Pages

Ads 468x60px

Saturday, April 12, 2014

JESHI LA POLISI LIMEFANILIWA KUZIMA VURUGU ZA MADEREVA WA BODABODA MKOANI MBEYA

Awali leo asubuhi waendesha bodaboda hao waliandamana baada ya mwenzao mmoja aliyefahamika kwa jina la Siza Mwambenja kuuawa na mtu anayedaiwa kuwa alitumwa na mkewe kufanya mauaji hayo.


Wananchi wakiandamana kufunga barabara ya Esso

Askari wa jeshi la polisi tarafa ya sisimba akizongwa na waendesha bodaboda eneo la mafiati             

Barabara zimefungwa kwa kuwekwa mawe eneo la Esso




KIKOSI CHA KUZUIA FUJO WAKIJAZA MAJI YA KUWASHA TAYARI KWA MAPAMBANO

Vurugu tupu 

Gari ya Polisi iliyovunjwa kioo







Mkuu wa polisi wilaya ya Mbeya Richard Mchomvu akiwasihi vijana kuacha vurugu

Askari mlezi wa bodaboda Lema akiwataka vijana wa bodaboda kufungua barabara ya Mafiati






BAADHI YA DEREVA BODABODA WALIOKAMATWA KATIKA VURUGU HIZO WAKISHUSHWA KATIKA KTUO CHA KATI JIJINI MBEYA

                                                                      HABARI KAMILI
Chanzo cha vurugu hizo inasemekana waendesha bodaboda  waliandamana baada ya mwenzao mmoja aliyefahamika kwa jina la Siza Mwambenja kuuawa na mtu anayedaiwa kuwa alitumwa na mkewe kufanya mauaji hayo.

Ilielezwa kuwa marehemu aliachana na mkewe ambapo mke inadaiwa alimtumia watu wamdhuru mumewe kwa kile kilichoelezwa kuwa mwanaume huyo aliamua kuachana na mkewe na kuishi sehemu nyingine kutokana na madai kutoelewana katika ndoa yao kwa mmoja kati yao kukosa uaminifu ndani ya ndoa.

Baada ya tukio hilo la mauaji kutokea, inadaiwa kuwa mtuhumiwa ambaye ni mke wa marehemu alikamatwa na polisi ndipo waendesha bodaboda walielekea katika eneo hilo na kutaka kuchukua sheria mkononi kumnyang'anya mtuhumiwa aliyekuwa chini ya ulinzi wa polisi ili wamuadhibu.

Kitendo hicho kilisababisha kuibuka kwa tafrani baina ya Jeshi la Polisi na waendesha boda boda ambao walikuwa wakihitaji kumchukua mtuhumiwa ambapo walifuatilia gari la polisi hadi kituo cha Polisi na baadaye kufunga barabara kwa kuweka mawe, ndipo mabomu yalipoanza kurushwa na kuibuka kwa vurugu katika maeneo ya Mafiat, Oilcom, Magorofani na Iyela.

Akizungumza tukio hilo Mwenyekiti wa waendesha Bodaboda Jiji la Mbeya Vicent Mwashoma alisema kuwa tukio hilo limewachanganya sana na kwamba yeye kama kiongozi alipata taarifa za kuibuka kwa vurugu wakati polisi wamekwisha anza kurusha mabomu.

Alisema kuwa hata hivyo Jeshi la Polisi lilipaswa kuwasiliana na uongozi wa waendesha bodaboda ili kufanya mazungumzo kabla ya kuchukua hatua hizo ambazo zimesababisha madhara kwa watu wengine ambao hawakuhusika katika tukio hilo.

0 comments:

Post a Comment