Pages

Ads 468x60px

Thursday, May 31, 2012


Watanzania wenge wamekuwa na kasumba mbaya yakutokuona umuhimu wa mikutano ya vitongoji, vjiji na mitaa hivyo kupelekea kushindwa kuwakilisha karo na mataatizo yao na kuona viongozi waliowachagua kuwa ni watendaji wabovu na wasiowajibika kwao

Hayo yamesemwa na diwani wa kata ya Inyala MWALINGO M. KISEMBA katika mdahalo ulioandaliwa na mtandao wa asasi za kiraia mkoani mbeya (MBENGONET)  kwa malengo ya kuimalisha  mahusiano na kuongeza wigo wa majadiliano kati ya wabunge, madiwani na wananchi

“Jukumu la diwani ni kuchukua matatizo na kero za wananchi  na kuipelekea serikali, Pia kuhamasisha wananchi katika shughuri za maendeleo na kuwawakilisha wananchi katika baraza la madiwani katika halmashauri nakushiliki kupanga bajeti kwa niaba ya wananchi . Hivyo wengi hawapendi kutokeza katika mikutano ya kimaendeleo “ amesema mwalingo.

Kwa upande wa wananchi wameulalamikia uwongozi akiwemo mbunge wa wilaya ya mbeya vijijini LACSON MWANJALA kwakuwa mbali na wapiga kura wake kwani tangu achaguliwe octoba 30/2010 hajawahi watembelea wala kujua matatizo na kero walizonazo na kushindwa mtetezi wa shida zao

Mmoja wa wananchi JOSEPH CHAMBELA alisema wamekuwa na matatizo mengi ikiwa na pamoja na ukosefu wa huduma bora katika hospitali yao haswa ukitumia huduma ya bima ya afya na ukihudumiwa utaambiwa hakuna dawa hivi tunatibiwa bule? Alihoji CHEMBELA

Matatizo mengine ni pamoja na gari la wagonjwa na tunapotaka huduma kwa mama wajawazito na wakati mwingine kuambiwa halina mafuta pia kutopata pembejeo za kilimo mbolea kwa wakati na kwa bei kubwa wakati mazao yanapovunwa huuzwa kwa bei ya chini hivyo kupelekea mkulima kutonufaika na kilimo.

Mwisho wananchi walishauri wilaya ya mbeya vijijini igawe upya kwakuwa ni kubwa sana na kupelekea baadhi ya vijiji kushundwa kupata huduma muhimu kwakuwa zinapatikana mbali, Pia kumpunguzia kajukumu Afisa mtendaji wa kata hiyo anayetumikia vijiji viwili na anaishi mbali na kata anayofanya kazi.


0 comments:

Post a Comment