Pages

Ads 468x60px

Thursday, June 14, 2012


Jinamizi la ajari lazidi kulikumba Jiji la Mbeya ni mara baada ya basi doga aina ya Hiace yenye namba za usajili T247 BUF Linalo milikiwa na Huruma mwakasa  maarufu( Daladala) lililokuwa likifanya safari  zake kati ya mwanjelwa na mbalizi kuligonga Lori kwa nyuma lenye namba za usaji T 786 BBH Linalomilikiwa na kampuni ya malumalu jijini hapa, Na kusababisha watu zaidi ya (20) kujeruhiwa vibaya
Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo jun 14/2012 maeneo ya Ituta Iyunga barabara ya Mbeya na Tunduma.
Chanzo cha ajari hiya kwa mujibu wa abiria ni mwendo kasi wa Dereva ambeye  hatukupata majina yake kushindwa kulimudu gari hilo na kuligonga lori hilo lilikuwa limeegeswa pembeni mwa barabara.
Ajali hii imekuja mara tu wananchi na wakazi wa Jiji la Mbeya bado hawajasahau machungu ya Ajali mbaya ya coster iliyokuwa ikitoka Mbeya kwenda Kyela kugongwa na lori la mizigo, iliyopoteza maisha ya ndugu jamaa na marafiki na wengine kupata kilema cha maisha iliyotokea hivi karibuni maeneo ya uyole Mbeya vijijini.
 Hivi ndivyo basi dogo Aina ya Hiace maarufu kama daladala jinsi lilivyo ligonga Lori kwa nyuma. (Picha na Richard Mwafulirwa)
 Wauguzi wa hospital ya Rufaa Mbeya wakiwapeleka majeruhi wodini mara baada ya kutibiwa (Picha na Richard Mwafulirwa)
Mwandishi wa Blogger ya Malafyaleleo Richard Mwafulirwa akihojiana na mmoja wa Abiria Ester Ntenga Mkazi wa Mama john Aliyekuwemo katika Ajali hiyo
   Askari Polisi usalama Barabarani wakiwa eneo lililotokea Ajari 
(Picha na Richard Mwafulirwa)

 

0 comments:

Post a Comment