Pages

Ads 468x60px

Monday, October 27, 2014

Timu ya Mbeya city mambo yanazidi kuwaendea kombo Yachezea kichapo na Mtibwa suger,



Mashabiki wamtaka Kocha wa timu hiyo Juma mwambusi kujiuzuru.
 Kocha Mbeya city Juma mwambusi akiongea na vyombo vya habari (Picha na maktaba yetu)

              Timu zote mbili zikiingia uwanjani kisha kukaguliwa nakuanza mtanange



                                    Kila timu zikifanya Dua kwaimani yake






                                      Mashabiki waliojitokeza kushangilia timu yao

















                        Tazama katika habari picha jinsi mchezo huo ulivyo kwenda
Baada ya kufungwa gori la pili mashabiki wakaanza kurusha mawe na makopo ya maji uwanjani

              Baadhi ya wachezaji na mashabiki wakitoka uwanjani wakilia machozi


                                                           Habari soma hapa
Na, Charles Abraham


Timu ya Mbeya city mambo yanazidi kuwaendea kombo Yachezea kichapo na Mtibwa suger,
Mashabiki wamtaka Kocha wa timu hiyo Juma mwambusi kujiuzuru.

Ni siku chache zimepita tangu timu ya Mbeya city iendeleze uteja kwa wana lambalamba Azam fc wa jijini dare s slaam kwa kuchapwa gori 1-0 na kuwatia machungu mashabiki wake ambao msimu uliopita walikua wakisherehekea raha za ushidi.

Jana tena timu hiyo imeendelea kuwanyima raha mashabiki hao kwa kuchezea kiminyo cha bila huruma 2-0 kutoka kwa wakata miwa Mtibwa Suger ya mjini Morogoro na kuwafanya wacharuke na kurusha mawe ndani ya uwanja baada ya kupachikwa bao la pili.
Mashabiki hao wakiongea kwa nyakati tofauti wamemtaka kocha wa timu hiyo Juma mwambusi kuchukua hatua ya kujiuzuru kutokana na kuwa yeye ndiye chanzo cha matokeo na mwenendo mbovu wa timu yao.

Akiongea moja wa mashabiki hao Razalo Mgwenda huku akitokwa machozi ameutaka uongozi kuchukua hatua za makusudi haraka iwezekanivyo kuongea na wachezaji kujua nini tatizo ili kuinusuru timu hiyo kabla haijafikia pabaya zaidi.

“Mimi nimechoshwa na kila wikiendi kuumizwa kichwa kwa kuja kushangilia timu yangu lakina haifanyi vizuri kila siku inafungwa kuanzia leo siji tena huku siko tayali kukosa raha kwani timu yenyewe haitupi hata nafuu ni kutuumiza tu” amesema shabiki huyo.

Pamoja na hayo kumekua na tetesi kutoka wadau hao wakiendelea kumtupia lawama Juma mwambusi kwa kuwapanga wacheza kwa manufaa yake binafsi, wamesema kuwa endapo mchezaji hakumpatia asilimia fulani ya posha yake hawezi kupewa nafasi ya kucheza.

Katika malalamiko hayo inasemekana wachezaji wenye uwezo hawakubaliani na hilo hivyo hawampatii posha hiyo kwa kuringia uwezo walionao na ndipo hawapangwi na ikitokea kacheza basi ni hucheza dakika chache za mwisho wa mchezo.

Kwa upande wake kocha huyo ameyapokea matokeo hayo kwani amekiri na kuona umuhimu wa kukaa na wachezaji wake ili kuangalia ni nini kilicho wapata msimu huu kwa kua hii ni mchezo wa pili wanapoteza wakiwa kiwanja cha nyumbani.

“ Nikweli nimepokea matokeo haya kwauchungu sana kuna haja kubwa kukaa na wachezaji wangu kuangali nini kimetokea kwakuwa hii ni mechi ya pili tunapoteza tukiwa nyumbani kitu ambacho hakijazoeleka Tutakaa chini Tujipange tuone cha kufanya” Amesma mwambusi

Nae kocha wa Mtibwa Suger Mecky mexime amekiri kuwa mechi anazo kutana nazo ni ngumu lakini wamejipanga vizuri amewasifia wachezaji wake kuwa wana hali ya kushinda nakwamba nafasi waliyopata wamezitumia vizuri  na ndio maana  wamepata matokeo hayo.

