Pages

Ads 468x60px

Wednesday, February 10, 2016

Tazama aibu za Nyani Kipunji alieko Milima ya Rungwe



Aibu zake zamefanya awe na thamani, Waandishi wa Habari za Utalii na uwekezaji Tanzani (TAJATI) wa msaka kwa udi na uvumba ili kumshuhudia.


                                                                       Nyani Kipunji

Hifadhi ya Mazingira ya Asili ya milima ya Rungwe Ni hifadhi inayo patikana Wilaya ya Rungwe mkoani mbeya,Iili hifadhiwa mwaka 1949 kwa lengo la kuhifadhi vyanzo vya maji na baionuai Hifadhi hii inaumbali  wa km 25 kusini mashariki mwa mji wa Mbeya na km 7 kusini mwa mji wa Tukuyu.

Baada ya kuona umuhimu wa hifadhi ya Mlima Rungwe, mchakato wa kupandisha hadhi ulianzishwa mwaka 2008 na hatimaye mwaka 2009 hifadhi ilipandishwa hadhi na kuwa Hifadhi ya Mazingira Asilia. Hifadhi ya Mazingira Asilia ni hadhi ya juu kuliko Msitu wa Hifadhi. Hifadhi ya Mazingira Asilia hairuhusu matumizi mengine zaidi ya elimu, utafiti na utalii.
Kutokana na sifa za kipekee za Hifadhi  ya Mazingira Asilia ya Mlima Rungwe: ikiwemo urefu wa mlima, mashimo ya volukano (paluvalutali, Lusiba na Ng’ombe) na wanyama aina ya kipunji, na maji moto. Vyote hivi vimekuwa vinashawishi watalii kutembelea hifadhi yenye  mazingira asilia ya mlima Rungwe. Pia hifadhi imepakana na hifadhi ya Kitulo ambayo ina vivutio vingi vya kitalii.
Hayo ndiyo yamepelekea kua kishawishi kikubwa kwa waandishi wa Habari za Utalii na uwekezaji Tanzania (TAJATI) kutembelea na kupanda mlima huo ili kujionea mambo hayo akiwepo Nyani aina ya kipunji mwenye sifa moja kubwa ya aibu ambayo inamfanya asionekene kwa urahisi kwa watu.
Akionge na waandishi wa habari mhifadhi mkuu wa mlima Rungwe Inocent Lipembembe amesema Nyani aina ya Kipunji haonekani kirahisi kutokana na aibu alizo nazo kwani hapendi kuonekana kilahisi kwa watu
“Pamoja na yote yaliyo kivutio kwa  watalii katika mlima huu yupo nyani Kipunji ambae hapatika ulimwenguni kote isipokua katika mlima Rungwe na ndiye kivutio kwa watalii na unapotaka kumuona lazima utoe taalifa mapema ili kuwaandaa watu maalumu ili kumtafuta mapema na ndipo wale waonataka kumuona tunawasiliana nao” Amesema Lupembe

Ameongeza kua  Kutokana na sifa za kipekee za Hifadhi  ya Mazingira Asilia ya Mlima Rungwe: ikiwemo urefu wa mlima, mashimo ya volukano (paluvalutali, Lusiba na Ng’ombe)  na maji moto. Vyote hivi vimekuwa vinashawishi watalii kutembelea hifadhi yetu ya mazingira asilia ya mlima Rungwe. Pia hifadhi imepakana na hifadhi ya Kitulo ambayo ina vivutio vingi vya kitalii.


                                         Mwandishi wa habari wa Blog hii Charles Abraham

Waandishi kufika getini kabla ya kuingia Hifadhini Kulia ni makamu mwenyekiti wa (TAJATI) Christopha Nyenyembe na Ezekiel Kamanga




 Mhifadhi mkuu Inocent Lipembembe akiongea jambo kwa waandishi wa habari kabla ya kupanda mlima

                            Mwandishi wa habari Rashid Mkwinda akifuatilia kwa makini jambo





                                                       Waandishi wakipanda Mlima Rungwe






0 comments:

Post a Comment