Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 22, 2012

WAVAMIZI WA MACHIMBO YA KOKOTO UYOLE YATISHIA USALAMA WA MAISHA YAO


Baadhi ya vijana wanao chimba kokoto maeneo ya Uyole jijini mbeya kwa kutumia zana zisozo rasmi kwa kazi hiyo wapo hatarini kuhatalisha maisha yao ya kuangukiwa na vifusi vya mawe.

Kwamjibu wa uchunguzi ulio fanywa na mwandishi wa blog hii umebaini kuwa, wachimbaji hao wanatumia njia ya kuchoma moto mataili ya magari kwa ajili ya kuyalainisha mawe  hayo ili kuwarahisishia kupasua.

Wasiwasi mkubwa unakuja pale ambapo vijana hao wanaingia chini ya shimo la kuchimba kokoto huku ukuta ukiwa na ufa mkubwa ambao muda wote unaweza kupolomoka na kuhatalisha kifo.


 HII NDIYO HALI HARISI YA UCHIMBAJI WA KOKOTO MAARUFU KAMA SHIMONI HUKO UYOLE JIJINI MBEYA


 HATARI YA MACHIMBO HAYO YANAYOZALISHA KOKOTO ZINAZOTUMIKA KATIKA KUJENGA MAJENGO YA JIJI LA MBEYA

                BAADA YA KUZALISHWA TAYALI KWA MATUMIZI YA UJENZI

Nitumaini langu machimbo hayo yanajulikana na maraka husika lakini yatachukuliwa hatua sitahiki mala baada ya kutokea maafa kwakua ndiyo destuli ya waliopewa dhamana wa nchi hii

0 comments:

Post a Comment