Pages

Ads 468x60px

Monday, January 7, 2013

MBUNGE AMWAGA CHOZI WAKATI WA KUMSHUKURU MUNGU KWA KUMUOKOA NA AJARI MBAYA


NI KATIKA IBAADA MAARUMU ILIYOFANYIKA KATIKA KANISA LA MORAVIANI USHIRIKA WA RUANDA

 

Mbunge wa viti maalumu jijini mbeya MARY MWANJELWA amemwaga machozi ya uchungu kumshukuru mungu kwa kumuokoa na ajari mbaya iliyo kuwa imetokea October 2 mwaka jana maeneo ya mbalizi mbeya vijijini iliyoghalimu uhai wamaisha ya watu zaidi ya kumi na moja.

Tukio hilo limetokea katika ibaada iliyoandaliwa maalumu kumshukuru mungu iliyofanyika katika kanisa la moraviani ushirika wa RUANDA kisha kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa serikali na kidini akiwemo baba Askofu kiongozi wa kanisa la Moraviani Tanzania ALINIKISA CHEYO.

Wengine ni Naibu Waziri wa elimu na ufundi PHILP MULUGO mkurugenzi wa shirika la nyumba MANYAMA mwenyekiti wa vijana uvccm AMANI KAJUNA pamoja na madiwani wa kata mbalimbali.
Katika ibaada hiyo MARY pamoja na familia yake walitoa shukurani yao ya pekee  pesa ambazo hazikitajwa kiasi gani, pia alitoa msaada wa baiskeli kumi kwa wenye ulemavu wa viungo

MARY ameshukuru sana mungu kumtoa katika ajali ambayo wengine walopoteza maisha yao akiwemo katibu wake ambaye aliteketea papo hapo kwa moto, Amewataka waumini na wanachi wote kuiombea amani inchi yetu na mkoa wa mbeya ili kuondokana na machafukao yanayo tokea kila wakati pasipo na sababu.

Aidha kwaupande wake Naibu waziri elimu na ufundi PHILP MULUGO amempongeza MARY MWANJELWA kwakumkumbuka mungu kuwa ndiye aliye mponya na ajari hiyo na kisha kumshuru, Amewataka waumini kujifunza mfano huo na  kutomuacha mungu kwani ndiye muweza wa mambo yote.

Naye Askofu kiongozi wa kanisa la moraviani Tanzania ALIKISA CHEYO amesema tendo alilotenda hapa ni jema tena amemuheshimu sana mungu na hata kwa wana jimii nzima kwa kuwakumbuka watu wasio jiweza na wenye ulemavu kwakutoa nyenzo itakayo warahisishia kutembea.

Ameongeza kuwa hakuwasaidia walemavu tu bali ni kwa wana MBEYA wote kwa tendo hili tutamkumbuka katika maisha yetu yote na mungu aendelee kumzidishia Baraka tele.

0 comments:

Post a Comment