Kwa kupitia Facebook Accout, Rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania
Addo Novemba amepost habari za kifo cha mwimbaji wa nyimbo za Injili
Tanzania Debora Said na hivi ndivyo alivyoandika, "Pigo Tena kwa Tasnia
ya Muziki wa Injili, ninayo huzuni kubwa
kuwatangazia Kifo cha Mwenzetu Deborah Said aliyefariki
Muhimbili..naomba ushirikiano katika kipindi kigumu, kwa kuwa nipo nje
ya Dar nikijiandaa kurudi nimeshamtuma Mhe Cosmas Chidumule aunganishe
wanamuziki wote..Bwana Ametwaa, Tuonane Milele Tuonane Bandarini Pale!"
Rumafrica imepokea kwa masikitiko makubwa sana juu ya kifo cha Debora,
tunawapa pole wafiwa na Watanzania wote na kupotelewa na mtumishi wa
Mungu ambaye amefanya kazi yake kwa upendo na uaminifu. Mungu azidi
kuipigania familia yake na wale wote waliokuwa wakimtegemea kiroho na
kimwili. Kazi ya Mungu daima haina makosa, tuzidi kumtumikia Mungu sisi
tuliobaki kwani hatujui vilivyombele yetu.
Huu ni wakati wa kuungama na kutubu makosa tunayoyafanya katika maisha
yetu hapa dunia, siku ya mwisho tutatupwa jehanamu kama tukizidi
kumsahau Mungu. Mungu amekupa kipaji fulani kwa kazi yake basi kitumia
na usiache. Debora amefanya kazi ya Mungu kwa njia ya uimbaji na sasa
Mungu amemchukua akampongezi kwa kile amekifanya duniani.
0 comments:
Post a Comment