                                                                             MWISHO




   

Wednesday, October 22, 2014

Kandoro azindua muungano wa makampuni matatu katika sekta ya kilimo na kuyataka yawe na mikataba itakayowanufaisha wakulima Nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abass Kandoro akiongea na wana mkutano uliofanyika katika ukumbe wa Mtenda Soweto
                 Mkurugenzi wa Kampuni ya Mtenda Kyela Rice co. LTD George Mtenda
                                  Mwenyekiti wa bod Stela Mtagwaba akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi
             Kwa niaba ya wakulima Oden Simkwai kutoka wilayani Momba akisoma Risala




                                           Baadhi ya wakulima waliohudhulia mafuzo hayo

Burudani kutoka kikundi cha Awilo kilimfanya mkuu wa mkoa kushuka jukwani na kumtunza mtoto aliekua kivutio kwa wana mkutano

Wajumbe katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro
Mchele Safi wa kyela kutoka kampuni ya usindikaji na uuzaji ya Mtenda Kyela Rice co (LTD)


                                                                         SOMA HAPA
NA, Charles Abraham


Kandoro azindua muungano wa makampuni matatu katika sekta ya kilimo na kuyataka yawe na mikataba itakayowanufaisha wakulima Nchini.

Katika kutekeleza kauli mbiu ya  kilimo kwanza, makampuni matatu yameunganisha nguvu ya pamoja ili kuimarisha na kuwasaidia wakulima  kukuza kipato  na uchumi katika sekta hiyo.

Shilikisho hilo lililozinduliwa likiambatana na  mafunzo ya kilimo bora cha mpunga kwa wakulima  limeziunganisha kampuni ya Mtenda Kyela rice co. LTD, Tanseed International na Yara (MTAYArF)

Akiongea katika uzinduzi huo Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro ameyataka makampuni yaweze kuwanufaisha wakulima katika mikataba watakayo kua wakiingia nao isiwe ya kuwakandamiza na hivyo kushindwa kunufaika na misaada pamoja na mafunzo mnayo wapatia.

“Nawapongeza sana wakurugenzi wa kampuni hizi tatu kwa kuchukua uamuzi wa kuunganisha nguvu ya pamoja katika kuendeleza shughuri za kilimo nchini, ninawaomba kupitia makampuni yenu muwasaidie wakulima kujiunga katika vikundi ili nao wawe na nguvu ya kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo cha kisasa” Amesema Kandoro

Ameongeza kuwa pamoja na umoja huo na kwa manufaa kwa kuwasidia wakulima kwa kuangalia mikataba ikae vizuri isiwe ya kuwandamiza bali iwe yenye kuwasaidia ili kujikwamua kiuchumi na kuleta maendeleo katika familia zao, pamoja na hayo serikali imekuwa ikitoa mchango wake kwa kwajengea miundo mbinu bora.

Kwa upande wake mmoja wawakulima Odeni Simkwai toka msangano Wilaya Momba amepongeza sana kampuni ya Mtenda rice kwa mchango wake na misaada kwa wakulima kwani limewanufiasha kwa pembejeo na bei nzuri kwa ununuzi wa mazao yao.

Awali akisoma Risara kwa mgeni rasmi Stela Mtagwaba mwenyekiti wa bodi hiyo amesema lengo la shilikisho hilo ni kupambana na changamoto wanazokutana nazo ikiwa ni ukosefu wa masoko ya uhakika, uzalishaji mdogo na ubora usiolidhisha.

“Ni vizuri ukajua lengo la shilikisho hili  utakalolizindua hivi punde japo kwa ufupi, kampuni hizi tatu pamoja na wakulima wa mpunga zimebaini vikwazo katika kilimo cha mpunga ikiwa ni kutojua mbinu za kilimo cha kisasa, pamoja na kutotumia mbegu bora, pia hawajui sayansi ya udongo,

Ameongeza kuwa kwa kuona hayo kampuni ya ununuaji wa mpunga, usindikaji na uuzaji wa mchele Mtenda Kyela rice, kampuni ya mbegu bora Tanseed International, Kampuni ya mbolea ya Yara na wakulima wa mpunga wa Kyela,Mbarali na Momba wameamua kuunda umoja huu ili kuunganisha nguvu ya pamoja katika kuleta maendeleo yao.  


                                                   MWISHO