neno la ‘mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake, bali mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe’ (Mithali 14:1) linamfanya awe na aibu mbele za watu.
“Unaambiwa kanisani (anasali Kanisa la Ufufuo na Uzima la Mchungaji Josephat Gwajima kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers, Dar) anaona aibu hasa kwa waumini wenzake.

“Flora amedumu na Ima (Mbasha) kwenye ndoa kwa miaka 12 hivyo kutokea kwa kilichotokea ni aibu kwani tayari walikuwa wamekomaa tofauti na walipoona wakiwa na umri mdogo.
“Hebu fikiria, mtoto amekuwa mkubwa, anaposikia mama ana matatizo na baba si ni aibu jamani? Cha msingi tuwaombee wamalize matatizo yao, inaweza kusaidia kuifuta aibu hiyo kwani imeandikwa ‘Ndoa na iheshimiwe na watu wote...’ ( Waebrania 13 : 4 -),” alisema mnyetishaji wetu akisisitiza kuwa akitajwa gazetini ataonekana mvujishaji wa mambo ya siri ya wanandoa hao.

AIBU YA PILI
Chanzo hicho kiliendelea kutiririka kuwa aibu ya pili inayomkabili Flora ni skendo ya yeye kudaiwa kuhamishia makazi kwa mchungaji wake, Gwajima.

Katika aibu hiyo, mumewe alinukuliwa na gazeti mama la hili, Uwazi akimlalamikia mchungaji huyo amwachie mkewe kwani yeye ndiye alisababisha sakarakasi zote hizo za ndoa yake.
Ilidaiwa kuwa kwa mke wa mtu achilia mbali mhubiri kwa njia ya nyimbo, kitendo cha kukumbwa na skendo nayo ni aibu pia.


Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima.
“Kwa mtumishi kutajwa kwenye jambo kama hilo lisilo na mrengo wa kupendeza masikioni mwa watu, ni aibu kuu,” kilidai chanzo hicho.
AIBU KUU YA TATU
Ilisemekana kuwa achilia mbali ndoa, mambo ya mchepuko lakini aibu kuu ya tatu kwa Flora, ni kashfa ya ubakaji wa shemejiye inayomkabili mumewe Mbasha.
“Unajua usifikirie kwamba mume akipata aibu mke anaweza kuikwepa. Hawezi kwa sababu ‘wanazungumza lugha moja’ (yaani ni mwili mmoja). Ona sasa mume anapandishwa kizimbani kwa ubakaji.


Mwimbaji wa nyimbo za injili Bongo Flora Mbasha
“Pia usifikiri watu watasema kashfa ni ya Ima peke yake. Kwanza hata kutamka watu wanasema mume wa Flora. Ikumbukwe aibu ya mume ni ya mke pia. Ni vigumu mno kwa Flora kusema aibu ni ya mumewe pekee,” alitiririka mto habari huyo.
FAMILIA ZATOFAUTIANA
Wakati hayo yakiendelea, habari zinadai kuwa familia za pande zote zinatofautiana huku kila moja ikilaumu nyingine.

Ilidaiwa kuwa upande wa Mbasha unamlalamikia mama wa Flora kuwa anamuunga mkono mwanaye badala ya kusaidia kutuliza hali ya hewa.
Ilielezwa kuwa upande wa Flora wao wanamlaumu Mbasha kwa madai kuwa chanzo cha yote ni mgawanyo wa mali hasa baada ya kuona kuwa hakuna tena ndoa.

Emmanuel Mbasha akiwa kwenye pozi.
FLORA ANASEMAJE?
Akizungumza na Ijumaa juzi kwa njia ya simu, Flora alitoa la moyoni: “Kweli naumia sana tena sana. Kwa sasa kesi ipo mahakamani, siwezi kuizungumzia lakini ndiyo hivyo. Siyo siri nateseka sana.”
Mbasha anadaiwa kumbaka ndugu wa Flora ambaye ni yatima kati ya  Mei 23 na 25, mwaka huu ambapo kesi yake inaendelea kuunguruma baada ya kukaa mahabusu ya Keko kwa siku kadhaa ambapo sheria ndiyo itakayoanika siri zote juu ya sakata hilo.
 
