Wakati neema ya mvua za vuli
ikiendelea kunawiri katika maeneo mbali mbali nchini ikileta faraja zaidi kwa
wakulima na wafugaji kwa kupata malisho ya Mifugo yao lakini kwa upande
mwengine mvua hiyo hiyo imeonekana kuleta hasara.
Hasara
hiyo inaonekana kuikumba Wizara ya Habari,Utamaduni, Utalii na Michezo kufuatia
Jengo lake Maarufu la Makumbusho ya Taifa la Beit Al- Ajaib liliopo Forodhani
Mjini Zanzibar kubomoka upande wa nyuma wa Jengo hilo.
Kifusi
kilichodondoka kutoka kwenye Dari ya Jengo hilo robo yake kimeishia kwenye gari
moja ndogo yenye nambari za usajili Z 897 DF inayomilikiwa na Bwana Said Saleh
Saidi Mkaazi wa Forodhani ambae alikuwa ameiegesha pembezoni mwa Jengo
hilo.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alifika mapema asubuhi katika eneo hilo
kuangalia tukio hilo baada ya kupata taarifa hiyo na kuonyesha masikitiko yake
kutokana na hasara hiyo kubwa.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Mh. Said Ali Mbarouk alimueleza Balozi
Seif kwamba Wizara hiyo ilikuwa ikiendelea na juhudi za kulifanyia matengenezo
Jengo hilo kwa kipindi kirefu sasa.
Waziri
Mbarouk alifahamisha kwamba jitihada hizo zilikuwa zikienda sambamba na
matayarisho ya kutaka kuliezeka jengo hilokwa upande wa nyuma.
Alieleza
kwamba kutokana na tatizo hilo Wizara ya Habari inakusudia kuwatumia Wataalamu
wa Wizara yake kwa kukaa pamoja na Wahandisi wa Idara ya Ujenzi Zanzibar
kuangalia hatua za kuchukuwa ili tatizo hilo lisije leta maafa.
Naye
Mmiliki wa gari ndogo iliyoegeshwa pembezoni mwa Jengo hilo ambayo imeharibika
kabisa kutokana na tukio hilo Bwana Said Saleh Said alisema alishuhudia
mporomoko huo ukitokea muda mfupi baada ya kuegesha gari yake.
CHANZO: DULLONET
0 comments:
Post a Comment