Pages

Ads 468x60px

Thursday, July 19, 2012


Katika hali isiokuwa yakawaida mwanamke mmoja mkazi wa Isanga jijini Mbeya amejitosa kwenye kazi iliyozoweleka na wanaume yakuendesha bajaji ili kujikwamua kimaisha.
Mwanamke huyo mkazi wa Isanga Jiji Mbeya Jasmini konga amesema hayo wakati akiwa katika shughuli zake akizungumza na blog ya malafyale na kuwataka wanawake kuondokana na matazamo potofu kuwa kuna kazi zinazo fanywa na wanaume tu.
Jasmini amesema kilichomvutia kufanya kazi ya kuendesha bajaji ni kutaka kuona kwamba hata wanawake wanaweza na pia ameipenda kwakua inamsaidia kupata kipato sha kujikimu kimaisha akisaidiana na mume wake kuendesha maisha ya kila siku nakuongeza kuwa muda mlefu alikuwa akiitamani  kazi hiyo hivyo anafurahia kutimiza ndoto yake.
Amesema licha ya changamoto nyingi anazokutana nazo akiwa barabarani bado hakati taamaa ikiwemo kuwahi kupaki mapema bajaji yake kutokana na majukumu mengine ya kutunza familia kwani ana mume na mtoto hivyo kusababisha wakati mwingine kutofikisha malengo ya tajiri yake.
 Mwanamke huyo amesema malengo yake ya baadae ni kuona anamiliki Bajaji yake mwenyewe ili kuwa huru zaidi kwa kijiajiri na kupata kipato chake.
Naye Abdalla Muhamed mmoja wa madereva hao ameitaka jamii kuheshimu kazi za madereva hao kwani inawapatia kipato chao cha kila siku hivyo kuizarau ni kuwakatisha tamaa vijana .
Dereva wa Bajiji Jasmini Konga akiwajibika katika Bajaji yake akiwa na Mtoto wake wa kiume
 Jasmini akiwa katika mkao wa kuondoka maeeneo ya kuegesha Bajaji karibu na jengo la Kasisi Mwanjelwa.

0 comments:

Post a Comment