Mume wa Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha akipelekwa mahabusu ya
Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar.


                               Emmanuel Mbasha akifungiwa ndani ya mahabusu.
                        ...Askari Magereza akifunga mlango wa mahabusu.


Mbasha baada ya kutolewa kwenye mahabusu ndogo ya mahakamani
hapo alionekana mnyonge na aliyechoka hali iliyosababisha simanzi kwa ndugu na
jamaa zake waliokusanyika mahakamani hapo.
Baada ya kesi hiyo kutajwa, rafiki wa Mbasha
aliyejitambulisha kwa jina la George Mushi na baba wa mtuhumiwa huyo, Mwahimu
Juma walifanikiwa kutimiza masharti ya dhamana.



Wednesday, June 18, 2014

Kanisa la Moraviani ya zidi kupoteza asili yake,


Ni katika misingi,miongozo na taratibu zake kuiga kutoka  katika madhehebu mengine na kuacha kutunza na kudumisha tamaduni zetu na kuwa enzi  waasisi wa kanisa hilo.


 Kwaya ya vijana (A) kanisa la Moraviani ushirika wa Nzovwe katika mashindano ya mtaa wa mbeya


  Kwaya ya Vijana (A) kanisa la Moraviani ushirika wa Mbeya mjini katika mashindano ya Mtaa wa Mbeya


 Kwaya ya Vijana (A) kanisa la Moraviani ushirika wa Itiji wakiimba katika mtaa wa mbeya 




            Kwaya ya Vijana (A) Kanisa la Moraviani Ushirika wa Mabatini




Kwaya ya Vijana (A) kanisa la Moraviani ushirika wa Meta wakiwa katika shughuli ya kushindana kaika mashindano ya Mtaa wa Mbeya


Huu ni mtazamo wangu Juu ya Kanisa la MORAVIANI Soma hapo chini

 Na Charles Abraham

Kanisa la Moravian yazidi kupoteza asili yake,

Ni katika misingi,miongozo na taratibu zake kuiga kutoka  katika madhehebu mengine na kuacha kutunza na kudumisha tamaduni zetu na kuwa enzi  waasisi wa kanisa hilo.

Nimekua nikitafakari kwa kina sana juu ya kanisa langu la Moravian Tanzania linaloitwa kanisa la Ndugu. Nikweli sipingani sana na msimamo na msemo huo kwamba ni kanisa la ndugu na ukweli unabakia kua ni kanisa la ndugu.

Kwa nini sipingani na msemo huo, ni kutokana na mfumo wake katika miongozo, taratibu, tamaduni zake na misingi asili. kweli ni ya kiu ndugu najivunia sana kuwa mmoja wa Ndugu, sijawahi jutia na wala sitajutia nina upenda sana Umoraviani wangu

Leo nimejitokeza katika ukurasa huu kutaka kujaribu kuangalia kwa kina na kwa akili zangu ndogo sana lakini kuna vitu navikumbuka katika kumtu mikia Mungu nikiwa katika kipande hiki cha kanisa la Moraviani kabla na baada ya kua muumini  wa imani hii.

Nachelea kusema haya, kwani nakumbuka siku nilipotakiwa kuwa mmoja wa waamini  wa kanisa hili kulikua na taratibu nyingi sana unazozipitia ili kujihakikishia kua mmoja wao wa watu wanaotakiwa kuwa washiriki halali na mwenye sifa na vigezo vya kuitwa huyu ni Mmoraviani mwenzetu.

Nakumbuka sana jinsi mzee wa kanisa alivyo heshimika na waumini wake tofauti na sasa, kwani yeye alikua na dhamana kubwa usipo muheshimu huyu wewe kupata huduma yoyote katika kanisa, usahau mpaka pale mzee wa kanisa akutambue na kukuwasilisha katika vikao harali vya maamuzi.

Najaribu kupitia mambo machache tu kati ya mengi yaliyokua msingi na msimamo wa kanisa lakini kwa sasa yameachwa na kujikuta kanisa la Moraviani linagongana katika baadhi ya mambo, Hebu kumbuka kwamba hapakua na maamuzi yoyote ambayo yaliamuliwa na mtu mmoja na kisha ya kaingia kwenye utekelezaji tofauti na sasa.

Kila jambo lilipitia katika vikao husika na kujadiliwa kwa kina na kisha kulitolea maamuzi ya pamoja na kuingia katika utekelezaji, na hapa mimi nadhani ndipo chimbuko la kauli hii ya Kanisa la ndugu kwamba hakuna alie juu ya mwingine wote sawa sawa, 

Leo hii watu wana msingizia Roho mtakatifu, kutaka kupitisha maamuzi yao utakuta mtu ama mtumishi akisema nime sukumwa na Roho nifanye hivi. Jamani Roho Mtakatifu gani amevunja utaratibu, na kuleta mgawanyiko na  manung`uniko kwa wengine? 

Siku moja nikiwa ndani ya moja ya ibada zetu katika taratibu za kawaida kama wamoraviani walivyo na taratibu za ibaada zao, Ilifika nafasi ya kufanya huduma ya watu walio jitenga kurudi kundini wale waliofuata taratibu za vikao waliitwa mbele kwa lengo la kutubu na kumrejea Mungu wao,

Nika sikia kwa masikio nakuona kwa macho yangu mchungaji akisema leo natoa promoshen kwa kila anaejua alijitenga ama amejitenga na kanisa  apite mbele ili tumrudishe kundini pamoja na hawa waliopita mbele, sikuamini masikio yangu kwamba hivi kanisa letu limefikia hapa kutoa promosheni?

Da! Nilishangaa sana pamoja na hilo siku nyingine nilisikia kiongozi mkubwa wa kanisa aliepewa dhamana ya kuliongoza kwanisa akasi mama mbele akasemea wale wote ambao hawaja okoka pita mbele tuwaongoze sala ya toba He! Hizi tamaduni ni za Moraviani kweli?

Naomba nieleweke siupingi wakovu nami pia nimeokoka, lakini napinga destuli za waokovu zisizo za kibiblia. Najaribu kuangalia tamaduni za Kimoraviani tangu mwanzo lilikuwepo hii? Kama halikuwepo tumelitoa wapi na liko wapi la kwetu? Wakuu wa kanisa hili naomba mnisidie maswali haya.

Ndugu zangu kila lililo kuwepo katika taratibu na tamaduni zetu awali lilikua na makusudi sana, kama tunataka kwenda na wakati tufanye hivyo pasipo kuharibu asili yetu, Ni kweli dunia imekua na utandawazi si kwa Moraviani tu, hata kwa makanisa mengine upo lakini wametunza asili yao.

Nakumbuka mwaka mmoja tukiwa katika maandalizi ya mkutano vijana (b) wa mtaa wa Mbeya mwaka fulani kulitokea ubishani  mkubwa sana ilipofika  agenda ya kumpata mtu wa kuja kukagua mashindano  katika idara ya uimbaji, baadhi ya watu wali pendekeza aje mwalim Chifupa, na dhani jina hili kwa Moraviani sana huku mbeya wanalikumbuka sana.

Swala hili lilipingwa vikali na baadhi ya viongozi katika kulipitisha jina hilo kila mmoja akitoa maoni yake kwamba wame choshwa na ukaguzi wake wengine wakidai alikua akipendelea baadhi ya kwaya kwakua amezifundisha yeye mwenyewe sana kwaya ya vijana uashirika wa mabatini.

