Pages

Ads 468x60px

Saturday, September 2, 2017

JESHI LA POLISI KUIMALISHA ULINZI SOMGWE AIRPOT MBEYA



JESHI la Polisi mkoani Mbeya limeanzisha kituo kidogo cha Polisi katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe ili kuimarisha ulinzi kwa abiria na wageni mbalimbali wanaosafiri.

Akithibitisha kuanzishwa kwa Kituo hicho, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohammed Mpinga alisema Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe unapokea wageni mbalimbali kutoka ndani na Nje ya Nchi hivyo unahitajika ulinzi ili wageni wawe katika hali ya usalama.

Alisema mbali na kuimarisha ulinzi kwa kuanzisha kituo kidogo cha Polisi pia anajipanga kuhakikisha kinakua na vitendea kazi vyote muhimu ikiwemo kuwepo wa Askari wa kutosha.

Aliongeza kuwa analazimika kuongeza ulinzi kutokana na tukio la hivi karibuni ambalo watu wasio waaminifu walivunja na kuiba Televisheni moja ya ukutani pamoja na kamera ya ulinzi katika mgahawa uliopo ndani ya uwanja huo.

Hata hivyo alisema wezi hao walishakamatwa na upelelezi unaendelea ili waweze kufikishwa mahakamani kwa ajili ya kesi inayowakabili kwani picha zao zilionekana katika Kamera zingine ambazo hawakuziona.

Aidha alitoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya wanaoishi na kufanya shughuli zao kuuzunguka uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe kuwa sehemu ya ulinzi wa Uwanja huo kwa kutoa taarifa pindi wanapobaini kuwepo kwa dalili za uhalifu.

Naye Meneja wa Uwanja wa Ndege Songwe, Hamis Amir alisema kutokana na umuhimu wa kuwepo kwa kituo cha Polisi Serikali ilitoa fedha kwa ajili ya kukarabati moja ya majengo yaliyopo uwanjani hapo kwa ajili ya matumizi ya kituo cha Polisi.

Alisema awali walikuwa wakitumia makampuni binafsi ya ulinzi ambayo uongozi wa Uwanja uliingia nao mkataba huku Jeshi la Polisi likifanya doria nyakati za usiku pekee tena kwa muda mfupi.

Alisema uwepo wa kituo cha Polisi kutasaidia kuimarisha ulinzi wa mali za Uwanja pamoja na usalama wa abiria katika kipindi ambacho Serikali inatarajia kumalisha ufungaji za Taa za kuwezesha ndege kutua nyakati za usiku na kiangazi sambamba na kukamilika kwa jingo la abirialenye uwezo wa kubeba abiria 450 kwa wakati mmoja.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment