Pages

Ads 468x60px

Friday, February 12, 2016

TAJATI WAJIONEA MKOA WA MBEYA ULIVYO HUJUMIWA NA WAWEKEZAJI UCHWALA



              JENGO LA KIWANDA CHA HISOOP LIMEGEUZWA KUA MAKAZI YA POPO

Chama cha waandishi wa uwekezaji na utalii Tanzania (TAJATI) watembelea kiwanda cha Sabuni cha hisop kilichopo iyunga jijini Mbeya na kujionea jinsi kilivyo filisiwa na wawekezaji wasio kua na huruma kwa nchi hii kwa kuiuwa kiochumi.

Waandishi hao wameshuhudi mazingira ya kiwanda hicho kugeuzwa kua mashmba ya maharagwe na mahindi badla ya utengenezaji wa sabuni iliyokua ikipendwa na wananchi wa mkoa huu, lakini pia kiwanda hicho kilitoa ajira kwa vijana.

Cha kushangaza sana katika kiwanda hicho hakuna kinacho endelea, isipokua  ndani ya godauni hilo waandishi wameshuhudi kung`olewa kwa vipuli vyote vya mashine na kuliacha gofu lililopo kua makazi ya popo baada ya kuliacha kwa muda mlefu bila kazi yoyote.

Akiongea mmoja wa walinzi waliopo hapo ambae hakutaka jina lake litajwe amesema hajawahi kuona jingo hilo likifunguliwa kwa muda mlefu sana na hamjui hata mmiliki wa eneo hilo tangu apangwe na viongozi wa kampuni yake kulinda lindo hilo amekua akifika na kuondoka bila kuona kitu chochote kinachoendelea.

Makamu mwenyekiti wa TAJATI ametoa wito kwa mamlaka husika kutupia jicho la pekee kwa wawekezaji wenye lengo baya la kuhujumu uchumi wa nchi kwa viwanda hivi ambavyo vilitoa manufaa kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
        WAANDISHI WAKIONGE NA MLINZI WALIPOWASILI KATIKA KIWANDA HICHO


WAANDISHI WALIPATA NAFASI YA KUTEMBE NDANI YA KIWANDA HICHO

MAKAMU MWENYEKITI CHRISTOPHA NYENYEMBE AKISHANGA KUHALIBIWA KWA MIUNDO MBINU




ILICHO IBAINI KAMRA YA MWANDISHI NGULI RASHID MKWINDA KUPITIA UPENYO HUU KILICHOPO NDANI YA KIWANDA HIKI
WAANDISHI WAKITOA MAONI JUU YA WALICHO KIONA KWA VYOMBO VYA HABARI

0 comments:

Post a Comment