Pages

Ads 468x60px

Wednesday, April 24, 2013

Uelewa mdogo wa wananchi nchini Tanzania kuhusu afya ya uzazi na mtoto umepelekea kuendelea kuzorota kwa idadi ya wanaume wanaohudhuria huduma ya kliniki kutokana ushirikiano hafifu uliopo katika jamii.

mmutta@fhi360.org -->

Hayo yamebainishwa na ofisi ya mganga mkuu mkoa wa mbeya kitengo cha huduma za afya ya uzazi na mtoto kwa kushirikiana na shirika la UJERUMANI (GIZ).

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake mratibu wa huduma hiyo PRISCA BUTUYUYU amesema kumekua na upungufu mkubwa kwa baadhi ya wanaume kutoshiriki katika huduma za afya ya uzazi.

“Katika tafiti zilizofanywa kwa wilaya nane za mkoa wa mbeya tangu mwaka 2009 hadi 2011  zimeonyesha idadi za wanawake wanaokwenda klinic wakiwa na wenzi wao imendelea kuporomoka kila wakati hivyo ofisi yetu imeliona hilo na umuhimu wake hivyo kuchukua jukumu la kuhamasisha wanaume kushiriki katika hupata huduma za afya wakiwa na wenzi wao” BUTUYUYU amesema.

Kunafaida kubwa kwa wenzi kushiriki pamoja katika huduma za afya  ya uzazi kama vile kupima pamoja, hususani maambukizi ya VVU kwani kwa kufanya hivyo mnaweza kujitambua na kuishi maisha ya kumlinda mtoto pamoja na mwenzi wake endapo mmoja wao atagundulika ana maambukizi, BUTUYUYU amesea

Ameongeza kua mbali na kupima magonjwa pia kunaelimu mbalimbali ikiwemo kujifunza namana ya kupanga uzazi, jinsi ya kulea mimba kujiandaa  kupokea mtoto atakapozaliwa  pamoja na jinsi ya kumlea.

Kwakuona umuhimu wa swala hilo kwa wananchi wa TANZANIA,   ENGENDER HEALTH kwa kushirikiana na shirika la FHI 360 limetoa mradi wa champion  wa kuhamasisha vyombo mbalimbali vya habari kushiriki katika kampeni hii ili kuandika habari pamoja na vipindi vyenye kutoa ujumbe wenye kuhamasisha wenza kushiriki katika huduma za afya ya uzazi,

Akiongea katika semina ya waandishi wa habari iliyofanyika katika ukumbi wa IFISI COMMUNITY CENTER afisa mratibu mwandamizi wa mradi wa champion MUGANYIZI MUTTA amewataka waandishi kushiriki katika kampeni hizi.

“Mradi huu upo katika mikoa kumi yenye maambukizi ya juu ya VVu, kwa hiyo tumelenga katika kuhamasisha wanaume kupunguza kuwa na mahusiano ya wanawake wengi, kupambana na mila na desturi katika jamii, Kuweka sera mahari pa kazi kuhusu swala la wanaume na maambukizi ya VVU” amesema MUGANYIZI.

Ameongeza kuwa habari zilenge kuhamasisha mambo hayo muhimu na  mwandishi  atakaye andika habari na ikatumika katika chombo chake itakuwa imeinga katika shindano la Champion ambalo zaidi ya Tshs milioni mbili kushindaniwa.
   

0 comments:

Post a Comment