Pages

Ads 468x60px

Thursday, March 14, 2013

MITUME WALIOPO NCHINI KWA MASLAHI YAO BINAFSI HAO HAWAJATUMWA NA MUNGU, NI MATAPELI NA HULIPELEKA TAIFA KUPOTEZA AMANI







MKURUGENZI WA JEM MINISTRY JEREMIA MWAKANYILENGE AKIONGE NA WAANDISHI WA HABARI OFISINI KWAKE
WAANDISHI WA HABARI WAKIWA OFISI YA JEM MINISTRY WAKIONGEA NA MKURUGENZI JEREMIA MWAKANYILENGE

-->
KWAKUA MITUME WA KWELI YEYE NI MUHUDUMU WA JAMII NA MUNGU HUYAFANYA MAMBO MAGUMU KUWA MEPESI

Hayo yasememwa na mtume JEREMIA MWAKANYILENGE wa huduma ya Jem ministry ya jijini mbeya alipokuwa akiitambulisha huduma hiyo kwa waandishi wa habari ofisini kwake.

Mwakanyilenge amewataka waumini kuwa makini sana na huduma hizi zilizoshamili kuibuka kila siku kutokana na kuwepo na baadhi ya watumishi matapeli wanaotumia jina la kristo kujinufaisha wenyewe binafsi

“Ukiona mtume huduma yake inaleta uchochezi katika taifa hili ujue huyo si wa mungu atakuwa amejituma mwenyewe na ni tapeli, kwani aliyetumwa na mungu kweli huyafanya yaliyo magumu kwa watu kuwa mepesi” amesema mwakanyilenge.

Katika kikao hicho pia alipata nafasi ya kuitambulisha rasmi hudu yake ya JEM MINISTRY kua si kanisa jipya bali ni tasisi ya kuihudumia jamii kwa kuwapatia ajira katika idara zake za biashara kama vile JP PRODUCTION studio inayofanya kazi za kurekodi audio cd pamoja na video, lakini pia imeanzisha mfuko wa kustaafu wachungaji.

JP PRODUCTION imetoa ajira kwa wachungaji na vijana mbalimbali wenye kipaji cha uimbaji kwa kujikimu na maisha yao kama wengine, Lakini pia imekuwa ikisambaza kazi za waimbaji kwa kuwapa faida kubwa kuliko wasamabazaji wengine.

Kwa hivi sasa JEM MINISTY pamoja na JP PRODUCTION imeto kazi mpya ambayo ipo sokoni yenye nyimbo nane zilizoimbwa live na mtumishi wa mungu JEREMIA MWAKANYILENGE kwa kushirikiana na mwaimbaji wa kimataifa EFRAIM SEKELETI toka nchini zambia.



0 comments:

Post a Comment