Pages

Ads 468x60px

Monday, April 28, 2014

WAUMINI WA DINI YA KRISTO WAMETAKIWA KULINDA SANA AMANI


MWINJILISTI ESAU MWAMTOBE





KWAYA KUU YA KANISA LA MORAVIANI USHIRIKA WA IWAMBI AMBAO WALIKUA KIVUTIO SANA KWA UIMBAJI WAO KATIKA IBAADA HIYO

KWAYA KUU YA USHIRIKA WA MBEYA MJINI WAKITMBUIZA KATIKA IBAADA
                       KWAYA YA SHULE YA JUMAPILI USHIRIKA WA MBEYA MJINI

                                KWAYA YA UINJILISTI USHIRIKA WA MBEYA MJINI





KWAYA YA VIJANA USHRIKA WA MBEYA MJINI WAKIONGOZA NYIMBO ZA KUABUDU ZIKIONGOZWA NA MWENYEKITI WA MICHEZO PENIELI MWAISANGO










ASILI YA JINSI YA KUONGOZA NYIMBO KWA KUPIGA MAPIGO KUTOKA KWAYA KUU IWAMBI

                                                                    HABARI KAMILI



WAUMINI WA DINI YA KRISTO WAMETAKIWA KULINDA SANA AMANI
KWAKUA NDIYO THAMANI YA MAISHA YA MWANADAMU HAPA DUNIANI

Hayo yamesemwa na mwinjilisti ESAU MWAMTOBE wa kanisa la Moraviani Tanzania Jimbo la kusini magharibi ushirika wa Mbeya mjini alipokua akihubiri katika ibaadailiyofanyika kanisani hapo  jumapili ya kwanza baada ya Pasaka, akisoma samo kutoka yohana 20:19-31 ambalo yesu alipo fufuka aliwaombea wanafunzi wake Amani.

Ili kuipata Amani ni lazima watu wamtegemee mungu na kumtumikia kwa uaminifu, akinukuu maandiko kutoka katika Biblia MWAMTOBE amesema  utafuteni kwanza ufalme wa mungu na mengine yote mtazidishiwa, watu wamekua wakitafuta Amani na furaha katika kujilimbikizia mali kitu ambacho ni ubatili mtupu

Wakristo wamekua wakikwepa majukumu yao katika kumtumikia mungu ili kueneza ijili yake ulimwenguni kote na kusababisha baadhi ya watu wengine kushindwa kumjua mungu na kukosa Amani  katika maisha yao na hivyo wengi watakosa kuiona mbingu kwa kukosa la kutomtumikia.

MWAMTOBE ameongeza kua hakuna jambo la muhimu katika maisha ya mwanadam zaidi ya Amani na ndicho kitu chenye thamani kubwa, Ameongeza kua wapo watu wana mali na kila kitu kilichopo duniani lakini hawana furaha moyoni mwao kutokana na kutokuwa na Amani.

0 comments:

Post a Comment