JK AMNG'OA UWAZIRI
PROFESA ANNA TIBAIJUKA SAKATA LA AKAUNTI YA ESCROW
Mh.Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na taifa kupitia Wazee wa
Dar es Salaam leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es
Salaam.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik na kulia
ni katibu wa Baraza la wazee wa Dar es Salaam Abdul Mtulia.Rais
alizungumzia sauala ya vurugu katika uchaguzi wa Srikali za Mitaa na
kuagiza vyombo vya kuwachukulia hatua za kisheria. Vilevile alifafanua
kuhusu sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow na kuchukua uamuzi wa kumng'oa
aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna
Tibaijuka na kumuweka kiporo Waziri wa Nishati na Madini, Profesa
Sospeter Muhongo.
Baadhi ya mawaziri wakisikiliza kwa makini hotuba ya Rais Jakaya
Kikwete, ambapo alifafanua kuhusu sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow na
kutangaza kumg'oa uwaziri aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na kumuweka kiporo Waziri wa
Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Baadhi ya wazee na wananchi wakimsikiliza kwa makini Rais Dkt.Jakaya
Mrisho Kikwete wakati alipokuwa akilihutubia taifa kupitia wazee wa Dar
es Salaam katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam leo
Wazee wa Wilaya ya Temeke wakiwa katika mkutano huo
Sehemu ya umati wa wananchi wakiwa kwenye mkutano huo
Baadhi ya viongozi wa dini wakiwa katika mkutano huo.
Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win
Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win
Rais wa
Jamhuri wa Tanzania Jakaya Kikwete ametangaza kutengua uteuzi wa Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka baada ya
vyombo vya Serikali kubaini na kijiridhisha kuwa amekiuka maadili ya
utumishi wa Umma kwa kuingiziwa fedha kiasi cha Sh1.65bilioni kwenye
akaunti yake binafsi.
Rais
kikwete ametangaza kufukuzwa kazi kwa Waziri huyo leo alipokuwa
anazungumza na wazee wa mkoa wa Dar es Salaam katika Ukumbi wa Diamond
Jubilee jijini hapa, na baada ya kutangaza kufukuzwa kwake maelfu ya
wazee waliohudhuria kwenye mkutano huo walipiga kelele za kumpongeza
Rais Kikwete kwa uamuzi wake.(MM)
Rais
kikwete amesema miongoni mwa mapendekezo ya Bunge kuhusiana na sakata la
uchotwaji wa fedha kwenye akaunti ya Escrow Tegeta yaliyofikishwa
kwenye Serikali ni pamoja na kuwajibishwa kwa Bodi ya Shirika la umeme
(Tanesco), Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka,
pamoja na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Rais
Kikwete amesema baada ya uchunguzi wa vyombo husika viliweza kubaini
kuwa kiasi cha Sh1.65bilioni kiliingizwa kwenye akaunti binafsi ya
Profesa Tibaijuka, jambo ambalo ni kinyume na maadili ya utumishi wa
Umma.
"Tumezungumza
na Profesa Tibaijuka na tumemuomba atupishe ili tuweze kuteua waziri
mwingine kwani viashiri vyote vinaonyesha kuwa alikiuka kanuni na sheria
ya maadili ya Umma," anasema Rais Kikwete.
Aidha
Rais Kikwete amesema katika suala la Waziri wa Nishati na Madini Profesa
Sospeter Muhongo analiweka kiporo maana bado hajapata ufafanuzi kuhusu
mambo kadha wa kadha, hivyo pindi atakapopata ufafanuzi na kujiridhisha
ataujulisha umma .
Amesema kuhusu suala la bodi ya Tanesco hana shida nalo kwa sababu tayari bodi hiyo imeshamaliza muda wake hivyo ni kama imekwishajifuta yenyewe, na kuongeza kuwa tayari Ikulu imeshapewa taarifa za kumtaka achague bodi nyingine, hivyo ndani ya siku chache bodi mpya ya Tanesco itatangazwa.
Amesema kuhusu suala la bodi ya Tanesco hana shida nalo kwa sababu tayari bodi hiyo imeshamaliza muda wake hivyo ni kama imekwishajifuta yenyewe, na kuongeza kuwa tayari Ikulu imeshapewa taarifa za kumtaka achague bodi nyingine, hivyo ndani ya siku chache bodi mpya ya Tanesco itatangazwa.
Amesema
suala la Katibu Mkuu wa Nishati na Madini na viongozi wengine wa
utumishi wa Umma ambao wametajwa katika sakata hilo tume ya maadili,
Taasisi ya Kuzuia na Kupapambana Rushwa (Takukuru) pamoja na jeshi la
polisi wanaendelea kufanya uchunguzi wao, na ikithibitika kuwa walikiuka
maadili yao ya kazi sheria stahiki zitachukuliwa.
0 comments:
Post a Comment