Pages

Ads 468x60px

Sunday, July 1, 2012


Amani, utulivu na Maendeleo ya nchi haviwezi paitikana bila waandishi wa Habari, Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa mbeya Diwani Athumani katika kikao cha pamoja alipowatembelea katika ofisi ya Clubu ya waandishi wa Habsri zilizopo uhindi jijini mbeya.

Diwani alifika ofisini hapo kwa malengo ya kujitambulisha kwa waandishi wa habari mara baada ya kuondoka kwa kamanda Advoket Nyombi na nafasi yake kuchukuliwa naye. Aliwataka waandishi wa habali kutoa ushilikiano kwa jeshi la polisi ili kufanikisha jiji kuwa katika hari ya usalama na amani.
“Ninajua waandishi wa habari ni makachelo na mnapata taarifa nyingi kuliko hata jeshi la Polisi, Tukishilikiana kwa pamoja tutakomesha vitendo vya uharifu vilivyoshamiri mkoani mbeya, Tukifanya hivyo tutaisaidi jamii kupata haki zao ambazoziko hatalini kupotea, Kwaupande wa jeshi la polisi tumejipanga sana” amesema Diwani.

Kwaupande wa waandishi wa habari wamempongeza kamanda Diwani kwakutambua umuhimu wa Tasinia hii ya Habari na kwatembelea katika Clubu yao ili  kujipanga na kufanya kazi kwa ushirikiano kama alivyotaka lakini walimuomba kutokuwa na ubaguzi kwa kuwataka baadhi ya waandishi na wengine kuona kama hawafai kwakufanya hivyo kutamfanya afanye kazi kwa uguma sana. 

0 comments:

Post a Comment