Pages

Ads 468x60px

Friday, March 1, 2013

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) KIMECHANGISHA FEDHA MKOANI MBEYA KWA AJIRI YA MAANDALIZI YA MAANDAMANO YA KANDA MARA BAADA YA KUISHA KWA SIKU KUMI NA NNE ZILIZOTOLEWA


MCHANGO HUO UMEFANYIKA KATIKA MKUTANO WA HADHARA ULIOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA RUANDA NZOVWE JIJINI HAPA NA KUPATIKA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI TATU

Akiongea na wananchi waliofulika kusikiliza hotuba hiyo iliyotolewa na mwaenyeti wa chama hicho PHILIMON MBOWE amewatake wananchi kujitokeza kwa wingi katika maandamano hayo yenye lengo la kushinikiza waziri wa Elimu SHUKURU KAWAMBWA pamoja na naibu wake
 PHILIP MURUGO kujiuzuru kutokana na matokeo mabovu ya wanafunzi wa kidato cha nne

Mbowe amewataka wabunge waote kuratibu maandamano hayo na wanafunzi waliofeli kidato cha nne, waalimu, na wanavyuo kujitokeza kwa wingi barabarani kuunga mkono mpango huo

“Kazi ya kwanza ninayo wapa nyie wabunge wote mliopo hapa ni kuratibu maandamano hayo ambayo tumeipa siku kumi na nne Serikali kuwawajibisha mawaziri wa wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi bado siku tatu kutimia” MBOWE alisema

Ninachosema si utani Mungu anataka kufanya mabadiliko katika nchi hii anakitumia chama cha chadema kufikia lengo la Mungu  hivyo hatuko tayali kufanya mzaha katika jambo hili lazima watu hawa wawajibike ama Serikali iwawajibishe  kwakuwa wameshindwa kufanya kazi wameidhalilisha elimu ya Tanzania

Akitoa takwimu ya ufaulu wa wananfunzi wa darasa la saba MBOWE amesema kila mwaka wanafunzi mlioni moja na laki mbili hufanya mtihani wa kumaliza Elimu hiyo ni lakitano tu wanaofauru kwenda kidato cha nne na laki saba hubaki n a hawa na watoto wa mlala haoi

Kwa wale wanaopata nafasi ya kufauru kwenda kidao cha nne hupelekwa katika shule za kata kusiko kuwa na madarasa, vitabu, wala maabara za kujifunzia hali hii tutakuwa nayo mpaka lini? MBOWE alihoji 


0 comments:

Post a Comment