MBUNGE MARY MWANJELWA
AKANUSHA KUHAMA CCM
Mbunge wa
viti maalum mbeya mjini kupitia chama cha mapinduzi ccm MARY MWANJELWA
amekanusha uvumi ulioenezwa na chombo kimoja cha habari kuwa anategemea
kukihama chake cha ccm na kuenda chama cha Demokrasia na maendeleo (chadema)
Kwa kile alichodai kuwa Rais amewachagua wabunge wageni na kuwapa uwaziri hivyo
kuwa dhalilisha wale wa zamani.
Hayo
ameyasema leo katika kikao chake na wandishi wa habari kilichofanyika katika
ukumbi wa ccm mkoa, nakuongeza kuwa hana
mpango wala hategemei kukihama chama chake hicho kwani yeye amechaguliwa
kutetea wananchi wa mbeya hivyo hawezi kuwasaliti.
Hata hivyo
amesema ataendelea na ubunge kwa muda wote uliosalia wa miaka mitatu kwani
mpaka sasa amewatumikia wananchi wake kwa muda wa miaka miwili tu hivyo anategemea
kugombea tena muhura ujao wa uchaguzi ili kutetea kiti chake.
Kikao hicho
kimehudhuliwa na viongozi mbalimbali wa chama cha mapinduzi ccm akiwepo katibu
HERENA SHIMBUSHO, Katibu umoja wa wananwake(UWT) mkoa TABU LUNGWESA, katibu
wilaya ya mbeya mjini RAYMOND SITIVINI pamoja na katibu mwenezi mkoa BASHIRU
MADODI.
Waandishi wa habari wakimsikiliza MARY MWANJELWA Akikanusha kukihama chama chake cha ccm.
0 comments:
Post a Comment