Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 5, 2015

IKIWA ZIMESALIA SIKU CHACHE KUKABIDHI MRADI WA BARABARA YA CHUNYA MBEYA



ZAIDI YA ALAMA 40 ZA KUONGOZEA MAGARI BARABARA YA CHUNYA MBEYA ZIMEIBWA

Katika hari isiyo ya kawaida watu wasiojulikana wameyaondoa mabomba yenye alama zakuongozea magari katika barabara mpya itokayo Mbeya kwenda Chunya,

Hali hiyo imejitokeza wakati zimebakia siku chache za kukamilika kwa mradi huo na kuukabidhi  kwa mwajiri ambae ni TANROAD

Akizungumza  kwa masikitiko makubwa Eng: Paul Lyakurwa meneja wa Tanroad mkoa wa mbeya katika mkutano wa hadhara na wananchi waishio karibu na mradi huo amesema  ni  vitendo vya aibu na visivyo vumilika na kwamba waliohusika lazima wanafahamika kwakuwa sehemu zilizo ondolewa vyuma hivyo ni makazi ya watu  hivyo si rahisi kutowafahamu.

Naye mgeni rasmi wa mkutano huo Nyerembe Munasa mkuu wa wilaya ya Mbeya amewataka wenye viti wa serikal za mitaa kufanya uchunguzi kwa kushirikiana na jeshi la polisi ili kuwabaini waliofanya vitendo hivyo haraka iwezekanvyo na kuwachukulia hatua stahiki.

Mmoja wa wananchi waishio kando ya maradi huo Jamesi kilumbo amesema baadhi ya sababu zinazopelekea vijana kuziondoa alama hizo ni ugumu wa maisha na ukosefu wa ajira hivyo kukosa pesa za kujikimu  pamoja na vitendo vya uvutaji bangi na ulevi wa kupindukia.

Pia Helena mwanjabili makazi wa Isanga imeitaka mamlaka husika kutoa elimu ya kutosha kuhusu umuhimu wa alama hizo kwa wananchi waishio pembezoni mwa barabara hiyo na kwamba kila mmoja awe na jukumu la kuona linamhusu kulinda ili vitendo hivyo viijirudii tena.
MWISHO

0 comments:

Post a Comment