Mkurugenzi
Mtendaji wa TBC, Clement Mshana ambaye pia ni Katibu wa bodi ya
wakurugenzi ya TBC akimueleza jambo Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo, Mh. Nape Nnauye leo jijini Dar es Salaam walipokutana
kuzungumzia changamoto mbali mbali za Shirika hilo.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye akiongea na
wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)
leo hii jijini Dar es Salaam. Mhe. Nape alifanya kikao na Bodi hiyo ili
kuzungumzia changamoto mbalimbali zinazolikabili shirika hilo na jinsi
ya kuyapatia ufumbuzi.Kulia kwa waziri ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo
Bi.Mwajabu Possi.
Baadhi
ya wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Utangazaji Tanzania
(TBC) wakimskiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh.
Nape Nnauye (hayupo pichani) jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment