Pages

Ads 468x60px

Tuesday, June 12, 2012


Chama cha Demokrasia na maendeleo( Chadema ) kimeandaa semina ya siku mbili (2) kwa viongozi ili kuwajengea uwezo  na ufahamu wa kutenda kazi zao ndani ya chama, viongozi hao ni wa chama na madiwani wake.

Akiongea na MALAFYALELEO mwenye kiti wa chama hicho mkoa wa Mbeya PETER K MWAMBONEKE amesema wameamua kufanya semina hiyo kwa viongozi na madiwani wa chama hicho wa mikoa mitatu ikiwemo RUKWA, RUVUMA na MBEYA ili kuwapa uwezo na ufahamu viongozi wake wa kujua wajibu wao katika kufanya kazi za chama.

Na kwa upande wa madiwani kujua majukumu yao kwa Halmashauri na wananchi walio wachagua ili wawatumikie
Semina hiyo imeanza tarehe 12-13/06/2012 maeneo ya sokomatola katika ukumbi wa MKAPA jijini MBEYA.

Wakufunzi wa semina hiyo ni;
1.    BENSON S. KIGAILA (Mkurungenzi wa mafunzo)
2.    LAZARO T. MAASAY (Mwenyekiti wa Halmashauri Karatu) Pia mjumbe kamati kuu.
3.     SHABANI MBAMBO (Meya Kigoma)
4.    ERASTO NDENKA (Program officer wa KONRAD ADONAYER STIFTUNG(KAS)
Mafunzo hayo yamedhaminiwa na chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) Taifa kwa kufadhiliwa na shirika la KONRAD ADONAYER STIFTUNG (KAS) la jijini Dar-es-salaam.
 Program officer wa KONRAD ADONAYER STIFTUNG (KAS) ERASTO NDENKA akitoa mafunzo kwa washiliki wa semina na viongozi wa (chadema) Picha na charles mwaipopo.
 Mwenyekiti wa chadema mkoa wa MBEYA PETER K. MWAMBONEKE akiuliza swali kwa mwezeshaji wa semina.(Picha na charles mwaipopo)
 
 Baadhi ya viongozi na madiwani walioshiriki semina hiyo (Picha na charles mwaipopo)
Huu ndo ukumbi mdogo wa kumbukumbu ya Rais Benjamin Mkapa Wanako fanyia semina hiyo (Picha na charles mwaipopo)

0 comments:

Post a Comment