Pages

Ads 468x60px

Friday, June 29, 2012


SAKATA LA KUGOMA KWA MADAKTARI LIME CHUKUA SURA MPYA MKOANI MBEYA MARA BAADA YA BODI YA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KUWAFUKUZA NA KUWARUDISHA KWA MWAAJIRI WAO KATIBU MKUU WA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII KWA HATUA ZA KINIDHAMU NA WALE WAISHIO HOSTELI KUONDOKA MARA MOJA IFIKAPO SAA KUMI NA MOJA NA KUVIACHA VYUMBA KUWA WAZI.
JANA WALIONEKANA MADAKTARI HAO WAKIHAHA KUTAFUTA HIFADHI YAO NA MALI ZAO ILI KUTII AMRI ILIYOTOLEWA NA HOSPITALI YA RUFAA ILIYOWATAKA KUONDOKA MARA MOJA, HALI HIYO IMEJITOKEZA KUTOKANA NA MSUGUANO KATI YA SERIKALI NA MADAKTARI HAO NCHI NZIMA WAKIDAI BAADHI YA HAKI ZAO.
MADAKTARI WAMEKUWA WAKIENDESHA MIGOMO ILI KUSHUNIKIZA SERIKALI KUWATIMIZIA MATAKWA YAO HAYO,NA  HII NI MARA YA PILI KUFANYA MGOMO WA AINA HIYO KWANI MNAMO MWEZI MARCH KULIENDESHWA  MGOMO KWA MADAKTARI NAKU SABABISHA VIFO NA  ADHA KUBWA KWA WANACHI WA TANZANIA.
MNAMO JUNE 23 MWAKA HUU KAMATI YA MADAKTARI ILIBADIKA TANGAZO LAKUANZA MGOMO USIO NA KIKOMO KITU AMBACHO KILITEKELEZWA KWAKUTOKUINGIA KAZINI .
HATAHIVYO MNAMO JUNE 28 MWAKA HUU BODI YA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA ILITOA MAAMUZI YA MAHAKAMA KUU YA KAZI JUU YA MGOGORO WAO HUO KWA KUYABANDIKA IKIWATAKA WASISHIRIKI MAANDAMANO WALA MGOMO  WOWOTE NAKISHA KUTOA WARAKA WAKUWAFUKUZA MADAKTARI HAO.

 Hili ni Tangazo liliwataka madaktari kuanza mgomo Hospitari ya Rufaa Mbeya,
 
PRESS RELEASE
MADAKTARI WA HOSPITAL YA RUFAA MBEYA KUTOTEKELEZA WAJIBU WAO WA KUHUDUMIA WAGONJWA.
Tarehe 22/6/2012 mahakama kuu ya kazi Tanzania (The high cout of Tanzania labour division of the high court at Dar es salam) ilitoa hukumu na. 73 ya 2012(miss Appl no.73 of 2012  kwenye kesi kati ya mwanasheria mkuu wa serikali (Attomey general na chama cha madaktari Tanzania (Medical Association of Tanzania (Mat) hukumu hiyo iliamuliwa wanachama wa MAT nchi nzima  wasifanye wala kushiriki kwenye mgomo. Ninanukuu (I therefore, based on the afore stated reasons do hereby grant the application order temporary injunction the following effect;
That the respondent and its members country, are restrained from colling or participating the strike pending the determination of the application into parties it is so orderd S.C Moshi
                 Judge
              22/6/2012
Hukumu hiyo ilijulishwa kwa wafanya kazi wote hata hivyo,Kuanzia june23mwaka huu Siku ya jumamaosi asubuhi yalibandikwa matangazo sehemu mbalimbali za Hospitali ya Rufaa ambayo yaliwaasa wafanyakazi wagome hayakuwa yameonyesha kuwa yametolewa na nani ila tu ilionyesha imetolewa na KAMATI
Siku hiyo yajune 23mwaka huu Wafanyakazi 15 waliokuwa zamu(Intern Doctor 12 na Registrars 3) hawakufika kazini Tarehe 24/6/2012 wafanya kazi 19 Intern Doctors 15 Registrars 4) hawakufika kazini na kuanzia tarehe 25/6/2012 hadi leo Imethibitika kuwa Intern Doctors 54 Registrars 18 hawakufika hadi leo Tarehe 28/6/2012.
Tarehe 25/6/2012 Bodi ya hospital ilifanya kikao cha dharura hali ya utendaji kazi na utaoji wa huduma hospitalini. Bodi iliamua yafuatayo
1.    Mwenyekiti wa bodi akutane na madaktari ambao hawakufika kazini ili awasikilize sababu za kutofika na kujadili namna ya kumaliza matatizo hayo.
2.    Madaktari wote ambao hawafiki kazini waandikiwe barua za kujieleza kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuvunja mkataba walioingia na Hospitali na pia kukiuka kanuni za kudumu za utumishi wa umma Toleo la 2009, kifungu na. f 16-f 17 na f 27
3.    Iwapo madaktari ambao hawafiki kazini hawataripoti au kueleza sababu za kulidhisha ifikapo Tarehe 28/6/2012 kwakuzingatia kanuni za utumishi wa umma toleo la 2009 kifungi na. 16-17 na f 27 madaktari hao watakuwa wamesimamishwa kazi na kurudishwa kwa mwaajiri wao ambaye ni Katibu mkuu wa wizara ya Afya ustawi wa jamii kwa hatua zaidi za kinidhamu zinazostahili
4.    Bodi iliwasiliana na Taasisi mbalimbali hapa Mbeya na nje ya mkoa ili kupata wafanyakazi wa kusaidia kupunguza makali ya katika Hospitali ya Rufaa Mbeya.

Matokeo ya maamuzi hayo ni kama ifuatavyo:-
 
(i)                Madaktari wote walioalikwa kukutana na mwenyekiti wa Bodi ya hospitali Rufaa Mbeya hawakuhudhuria
(ii)             Barua walizo andikiwa ili kujieleza kwa nini wasichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kutofika kazini hazikujibiwa.
(iii)           Tumepata ushirikiano toka kwa mkurugenzi wajiji kwa kupatiwa madaktari watano kusaidi hospitali ya Rufaa

Leo Tarehe 28/6/2012 madaktari Intern 54 wanapewa barua zao za kuwaeleza kuwa Bodi ya hospitali ya Rufaa Imesitisha Internship yao hapo hospitalini na kuwarudisha kwa Katibu Mkuu wa wizara ya Afya na ustawi wa jamii kwa hatua zaidi zinazosthili. Hivyo kwa wale wanao kaa Hostel waondoke kabla ya saa kumi na moja jioni leo.

Madaktari waajiliwa wanakabidhiwa Barua zao za kusimamishwa ajira yao katika hospitali ya Rufaa Mbeya  na kurudishwa kwa Katibu mkuu wa wizara ya Afya na ustawi wa jamii kwa hatua zaidi za kinidhamu.

Aidha wote wanapaswa kukubidhi mali zote za Hospitali.
Madaktari wakijiandaa kuondoka katika Hostel ya Hospitali ya Rufaa Mbeya. Wakitii Amli ya kuwataka kufanya hivyo.
MADKTARI WA HOSPITAL YA RUFAA MBEYA WAKIONDOKA ENEO LA HOSTEL MARA BAADA YA KUONDOLEWA NA BODI YA HOSPITALI HIYO
 

0 comments:

Post a Comment