Wengi walikubaliana na wazo hilo la kubadilisha waamuzi, na ndipo kikao hicho kilikubaliana kwenda katika chuo cha Kidugala seminali, kilichopo Mkoa Njombe  chuo hiki kina milikiwa na kanisa la Kilutel (KKKT) kwa makubaliano hayo walikuja wakaguzi kutoka huko wakakagua na kutoa matokea lakini haikua dawa yakumaliza ubishanibado lawama za  kupendelewa kwaya fulani ziliibuka tena.

Mwaka uliofuata maandalizi ya uimbaji kwaya nyingi zilikwenda kutafuta waalimu wa nyimbo kutoka makanisa ya Kiluteli, Huo ukawa mwanzo wa kupoteza asili ya uimbaji wa kimoraviani katika kwaya za vijana mpaka leo hii ninapo andika Tahariri hii nina sikitika na kufadhaika sana moyoni.

Nenda katika shirika mbalimbali za hapa mjini kajionee kwaya nyingi zimecha asili uimbaji wake  kama hawajaiga uimbaji wa kasikazini magharibi basi utakuta wanaimba Kiluteli jamani nani katuloga wa Moraviani? Nini kinasukuma kuuchukia utamaduni na asili yetu mbona kuna wengi wanazipenda na kutukubali lakini tunaziacha bila sababu.

Kwanza ni siwe mchoyo wa fadhila kwa waalimu na waimbaji kwa baadhi ya kwaya kuu zilizo nyingi bado hazijaondoka sana katika maudhui ya ki Moraviani napenda kuwapa pongezi sana kwa kulinda U Moraviani wetu nataka kusema hakuna wa kufanana na Moaraviani.

Kuna siku nilipata nafasi ya kuongea na mmoja viongozi wa kanisa letu nilimuuliza mambo mengi kuhusiana na maswali yangu haya, alinipa jibu jepesi sana ambalo mpaka leo najiuliza kanisa lipo kwa ajili ya watu au watu wapo kwa ajili ya kanisa?

“Unajua mtumishi siku hizi hatupendi kuwalazimisha waumini kufata sana sheria ukifuata sana ngumu waumini wata kukimbia wote na kwenda makanisa mengine na kubakia na kanisa tupu, kwa hiyo tunajaribu kulegeza kidogo mashart ili tuendelee kuwa na waumini wetu wasiondoke” mwisho wa kumnukuu

Ewe mtumishi wa mungu unashindwa kusimamia misingi na taratibu za kanisa na kusema kweli ya mungu kwa kuogopa waumini watakukimbia kweli? Hivi ukija kutana na Babu yetu JOHN HUSS utakuja kumjibu upuuzi huo unaonieleza mimi umeujaza katika kicha chako na kuacha kanisa linateketea na kuelekea kusiko julikana? umesahau ulikubali dhamana na kiapa chako mbele za kanisa na Mungu kwamba utalinda na kuheshimu taratibu za kanisa.

Sitaki kuonekana nahukumu ila nataka kutoa maoni yangu kwenu Wachungaji na viongozi wa kanisa la Moraviani mliopo zamu kwa sasa jiandaeni kujibu maswali mbele za Mungu  mlipolifikisha kanisa lake kwani ninayo imani kila mlipandalo mtalitolea hesabu mbele zake.

Nikajaribu kuangalia taratibu za kanisa lingine kama vile Roman catholic lenye taratibu ngumu tangu mwanzo wa kanisa mpaka sasa waumini wake wanazifuata hadi leo bila kujali wala kukimbiwa na waumini wao mpaka leo hii na wanaendelea kujaa kuliko hata sisiwa Moraviani Tunaojiita kanisa la Ndugu.

Ninayo mengi moyoni mwangu juu ya kanisa langu kwani sikukosea kuwa muamini wake naumia kuona mambo yakienda kombo kwani imani yangu ya kuuona ufalme wa mungu nimeiweka Moraviani naogopa nikashindwa ufikia uzima wa milele kwa kusahau majukumu na miongozo yake.
              
 Usikose toleo lijalo,  
Mwisho