Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 4, 2012


Mwananchuo  wa chuo cha ualimu cha ST Aggrey  kilichopo uyole jijini mbeya anasadikiwa kufariki  dunia  baada ya kupigwa na wananchi  wenye hasira kali katika maeneo ya Isanga  kwa tuhuma zakuiba pikipiki zakusafirishia abiria  maarufu kama bodaboda.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo PRAY GOD  MGONJA  amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni VEDASTO PIUS anayekadiriwa kuwa na  umri  kati 25 mpaka 30 .
Mgonja  amesema  tukio hilo limetokea  mnamo july 2 mwaka huu majira ya saa  8 za mchana katika  daraja lilopo karibu na hotel ya Rift Valley barabara yakuelekea isanga jijini mbeya.
Amesema  mtuhumiwa amekumbwa na mkasa huo  baada yakupewa taarifa za kuibiwa kwa pikipiki yenye No T 438BZU aina T-BETTER yenye alama ya chama cha Demokrasia na maendeleo  mali ya JOSEPH  KAPASI(23)mkazi wa Ilomba jijini hapa.
Kwaupande wake  mmiliki wa pikipiki hiyo JOSEPH KAPASI amesema  aliombwa kumfundisha  mtuhumiwa  huyo na baadae alipoanza kuendesha vizuri alitokomea nayo   na marabaada  ya hapo alipatikana eneo la isanga akielekea barabara ya chunya ili aibe na ndipo akakamatwa na wanainchi wenye hasira kali nakuanza kumpa kichapo ambacho kimemfanya azirai.
TUNAOMBA LADHI KWA PICHA UTAKAZOZIONA KATIKA HABARI HII
 Vedastos Pius akiwa amelala chini baada kupata kichapo kwa tuhuma za wizi wa pikipiki
                                                          Kitambulisho chake cha Aggrey Teachers College
                                                     Picha yake kabla ya kupata kichapo
Mwandishi wa Blogg hii Charles Mwaipopo Akimhoji Praygod aliyefanikisha kumkamata anayetuhumiwa kwa wizi wa pikipiki

0 comments:

Post a Comment