Thursday, October 30, 2014
Monday, October 27, 2014
Timu ya Mbeya city mambo yanazidi kuwaendea kombo Yachezea kichapo na Mtibwa suger,
Mashabiki wamtaka Kocha wa timu hiyo
Juma mwambusi kujiuzuru.
Kocha Mbeya city Juma mwambusi akiongea na vyombo vya habari (Picha na maktaba yetu)
Timu zote mbili zikiingia uwanjani kisha kukaguliwa nakuanza mtanange
Kila timu zikifanya Dua kwaimani yake
Mashabiki waliojitokeza kushangilia timu yao
Tazama katika habari picha jinsi mchezo huo ulivyo kwenda
Baada ya kufungwa gori la pili mashabiki wakaanza kurusha mawe na makopo ya maji uwanjani
Baadhi ya wachezaji na mashabiki wakitoka uwanjani wakilia machozi
Habari soma hapa
Na, Charles Abraham
Timu ya Mbeya city mambo yanazidi
kuwaendea kombo Yachezea kichapo na Mtibwa suger,
Mashabiki wamtaka Kocha wa timu hiyo
Juma mwambusi kujiuzuru.
Ni siku
chache zimepita tangu timu ya Mbeya city iendeleze uteja kwa wana lambalamba
Azam fc wa jijini dare s slaam kwa kuchapwa gori 1-0 na kuwatia machungu
mashabiki wake ambao msimu uliopita walikua wakisherehekea raha za ushidi.
Jana tena
timu hiyo imeendelea kuwanyima raha mashabiki hao kwa kuchezea kiminyo cha bila
huruma 2-0 kutoka kwa wakata miwa Mtibwa Suger ya mjini Morogoro na kuwafanya
wacharuke na kurusha mawe ndani ya uwanja baada ya kupachikwa bao la pili.
Mashabiki
hao wakiongea kwa nyakati tofauti wamemtaka kocha wa timu hiyo Juma mwambusi
kuchukua hatua ya kujiuzuru kutokana na kuwa yeye ndiye chanzo cha matokeo na
mwenendo mbovu wa timu yao.
Akiongea moja
wa mashabiki hao Razalo Mgwenda huku akitokwa machozi ameutaka uongozi kuchukua
hatua za makusudi haraka iwezekanivyo kuongea na wachezaji kujua nini tatizo ili
kuinusuru timu hiyo kabla haijafikia pabaya zaidi.
“Mimi
nimechoshwa na kila wikiendi kuumizwa kichwa kwa kuja kushangilia timu yangu
lakina haifanyi vizuri kila siku inafungwa kuanzia leo siji tena huku siko
tayali kukosa raha kwani timu yenyewe haitupi hata nafuu ni kutuumiza tu”
amesema shabiki huyo.
Pamoja na
hayo kumekua na tetesi kutoka wadau hao wakiendelea kumtupia lawama Juma
mwambusi kwa kuwapanga wacheza kwa manufaa yake binafsi, wamesema kuwa endapo mchezaji
hakumpatia asilimia fulani ya posha yake hawezi kupewa nafasi ya kucheza.
Katika
malalamiko hayo inasemekana wachezaji wenye uwezo hawakubaliani na hilo hivyo
hawampatii posha hiyo kwa kuringia uwezo walionao na ndipo hawapangwi na ikitokea
kacheza basi ni hucheza dakika chache za mwisho wa mchezo.
Kwa upande
wake kocha huyo ameyapokea matokeo hayo kwani amekiri na kuona umuhimu wa kukaa
na wachezaji wake ili kuangalia ni nini kilicho wapata msimu huu kwa kua hii ni
mchezo wa pili wanapoteza wakiwa kiwanja cha nyumbani.
“ Nikweli
nimepokea matokeo haya kwauchungu sana kuna haja kubwa kukaa na wachezaji wangu
kuangali nini kimetokea kwakuwa hii ni mechi ya pili tunapoteza tukiwa nyumbani
kitu ambacho hakijazoeleka Tutakaa chini Tujipange tuone cha kufanya” Amesma
mwambusi
Nae kocha
wa Mtibwa Suger Mecky mexime amekiri kuwa mechi anazo kutana nazo ni ngumu lakini
wamejipanga vizuri amewasifia wachezaji wake kuwa wana hali ya kushinda nakwamba
nafasi waliyopata wamezitumia vizuri na
ndio maana wamepata matokeo hayo.
