Pages

Ads 468x60px

Monday, June 20, 2016

Mama JANETH MAGUFULI akabidhi Vyakula Kwa ajili ya Futari

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akikabidhi sehemu ya vyakula hivyo kwa Mwenyekiti wa Kituo cha Charambe Islamic Center Dkt. Haruni Kondo aliyepokea kwa niaba ya vikundi vigine vinne. Mke wa Rais amekabidhi mchele kilo 500, sukari kilo 500 na tende kilo 28, tukio hilo limefanyika katika ofisi ya Mke wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam.
Khalifa wa Zawiyatul lqadiria, Abas Hamdan watatu kutoka kulia akiongoza dua ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na viongozi wengine wakuu wa serikali mara baada ya tukio la kukabidhi vyakula hivyo. Wengine katika picha ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli, Mke wa Waziri mkuu Mama Marry Majaliwa pamoja na viongozi mbalimbali vya vikundi vya kulea watoto yatima na watu waishio kwenye mazingira magumu.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na Mama Mlezi wa Kituo cha Charambe Islamic Center Asile Zahali mara baada ya kukamilika zoezi la utoaji wa vyakula mbalimbali kwa vituo vinne vya kulea watoto na watu waishio kwenye mazingira magumu. 
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa na mke wa Waziri Mkuu Mama Marry Majaliwa akizungumza na viongozi mbalimbali wa vituo hivyo kabla ya kuwakabidhi vyakula hivyo katika Ofisi yake Ikulu jijini Dar es Salaam. 

PICHA NA IKULU

0 comments:

Post a Comment