Pages

Ads 468x60px

Sunday, July 28, 2013

MKIMBIAJI WA KIKE MKENYA, IRENE CHEBET CHEPTAI, AANGUKA NA KUZIMIA WAKATI AKIMALIZIA MBIO ZA MITA 3,000 JIJINI LONDON......


Collapsed: Irine Chebet Cheptai was rushed to hospital after collapsing following the 3,000m
Jopo la Madaktari wakihaha kumpatia huduma ya kwanza, mkimbiaji mwanadada wa nchini Kenya, Irine Cheptai, aliyeanguka na kuzimia wakati akimalizia mbio za mita 3,000 kwenye Uwanja wa Olimpiki.
treatment: Chebet Cheptai left the track unconscious but, according to reports, later regained consciousness in hospital
Cheptai akiwa amewekeaa mtungi wa hewa ya oksijeni, baada ya kuanguka na kuzimia kutokana na shambulio la moyo. Hata hivyo aliweza kupata fahamu na kuzinduka baada ya kufikishwa hospitali.
The Kenyan finished 11th in the race
Cheptai (wa pili kulia) akikimbia mbio za mita 3,000 kwenye Uwanja wa Olimpiki jijini London.
*********************************
LONDON, England

Cheptai, binti wa miaka 21, alimaliza mbio akiwa nafasi ya 11, katika muda bora zaidi katika rekodi yake binafsi, alipotumia dakika 8:56.20, lakini akaanguka ghafla na kupoteza fahamu baada tu ya kuvuka mstari wa kumalizia

MKIMBIAJI wa mbio ndefu wa kimataifa wa Kenya, Irine Chebet Cheptai jana alikimbizwa hospitali kwa matibabu baada ya kupatwa na mshituko wa moyo kwenye Uwanja wa Olimpiki baada ya kumaliza mbio za mita 3,000.

Cheptai, binti wa miaka 21, alimaliza mbio akiwa nafasi ya 11, katika muda bora zaidi katika rekodi yake binafsi, alipotumia dakika 8:56.20, lakini akaanguka ghafla na kupoteza fahamu baada tu ya kuvuka mstari wa kumalizia.

Madaktari waliokuwa uwanjani hapo wakaharakisha kumtundikia mtungi wa Oksijeni, ambapo kwa mujibu wa taarifa kuhusiana na tukio hilo zilipasha kuwa alikuja kurejewa na fahamu akiwa hospitalini.

Tukio lake limeshtua wengi kutokana na kukimbia katika mbio fupi kulinganisha na zile alizozoea za mita 5,000, ambazo ameshiriki Diamond League mara mbili msimu huu, na anakumbukwa kwa rekodi yake ya dakika 14:50.99 jijini Shanghai, Mei mwaka huu.
Daily Ma

0 comments:

Post a Comment