Pages

Ads 468x60px

Thursday, July 14, 2016

Rais Dkt MAGUFULI azindua Mpango wa Ugawaji Madawati Kwenye Majimbo

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akimuonesha Rais Dkt. John Pombe Magufuli sehemu ya Madawati yaliyotengenezwa na fedha zilizopatikana kutokana na kubana matumizi kutoka Ofisi ya Bunge katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amekaa kwenye moja ya Dawati katika hafla hiyo fupi ya ugawaji wa Madawati hayo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Bunge wakwanza kulia Mariam Elias (darasa la tatu na wapili kutoka kushoto George Samwel mwanafunzi wa darasa la tano wakiwa wanapiga makofi kabla ya tukio la ugawaji wa madawati hayo yaliyotokana na kubana matumizi kutoka Ofisi ya Bunge.
Mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya Msingi Bunge George Samwel akimtajia Mheshimiwa Rais Jina la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kumuuliza huku Waziri Mkuu akitazama kwa furaha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Mbunge wa Ilala Mussa Azzan Zungu ambaye aliyapokea kwa niaba ya Wabunge wa majimbo mbalimbali nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Mwanafunzi wa Darasa la tatu katika Shule ya Msingi Bunge Mariam Samwel wakati akiondoka kwenye viwanja hivyo.
Sehemu ya Madawati yaliyokabidhiwa leo.... 

0 comments:

Post a Comment