Pages

Ads 468x60px

Friday, April 25, 2014

Chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) kimemtuhumu meya wa jiji la mbeya kuendesha njama za kumfunga jela mwenyikiti wao mtaa wa itiji



Ezekieli king alieye hukumiwa kutumikia kifungo cha miaka saba kwa kosa la kupiga na kujeruhi.

Mwenyekiti Wa Chadema kata ya Itiji Daniel Mwakasita akiongea na mwandishi wa habari hii
Mwenyekiti wa mtaa wa itiji Ezekiel King akiwa kizimbani baada ya kuhukumiwa
                       Meya wa jiji la Mbeya Atanas kapunga ( Picha na Libraly yetu)

                                                                    Habari Kamili

Hayo yamesamwa na DANIELI MWAKASITA mwanyekiti wa kata ya Itiji kupitia chama hicho katika ofisi za wilaya ya mbeya mjini walipokua wakushughulikia rufaa ya kupinga hukumu hiyo
MWAKASITA  amemtupia lawama meya wa jiji la mbeya ATANASI KAPUNGA kuhusika na hukumu hiyo kua haikuwa na haki na kunasiasa ndani yake kutokana na kutokuwepo kwa mahusia mazuri kati yake na mwenyekiti huyo kutoka na kukihama chama chake mapinduzi (ccm) kwenda chadema

Ameongeza kua meya huyo alijitapa katika moja ya mikutano yake ya hadhara kwamba atahakikisha mwenyekti huyo ametumia gharama yoyoe kumfunga na sasa adhima yake imetimia na wao kama wanachama wa chadema hawako tayali kukubaliana na hukumu hiyo hivyo wana kata rufaa na kuweka wakili wa kumtetea kiongozi wao.

Nae DOMI MWASALEMBA mmoja wa wafuasi wa chama hicho amehoji hukumu hiyo kuwa haikua na haki kutokana na kesi kutofuta ushahidi wa kidaktali kwamba anaedai kupigwa anatatizo la ugojwa wa akili na kwamba alileta fujo kilabuni akapingwa na watu wengine lakini amemtaja king kwakua ndiye aliye mpeleka Polis kisha Hospital

Awali mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Itiji Jijini Mbeya mkoani Hapa anayewakilisha (CHADEMA) Ezekiel King(52) na mwenzake Antony Simon(53) wamehukumiwa kwenda jela miaka 7 kutokana na makosa ya shambulio na kumdhuru mwili Nicholaus Mwakasinga(56) mkazi wa Itiji mjini humo.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu mkazi wa mahakama ya Mkoa wa Mbeya Maria Batulaine, mbele ya mwendesha mashtaka wa serikali Juliana William alisema kuwa washitakiwa kwa pamoja walimshambulia Mwakasinga kwa kumpiga na kumjeruhi kichwani na mkononi wakati wakiwa katika kilabu cha pombe za kienyeji kilichopo mtaa wa Itiji.

Alisema anawatia hatiani washitakiwa hao kutoka na kuwepo kwa mashaka juu ya ushahidi wa watu watatu  upande utetezi kugongana na hivyo kuridhika na ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka  na hivyo kuwatia hatiani na kwamba hata hivyo wanayo fursa ya kukata rufaa iwapo hawajaridhika na hukumu iliyotolewa.


 

0 comments:

Post a Comment