Pages

Ads 468x60px

Tuesday, August 12, 2014

Baadhi ya wadau washiliki warsha kujadili mustakabali wa Tazania miaka 20 ijayo


Mkutano wafanyika katika ukumbi wa Paradise hotel jijini Mbeya,
kwa ufadhili wa Society for Intrnational development (SID) na Foundation for civil Society (FCS)

Muwezeshaji wa warsha hiyo Edmund Matotay kutoka (SID) akitoa maelezo kwa washiliki
                            Monica Hangi Program Manager Society International Develpment (SID)
Neema Yobu Program Manager Foundation For Civil society (FCS)

 Neema Yobu aliepo kulia na Monica Hangi wakiratibu mambo mbalimbali yanayohusu Warsha







Wana warsha wakisikiliza kwa makini kutoka kwa mkufunzi Edmund Matotay
                                                                                Emile Malinza
                                                      Regina Ngalawa Mwanafunzi (MNMA)
                                                    Alpha Laizer, Mwanafuzi wa chuo kikuu Teku
                                     Christina Patrick Afisa mtendaji kata ya Itezi Jijini Mbeya
                                      Eugen Kisonga Mkurugenzi Mbeya Hop for Ophans
        Aggrey Kandonga, Mwenyekiti wa Mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali wilaya ya Mbeya
                                              Samwel Mbaule, Mwalimu shule ya sekondal Vanessa
                                             Issa Mwasinyanga, Mchungaji wa kanisa la Baptist
                    Simon Mkaya, Mweka hazina Mbengonet

Baadhi ya wana warsha wakichangia maoni ya mada husika katika mkutano unaendelea katika ukumbi wa Paradise Hotel 

                                               
                                             Habari 

Baadhi ya wadau washiliki warsha kujadili mustakabali wa Tazania mika 20 ijayo,
 Mkutano wafanyika katika ukumbi wa Paradise hotel jijini Mbeya,
kwa ufadhili wa society for Intrnational development (SID) na Foundation for civil Society

Baadhi ya wadau mkoani hapa wamekutana kataka warsha ya siku moja katika ukumbi wa Paradise Hoteli uliopo maeneo ya Soweto kwa lengo la kujadiliana kuhusu mustakabali wa Taifa la  Tazania miaka 20 ijayo yaani hatima na mustakabali wa taifa  ifikapo mwaka 2035

Katika warsha hiyo Iliyoendeshwa na mkufunzi Edmund Matotay toka Socety International Divelopment (SID) na kuratibiwa nae Neema Yobu wa Foundational for civil (FCS) pamoja na Monica Hangi kutoka Society International.

Ililenga kujadili nafasi ya Tanzania katika Shirikisho la Afrika mashariki, miundombinu ya nchi, hali na mustakabali wa muungano wetu,mustakabali wa kilimo chetu na mabadiliko ya nchi na athari zake.

Akiongea mkufunzi wa walsha hiyo Matotay, amewataka washiriki kujadili na kupambanua mustakabali wan chi yetu kwa miaka mingi ijayo lakini pia kuangali maswala muhimu nay a msingi kama vile nini kimetusaidia nchi yetu kufikia hapa ilipo leo.

Ameongeza kua Tanzania itakuaje ifikapo mwaka 2035 nini kitafanya jamii yetu kubadilika na nini kitatokea majadiliano hayo yaibue maono ya pamoja hata yale ya kutofautiana lakini pia mwisho wa siku kuibua matumaini ya pamoja na mustakabali wa Tanzania yetu ya baadae.

Wakijadili mada hiyo makundi yalikua na maono mbalimbili kwa kujifikilisha ikiwemo Tanzania ya miaka hiyo itakuana  ufinyu wa fursa na kuchochea uasi kwa wasio nacho kuchoshwa na umasikini wa kutupwa pia huduma mbaya za kijamii.

Mambo mengine ni kushindwa kulipa madeni ambayo nchi inaingia na kusababisha nchi wahisani kuacha kuipa mikopo na kushindwa kujiendasha kwakua Tanzania inategemea bajeti zake kutekelezwa kwa misaada.

Lakini pia kumekuwepo na mashaka ya usalama wa nchi kutokana na majeshi yetu kujiendesha kwa misaada na kisha kusababisha mpasuko kutokana na siasa zinazo enazoendelea kama vile mgawanyiko wa muungano wetu,

Majadiliano hayo yanafanyika nchi nzima kwa muda wa miezi miwili ijayo. Mpaka ifikapo Novemba 2014 muhtasar wa majadiliano utaandaliwa na kuchapwa katika machapisho ambayo yatapelekwa kwa wadau wote ili kuongeza na kua na ushiriki mpana hasa ni kutia chachu ya kitaifa na kua na ushiriki shadidi na ushahidi wa kutosha ili kusonga mbele.  

0 comments:

Post a Comment