Machafuko
 makubwa yametokea leo katika kijiji cha Buseresere Wilayani Chato 
Mkoani Geita kati ya waslam na wakristu na kupelekea watu 10 kujeruhiwa 
vibaya kwa mapanga huku mchungaji wa kanisa la Pentekoste Assemblies of 
God Mathayo Kachila (45) akipoteza maisha kwa kuchinjwa na watu 
wanaodaiwa ni waumini  wadini ya kiislam kisha mwili wake kutelekezwa 
kwenye vibanda vya maduka ambavyo vilikuwa jirani na eneo hilo.
Habari
 za kaminika eneo la tukio hilo lililotokea majira ya asubuhi zimeeleza 
kuwa chanzo cha machafuko hayo ni watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wadini ya
 kiislam kuvamia bucha lililokuwa likiwauzia nyama wakristo wa kijiji 
hicho waliokuwa wamepanga foleni kwa wingi kusubili huduma hiyo.
Imeelezwa
 kuwa Wakristu hao walikuwa wamechinjia ng'ombe mmoja na mbuzi wawili 
eneo la Kanisani kabla ya kuleta nyama hiyo katika bucha hilo lililopo 
eneo la Buselesele Sokoni na ndipo walipokumbana na kadhia hiyo ya 
waislamu.
Tukio
 hilo lilianza majira ya saa 2 asubuhi muda mfupi baada ya nyama 
kuwasili katika bucha hilo la wakristu kwa ajili ya kuuzwa jambo 
linalodaiwa liliwakera waislam ambao waliivamia bucha hiyo kwa lengo la 
kuifunga.
Wakati
 wakristo wakitafakari uwepo wa waislam kwenye bucha lao lililpambwa kwa
 maandishi BWANA YESU ASIFIWE,YESU NI BWANA, ndipo waislam ambao kwa 
wakati huo walikuwa wametapakaa mtaani kwa lengo la kuhamasishana 
waliongezeka eneo lilipo bucha hilo na kisha kuimwagia nyama iliyokuwa 
kwenye bucha hilo vitu vinavyodaiwa kuwa ni sumu.
Kutokana
 na hali hiyo wakiristo walionekana kukerwa na kitendo cha waislam 
kuimwagia nyama hiyo vitu hivyo na kisha mapambano yalianza baina ya 
wakristu na waislam ambapo mbali na wakristu kutumia mawe waislamu wao 
walitumia mapanga na majambia.
Hata
 hivyo wakati mapambano hayo yakiendelea mchungaji huyo ambaye kwa sasa 
ni marehemu alifika eneo la tukio ili kujua kulikoni na ndipo naye 
alipojikuta akishambuliwa kwa mapanga sehemu mbalimbali za kichwa chake 
na alifia njiani wakati akikimbizwa katika hospital ya Wilaya ya Geita 
kwa matibabu zaidi.
Mbali
 na mchungaji huyo kupoteza maisha,wengine waliojeruhiwa ni pamoja na 
Said Ntahompagaze(45),Sadick Yahaya(40),Yasin Rajab(56),Vicent 
Damon(22),wote wakazi wa Buselesele na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina 
moja la Ramadhani ambaye yuko mahututi katika wodi namba nane katika 
hospital ya wilaya ya Geita.
Hata
 hivyo watu wengine watano ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara 
moja walitibiwa na kuruhusiwa kutokana na hali zao kuwa nzuri.
Jeshi
 la polisi Wilayani Chato na Geita lilifika eneo la tukio hilo majira ya
 saa 4:30 na kukuta uharibifu mkubwa umekwishafanyika ikiwa ni pamoja na
 kukuta duka la Mwenyekiti wa BAKWATA wilaya ya Chato Yusuph Idd 
linalotumika kwa biashara ya M-Pesa na vinywaji baridi likiwa 
linateketea kwa moto uliodaiwa kuwashwa na waumini wa dini ya kiislam.
Mkuu
 wa Wilaya ya Chato Ludorick Mpogolo aliyefika eneo la tukio muda mfupi 
baada ya polisi kuwasili eneo hilo mbali na kusikitishwa na kitendo 
hicho aliwataka wananchi kuwa watulivu wakati serikali ikiangalia njia sahihi za kutatua mgogoro huo ambao unakuwa kwa kasi kila kukicha.
Akizungumza
 kwa njia ya simu na gazeti hili mkuu wa Mkoa wa Geita Magalula Said 
Magalula mbali na kuthibitisha kuwepo kwa tukio hilo, alionyesha kukerwa
 na watu ambao wanafurahia vurugu zisizo na msingi na kuonya 
kuwashughulikia wale wote watakaobainika ni wachochezi wa masuala ya 
kidini.
0 comments:
Post a Comment