MWISHO
Wednesday, October 22, 2014
Kandoro azindua muungano wa makampuni matatu katika sekta ya kilimo na kuyataka yawe na mikataba itakayowanufaisha wakulima Nchini.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abass Kandoro akiongea na wana mkutano uliofanyika katika ukumbe wa Mtenda Soweto
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mtenda Kyela Rice co. LTD George Mtenda
Mwenyekiti wa bod Stela Mtagwaba akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi
Kwa niaba ya wakulima Oden Simkwai kutoka wilayani Momba akisoma Risala
Baadhi ya wakulima waliohudhulia mafuzo hayo
Burudani kutoka kikundi cha Awilo kilimfanya mkuu wa mkoa kushuka jukwani na kumtunza mtoto aliekua kivutio kwa wana mkutano
Wajumbe katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro
Mchele Safi wa kyela kutoka kampuni ya usindikaji na uuzaji ya Mtenda Kyela Rice co (LTD)
SOMA HAPA
NA, Charles Abraham
Kandoro azindua muungano wa makampuni matatu katika sekta ya kilimo na kuyataka yawe na mikataba itakayowanufaisha wakulima Nchini.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mtenda Kyela Rice co. LTD George Mtenda
Mwenyekiti wa bod Stela Mtagwaba akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi
Kwa niaba ya wakulima Oden Simkwai kutoka wilayani Momba akisoma Risala
Baadhi ya wakulima waliohudhulia mafuzo hayo
Burudani kutoka kikundi cha Awilo kilimfanya mkuu wa mkoa kushuka jukwani na kumtunza mtoto aliekua kivutio kwa wana mkutano
Wajumbe katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro
Mchele Safi wa kyela kutoka kampuni ya usindikaji na uuzaji ya Mtenda Kyela Rice co (LTD)
SOMA HAPA
NA, Charles Abraham
Kandoro azindua muungano wa makampuni matatu katika sekta ya kilimo na kuyataka yawe na mikataba itakayowanufaisha wakulima Nchini.
Katika kutekeleza
kauli mbiu ya kilimo kwanza, makampuni
matatu yameunganisha nguvu ya pamoja ili kuimarisha na kuwasaidia wakulima kukuza kipato na uchumi katika sekta hiyo.
Shilikisho
hilo lililozinduliwa likiambatana na mafunzo ya kilimo bora cha mpunga kwa wakulima
limeziunganisha kampuni ya Mtenda Kyela
rice co. LTD, Tanseed International na Yara (MTAYArF)
Akiongea
katika uzinduzi huo Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro ameyataka makampuni
yaweze kuwanufaisha wakulima katika mikataba watakayo kua wakiingia nao isiwe
ya kuwakandamiza na hivyo kushindwa kunufaika na misaada pamoja na mafunzo
mnayo wapatia.
“Nawapongeza
sana wakurugenzi wa kampuni hizi tatu kwa kuchukua uamuzi wa kuunganisha nguvu
ya pamoja katika kuendeleza shughuri za kilimo nchini, ninawaomba kupitia
makampuni yenu muwasaidie wakulima kujiunga katika vikundi ili nao wawe na
nguvu ya kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo cha kisasa” Amesema Kandoro
Ameongeza kuwa
pamoja na umoja huo na kwa manufaa kwa kuwasidia wakulima kwa kuangalia mikataba
ikae vizuri isiwe ya kuwandamiza bali iwe yenye kuwasaidia ili kujikwamua
kiuchumi na kuleta maendeleo katika familia zao, pamoja na hayo serikali imekuwa
ikitoa mchango wake kwa kwajengea miundo mbinu bora.
Kwa upande
wake mmoja wawakulima Odeni Simkwai toka msangano Wilaya Momba amepongeza sana
kampuni ya Mtenda rice kwa mchango wake na misaada kwa wakulima kwani limewanufiasha
kwa pembejeo na bei nzuri kwa ununuzi wa mazao yao.
Awali akisoma
Risara kwa mgeni rasmi Stela Mtagwaba mwenyekiti wa bodi hiyo amesema lengo la
shilikisho hilo ni kupambana na changamoto wanazokutana nazo ikiwa ni ukosefu
wa masoko ya uhakika, uzalishaji mdogo na ubora usiolidhisha.
“Ni vizuri
ukajua lengo la shilikisho hili utakalolizindua hivi punde japo kwa ufupi, kampuni
hizi tatu pamoja na wakulima wa mpunga zimebaini vikwazo katika kilimo cha mpunga
ikiwa ni kutojua mbinu za kilimo cha kisasa, pamoja na kutotumia mbegu bora,
pia hawajui sayansi ya udongo,
Ameongeza
kuwa kwa kuona hayo kampuni ya ununuaji wa mpunga, usindikaji na uuzaji wa
mchele Mtenda Kyela rice, kampuni ya mbegu bora Tanseed International, Kampuni
ya mbolea ya Yara na wakulima wa mpunga wa Kyela,Mbarali na Momba wameamua
kuunda umoja huu ili kuunganisha nguvu ya pamoja katika kuleta maendeleo yao.
MWISHO
Subscribe to:
Posts (Atom)