Pages

Ads 468x60px

Monday, September 11, 2017

WAFUGAJI WA KIMASAI WAONDOA MIGOGORO NA WAKULIMA KWA KUWEKA MIUNDO MBINU RAFIKI YA MALISHO

WA PILI KUSHOTO MWANEKITI WA KIJIJI CHA MATEBETA BAADHI YA WAASISI WA KIJIJI HICHO

MWANDISHI WA HABARI RASHIDI MKWINDA AKIONGEA JAMBO KATIKA MKUTANO NA WANA KIJIJI
MWANDISHI WA HABARI LAUDENCE SIMKONDA AKIMUHOJI MAMA MCHUNGAJI ELIZA SAILENI

NAMNA YA SALAMU ZA KABILA LA WAMASAI






WANAWAKE WA KIMASI WANUFAIKA NA MRADI WA MAJI NA KUPUNGUZA ADHA YA KWENA MWENDO MLEGFU KUPATA MAJI


MIFUGO IKIFURAHIA KUNYWA MAJI KATIKA MABILIKA YALIYOJENGWA NA WANAKIJIJI


                                WAFUGAJI WAKIPATA MAJI SAFI NA SALAMA




Na Laudence Simkonda, Mbeya.

ZAIDI ya Wafugaji elfu Tatu Miatano wa Jamii ya Kimasai  Kijiji cha Matebete wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya, wameamua kuthibiti migogoro ya ardhi ya mara kwa mara na Wakulima kwa kujiwekea  mikakati  ya ufugaji wenye tija kwa kupunguza mifugo na kuweka miundobinu rafiki kwa ajili ya malisho.

Kwa miaka mingi kumekuwepo na migogoro baina ya wakulima na Wafugaji kugombea maeneo ya Kilimo na Malisho ya mifugo katika maeneo mengi ya vijiji vya wilaya ya Mbarali ikiwemo kata ya Itambolewo. .

Matebete ni kijiji kilichopo ndani ya kata ya Itambolewo, amabacho kwa asilimia tisini kinakaliwa na wafugaji jamii ya Kimasai.

Wafugaji hao wanadai wamesema wanaeneo la ardhi lenye ukubwa wa ekari elfu 32,000 ambayo inamilikiwa kwa mjibu wa shereia, amabyo kwa sasa wanaendelea kuiwekea miundombinu rafiki kwa malisho.

Mwenyekiti wa kijiji  Julius Tissho na Mwasisi wa kijiji cha hicho cha Matebete Mzee Policarp Olekurupashi wamesema kuwa  kwanguvu zao wenyewe  wafaugaji wa kijiji cha Matebete, wamaeamua kwenda mbali zaidi kwa kuanza kuweka miundo mbinu ya maji, ikiwa ni pamoja na kujenga Mabirika  kwa ajili ya kunyweshea mifugo yao.

Kutokana na kijiji cha matebete kukabiliwa nachangamoto kubwa ya ukame, wafugaji wananlazimika kusafiri umbali mrefu kusaka maji na marisho, hali ambayo inachangia migogoro ya mara kwa mara baina yao na wakulima, hali ambayo inawafanya kuomba serikali kuunga mkono juhudi zao.

Kwaupande wake Afisa Mtendaji wa kijiji ncha Matebete, Sitengas Satullo, amesema kuwa tayari wafugaji wametumia zaidi ya shilingi milioni 50 katika ujenzi wa Mabirika matatu ya maji, na kudai kuwa kwa sasa mikakati inayofanywa na serikali ya kijiji ni kuzidi kuboresha miundombinu hiyo.

Kwa taarifa za Mwenyekiti wa kijiji hicho, Kijiji cha Matebete hadi sasa kinamifugo elfu tano, huku akibanisha kuwa lengo ni kuhakikisha mifugo haitoki nje ya kijiji hicho ili kuondokana kabisa na migogoro inayo wakumba.

MWISHO.


0 comments:

Post a Comment