Pages

Ads 468x60px

Tuesday, May 20, 2014

FUATILIA SAKATA LA UTAFUTAJI WA NYOKA MKUBWA ANAETISHIA MAISHA YA WAKAZI WA JIJI LA MBEYA


SERIKALI MKOANI MBEYA  IMEWATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHALI YA UWEZEKANO WA KUWEPO KWA NYOKA MKUBWA KATIKA MTO WA SHULE YA SEKONDARI MBEYA DAY
 Afisa mali ya asili mkoa wa Mbeya Joseph Butuyuyu akiongea na mwandishi wa blog hii ofisini kwake

muonekano wa sehemu inayosemekana kuwepo kwa chatu anae meza mbwa na mbuzi maeneo ya sabasabana shule ya Mbeya sekondari



Baadhi ya njia zinazotiliwa shaka kiwepo kwa chatu mkubwa lakini bado watu wanapita bila shaka hapa ni daraja linalopitisha watu kutokea kichochoro kati Tanrod na Mbeya Sekonari


 Moja ya maeneo ya mto unaodhaniwa kuwepo na chatu mkubwa

Vinjia vilivyopo pembezoni mwa mto na wigo wa mbeya sekondali vinavyotumika kupita watu pamoja na kuwepo kwa tahadhari ya nyoka mkubwa



 Hata hivyo shughuri za kuoga bado zinaendelea kwa wakazi waliopo karibu na mto huo
Wananchi bado wanatumia daraja linalo wavusha kutoka jakaranda kwenda katika makaburi ya sabasaba

Wanafunzi wa Mbeya sekondari wanaendelea na shughuri zao japo nje ya wigo huo niko anakosakwa chatu

Katika mapolomoko haya kuna mti mkubwa mkavu inasemekana ndipo yalipo makazi ya chatu huyo
Mtaala wa kukamata nyoka Mazoea Hamisi toka Chalinze akiwajibika kumtafuta chatu Huyo

Wataalam wa kukamata nyoka wamefanikiwa kumkata nyoka wa kijani

Mazoea alikosea kumkamata nyoka aliruka na kumgonga kidole gumba


Mtaalamu wa kukamata nyoka akifanikiwa kumdhiditi tena nyoka huyo


Hapa akitoa meno ya nyoka kisha kujitibia kwa dawa zake



 kazi ya kusaka nyoka huyo inaendelea kwa kuzama mapangoni na mapolini





Hatimaye tumaini linaongezeka baada ya kumnasa mmoja wa chatu hao ambao inasemekana ni mtoto na kuna uwezekano wa kuwepo wazazi wake

Tuna mshukuru mchina kwa kutuletea simu zenye kamera na hawa ni wakazi wa jiji la mbeya waliojitokeza kumuona nyoka huyo

                                    Habari kamili

SERIKALI MKOANI MBEYA  IMEWATAKA WANANCHI KUCHUKUA TAHADHALI YA UWEZEKANO WA KUWEPO KWA NYOKA MKUBWA KATIKA MTO WA SHULE YA SEKONDARI MBEYA DAY

Hayo yamebainishwa nae JOSEPH BUTUYUYU afisa mali ya asili mkoni mbeya alipokua akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofini kwake, Butuyuyu amewataka wanachi kuto dharau kuwepo kwa taarifa zanyoka mkubwa katika mapango ya mto unaopita kati shule ya sekondali ya mbeya day

Ameongeza kuwa Serikali imepata taarifa hizo na sasa tayali imechukua hatua ya kuiagiza Halmashari ya jiji la mbeya kutafuta wataaram wanao weza kumtafuta nyoka huyo na kisha kumpeleka katika ya hifadhi ifisi na tayali wataalamu hao kutoka chunya na chalinze wamekwisha wasili na kuianza kazi hiyo mala moja

Kwa upande wake mtaalam wa kumtafuta nyoka huyo Athumani Kenthi kutoka wilayani chunya amethibisha kuwepo na dalili ya kuwepo kwa nyoka  kutokana na kuziona alma za njia anazopita na kwamba wanaendelea kumtafua na kutoa wito kwa wwananchi watakao weza kumuona kutoa taarifa katika maraka husika ili kuharakisha zoezi hilo.

Athumani ameongezakuwa zoezi hilo ni gumu na kuna uwezekano wa kuchukua muda mrefu kutokana na tabia ya nyoka huo kuto onekana mara kwa mara endapo kameza mzoga mkubwa mpaka pale utakapo kua umeozesha Lakini hilo haliwakatishi tamaa mpaka atakapo patikana.

Nae mmoja wa wanafunzi wa shule ya mbeya sekondari inayo pakana na mto huo Gasto Mtega ameiomba serikali kuchukua hatua za makusudi na za haraka kwani mpaka sasa wamekua wakiishi kwa mashaka kutoka kuzagaa kwa habari  hizo ili kukabiliana nae kabla hajatoa madhara kwa wanadamu. 
                                        Mwisho



0 comments:

Post a Comment