Pages

Ads 468x60px

Wednesday, July 18, 2012


KANISA LA MORAVIANI TANZANIA KUWATENGA WAUMINI WAKE WATAKAO OA AMA KUOLEWA NA WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU.
WALIOPATA KIPAIMARA WATATENGWA WENYEWE WASIOPATA KIPAIMARA KUTENGWA WAZAZI WAO.
Hayo yamesemwa na mchungaji ALIYIZA SILUMBWE wa Kanisa la Moraviani Tanzania Jimbo la kusini Magharibi ushirika wa Chindi Wilyani Momba, Akiongea wakati wa kuendesha ibaada ya sikuku ya umoja wa akina mama iliyo fanyika kimtaa katika kanisa la Moravia ushilika wa Msangano Silumbwwe aliwataka wazazi kutowakubalia watoto wao kuoa ama kuolewa na waumini wa dini ya Kiislamu.
“Ndugu zangu wenzetu waislamu wamepanga mikakati ya kuumaliza ukristo kwa kuwashauri vijana wao kuoa mabinti zetu kwa gharama kubwa na kwa mabiti wao waolewe na vijana wetu kwa ahadi za kuwapa mali na mitaji ya kuanzia maisha katika ndoa zao ila wauache ukristo sasa basi kama kanisa limegundua hilo na kutoa tamko kuwa kila muumini asikubali mototo wake kuolewa na mtomto wa kiislamu”amesema Silumbwe.
 Maandamano ya wachungaji na akina mama katika sikuuu ya umoja wa akina mama mtaa wa Msangano Wilayani Momba.
 Mchungaji Aliyiza Silumbwe Akisisitiza jambo wakato wa ibaada hiyo
 Mwalimu wa shule ya jumapili mwanye ulemavu wa macho ushirika wa Msangano Mwenyekipaji cha aina yake kwa kusoma vifungu vyote vya Biblia. 
 Huu ni mnara wa kumbukumbu ya mwinjilisti wa kwanza AMBILISHISHE MWACHANIKA kupeleka Injili katika Bonde la Unyamwanga mwaka 1907-1911 Mnara huu umejengwa nje ya kanisa la Moraviani ushirika wa Msangano.

0 comments:

Post a Comment