Pages

Ads 468x60px

Monday, August 28, 2017

MBEYA WAKWAMA KUTEKELEZA AGIZO LA JPM.


RC Makalla ahaha, apiga marufuku
 Ma-dc, Ma-ded na Wakuu wa Idara kusafiri nje ya Mkoa
 
Na Moses Ng’wat,Mbeya.

 MKUU  wa Mbeya, Amos Makalla,
 amezuia  likizo na safari zote kwa Wakuu wa Wilaya,
 Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakuu wa Idara za Mkoa huo,
 baada ya kushindwa kuandaa mpango kazi wa kutekeleza dhana
 ya Viwanda, ambao ni kipaumbele cha serikali ya awamu ya
 Tano.

 Alitoa agizo hilo jana Wilayani Rungwe,
 wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani cha kupitia na kutoa
 majibu ya hoja za Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa hesabu za
 serikali (CAG).

 Makalla alifikia hatua hiyo, kutokana
 na makubaliayaliyofikiwa na viongozi hao June 2 mwaka huu,
 ambapo walipeana majukumu ya namna Mkoa huo utakavyotekeleza
 uanzishwaji wa viwanda.

 Mkuu huyo wa Mkoa alisema, katika hali
 ya kushangaza hadi kufikia sasa hakuna Halmashauri hata moja
 ambayo imendaa mpango kazi wa uanzishwaji wa viwanda.

 “Kuanzia sasa hakuna, Mkuu wa Wilaya,
Mkurugenzi au Mkuu wa idara kutoka nje ya Mkoa, labda kwa
 wale wenye matatizo kama kuumwa na mialiko yote ya semina
 sasa isomeni, weka pembeni…maana ukiuliza watendaji
 utasikia tuko mbioni, sasa nimeona safari za kufuata mialiko
 Dodoma ziwe mwisho. ” alifafanua Makalla.

 Aidha, Makalla aliwataka wakurugenzi
 wote wa Halmashauri saba za Mkoa huo, wakishirikiana na
 Madiwani  kusimamia kwa umakini vyanzo vya mapato 
 ili kuinua mapato na kuepukana na utegemezi kutoka serikali
 Kuu.

 Alisema kwa mujibu wa taarifa hiyo ya
 CAG , Halmashauri hizo za Mkoa wa Mbeya zinajitegemea kwa
 asilimia 6.6 tu, huku zikitegemea ngvu ya serikali kuu kwa
 asilimia 93.6, kinyume na agizo la Waziri Mkuu, Kassim
 Majaliwa, aliyeagiza Halmashauri zote nchini kukusanya
 asilimia 80 kutoka vyanzo vyake vya ndani.

 Akizungumza nje ya kikao hicho, Diwani
 wa kata ya Kyimo, Peter Makoye, alipongeza  hatua
 iliyochukuliwa na Mkuu wa Mkoa akieleza kuwa, limekuja kwa
 wakati muafaka kwa kuwa licha ya Rais, Dk. John Magufuli,
 kutoa muelekeo wake, bado baadhi ya watendaji wamekuwa
 hawatekelez
 Naye, Diwani wa kata ya Kawetele,
 Anyimike Anganile, alionekana kushtushwa na taarifa
 iliyotolewa mbele ya mkuu wa Mkoa kuwa Wilaya ya Rungwe ina
 uhaba wa ardhi ya uwekezaj

 “Uwezo wa kuwekeza katika viwanda kwa
Rungwe ni mkubwa kwa kuwa, kuna maeneo mengi Mfano kata za
 Ilima, Kisondela na Ibigi ambako kuna mashamba ya
 halmashauri, lakini shida imekuwa ni dhamira ya viongozi
 kutaka  kuwekwa mjini” alisema Anganile.
 
Mkoa wa Mbeya ulikuwa ni miongoni mwa
 mikoa iliyokuwa na idadi kubwa ya viwanda, lakini
 vilibinafsishwa kwa wakezaji na kushindwa kuviendesha,.
 
Miongoni mwa viwanda hivyo
 vilivyobinafsishwa na kushindwa kuendelea na uendeshajini ni
 kiwanda cha nguo cha Mbeya Tixtile, kiwanda cha kutengeneza
zana za kilimo (ZZK), kiwanda cha Sabuni cha Hisoap, pamoja
 na kile cha nyama cha Tanganyika Packers.
Mwisho

0 comments:

Post a Comment