Mwenyekiti
 wa MISATAN, Simon Berege akizungumza na waandisshi wa habari kuhusu 
SIku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari. Kushoto ni Afisa Mafunzo wa TMF, 
Raziah Mawanga na Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri na Makamu 
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Deodatus Balile.
Siku
 za Uhuru wa Vyombo vya Habari ambayo hufanyika Mei 3 ya kila mwaka 
inataraji kufanyika jijini Mwanza kwa mwaka huu ambapo mgeni rasmi 
anatarajiwa kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande Othman na 
kuhudhuliwa na viongozi wengine nchini na wengine kutoka nje ya nchini 
ambapo kwa mwaka huu kaulimbiu ni KUPATA TAARIFA NI HAKI YAKO YA MSINGI.
Akizungumzia
 sherehe hizo katika mkutano na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa 
MISATAN, Simon Berege amesema sherehe za mwaka huu zinataraji kuwa na 
wageni zaidi ya 250 akiwepo Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na 
Michezo, Mhe. Nape Nnauye, Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, 
Alvaro Rodriguez na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa 
Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira 
Rodrigues.
Aidha
 Berege amesema kuwa siku ya uhuru wa vyombo vya habari kwa mwaka huu 
itafanyika kwa siku mbili, Mei, 2 kutakuwa na kongamano ambalo 
litatumika kujadili hali ya uhuru wa vyombo vya habari nchini na Mei, 3 
ndiyo itakuwa siku husika ya maadhimisho.
“Kikawaida
 huwa kuna  mambo tunafanya katika siku hiyo, tutawakumbuka waandishi wa
 habari waliopoteza maisha kazini, tutawakumbuka waandishi wa habari 
maveterani na waandishi wa habari waliopatwa na matatizo wakiwa kazini 
... kwa mwaka huu tutakuwa na mambo ya kipekee tofauti na miaka 
iliyopita,” amesema Berege.
Pia
  ameongeza kuwa watapitia sheria zinazohusu uhuru  wa vyombo vya habari
 kama Cyber Crime Act 2015 na Sheria ya Takwimu 2015 pia kuipitia 
miswada ya huduma ya vyombo vya habari na uhuru wa kupata taarifa.

Mhariri
 Mtendaji wa Gazeti la JAMHURI na Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la 
Wahariri (TEF), Deodatus Balile akizungumzia hali ya uhuru wa vyombo vya
 habari na haki ya kupata taarifa ilivyo nchini.  Kulia ni Afisa Mafunzo
 wa TMF, Raziah Mawanga, Mwenyekiti wa MISATAN, Simon Berege na Ofisa 
Miradi katika Kitengo cha Mawasiliano na Tehama UNESCO, Nancy Kaizelege.

Afisa
 Mafunzo wa TMF, Raziah Mawanga akizungumza jinsi TMF inawasaidia 
waandishi wa habari ili waweze kufanya kazi zao kwa weledi. Kushoto ni 
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri na Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la 
Wahariri (TEF), Deodatus Balile. Kulia ni Mwenyekiti wa MISATAN, Simon 
Berege na Ofisa Miradi katika Kitengo cha Mawasiliano na Tehama UNESCO, 
Nancy Kaizelege.

Ofisa
 Miradi katika Kitengo cha Mawasiliano na Tehama UNESCO, Nancy Kaizelege
 akizungumzia ushiriki wa UNESCO katika kuandaa Siku ya Uhuru wa Vyombo 
vya Habari ambapo kwa mwaka huu zinafanyika Mwanza. Kushoto ni 
Mwenyekiti wa MISATAN, Simon Berege na Afisa Mafunzo wa TMF, Raziah 
Mawanga.

Afisa
 Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia 
Nkhoma-Ledama akieleza kazi za Umoja wa Mataifa ili kuvisaidia vyombo 
vya habari kupata uhuru wa kufanya kazi bila kuingiliwa.

Baadhi ya waandishi wa habari na watumishi waliohudhuria mkutano huo.
0 comments:
Post a Comment