Pages

Ads 468x60px

Wednesday, March 20, 2013

GLOBAL NEWS: PAPA FRANCIS ATAWAZWA



Baba Mtakatifu Francis, leo ametawazwa rasmi kuliongoza Kanisa Katoliki duniani katika Ibada ya Misa inayofanyika kwenye Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican. 
 http://static.guim.co.uk/sys-images/Guardian/Pix/pictures/2013/3/19/1363679536671/Pope-Francis-drives-throu-010.jpg
Katika Ibada hiyo, Baba Mtakatifu Francis amevalishwa pete ikiashiria sasa amekuwa Baba Mtakatifu wa 266. Ibada hiyo inahudhuriwa na waumini wengi, tangu Mei, mwaka 2011 ambapo zaidi ya watu milioni 1.5 walifika Vatican kuhudhuria sherehe za kutangazwa mwenye heri, Papa Yohana Paulo wa Pili . Viongozi 130 kutoka duniani kote, wanahudhuria Ibada hiyo, akiwemo Makamu wa Rais wa Marekani, Joe Biden na Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe.

0 comments:

Post a Comment