Pages

Ads 468x60px

Monday, May 19, 2014


SERIKALI MKOANI MBEYA  IMEWATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHALI YA UWEZEKANO WA KUWEPO KWA NYOKA MKUBWA KATIKA MTO WA SHULE YA SEKONDARI MBEYA DAY

Hayo yamebainishwa nae JOSEPH BUTUYUYU afisa mali ya asili mkoni mbeya alipokua akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofini kwake Butuyuyu amewataka wanachi kuto dharau kuwepo kwa taarifa zanyoka mkubwa katika mapango ya mto unaopita kati shule ya sekondali ya mbeya day

Ameongeza kuwa Serikali imepata taarifa hizo na sasa tayali imechukua hatua ya kuiagiza Halmashari ya jiji la mbeya kutafuta wataaram wanao weza kumtafuta nyoka huyo na kisha kumpeleka katika ya hifadhi ifisi na tayali wataalamu hao kutoka chunya na chalinze wamekwisha wasili na kuianza kazi hiyo mala moja

Kwa upande wake mtaalam wa kumtafuta nyoka huyo Athumani Kenthi kutoka wilayani chunya amethibisha kuwepo na dalili ya kuwepo kwa nyoka  kutokana na kuziona alma za njia anazopita na kwamba wanaendelea kumtafua na kutoa wito kwa wwananchi watakao weza kumuona kutoa taarifa katika maraka husika ili kuharakisha zoezi hilo.

Athumani ameongezakuwa zoezi hilo ni gumu na kuna uwezekano wa kuchukua muda mrefu kutokana na tabia ya nyoka huo kuto onekana mara kwa mara endapo kameza mzoga mkubwa mpaka pale utakapo kua umeozesha Lakini hilo haliwakatishi tamaa mpaka atakapo patikana.

Nae mmoja wa wanafunzi wa shule ya mbeya sekondari inayo pakana na mto huo Gasto Mtega ameiomba serikali kuchukua hatua za makusudi na za haraka kwani mpaka sasa wamekua wakiishi kwa mashaka kutoka kuzagaa kwa habari  hizo ili kukabiliana nae kabla hajatoa madhara kwa wanadamu.

0 comments:

Post a Comment