Mashabiki wamtaka Kocha wa timu hiyo
Juma mwambusi kujiuzuru.
Kocha Mbeya city Juma mwambusi akiongea na vyombo vya habari (Picha na maktaba yetu)
Timu zote mbili zikiingia uwanjani kisha kukaguliwa nakuanza mtanange
Kila timu zikifanya Dua kwaimani yake
Mashabiki waliojitokeza kushangilia timu yao
Tazama katika habari picha jinsi mchezo huo ulivyo kwenda
Baada ya kufungwa gori la pili mashabiki wakaanza kurusha mawe na makopo ya maji uwanjani
Baadhi ya wachezaji na mashabiki wakitoka uwanjani wakilia machozi
Habari soma hapa
Na, Charles Abraham
Timu ya Mbeya city mambo yanazidi
kuwaendea kombo Yachezea kichapo na Mtibwa suger,
Mashabiki wamtaka Kocha wa timu hiyo
Juma mwambusi kujiuzuru.
Ni siku
chache zimepita tangu timu ya Mbeya city iendeleze uteja kwa wana lambalamba
Azam fc wa jijini dare s slaam kwa kuchapwa gori 1-0 na kuwatia machungu
mashabiki wake ambao msimu uliopita walikua wakisherehekea raha za ushidi.
Jana tena
timu hiyo imeendelea kuwanyima raha mashabiki hao kwa kuchezea kiminyo cha bila
huruma 2-0 kutoka kwa wakata miwa Mtibwa Suger ya mjini Morogoro na kuwafanya
wacharuke na kurusha mawe ndani ya uwanja baada ya kupachikwa bao la pili.
Mashabiki
hao wakiongea kwa nyakati tofauti wamemtaka kocha wa timu hiyo Juma mwambusi
kuchukua hatua ya kujiuzuru kutokana na kuwa yeye ndiye chanzo cha matokeo na
mwenendo mbovu wa timu yao.
Akiongea moja
wa mashabiki hao Razalo Mgwenda huku akitokwa machozi ameutaka uongozi kuchukua
hatua za makusudi haraka iwezekanivyo kuongea na wachezaji kujua nini tatizo ili
kuinusuru timu hiyo kabla haijafikia pabaya zaidi.
“Mimi
nimechoshwa na kila wikiendi kuumizwa kichwa kwa kuja kushangilia timu yangu
lakina haifanyi vizuri kila siku inafungwa kuanzia leo siji tena huku siko
tayali kukosa raha kwani timu yenyewe haitupi hata nafuu ni kutuumiza tu”
amesema shabiki huyo.
Pamoja na
hayo kumekua na tetesi kutoka wadau hao wakiendelea kumtupia lawama Juma
mwambusi kwa kuwapanga wacheza kwa manufaa yake binafsi, wamesema kuwa endapo mchezaji
hakumpatia asilimia fulani ya posha yake hawezi kupewa nafasi ya kucheza.
Katika
malalamiko hayo inasemekana wachezaji wenye uwezo hawakubaliani na hilo hivyo
hawampatii posha hiyo kwa kuringia uwezo walionao na ndipo hawapangwi na ikitokea
kacheza basi ni hucheza dakika chache za mwisho wa mchezo.
Kwa upande
wake kocha huyo ameyapokea matokeo hayo kwani amekiri na kuona umuhimu wa kukaa
na wachezaji wake ili kuangalia ni nini kilicho wapata msimu huu kwa kua hii ni
mchezo wa pili wanapoteza wakiwa kiwanja cha nyumbani.
“ Nikweli
nimepokea matokeo haya kwauchungu sana kuna haja kubwa kukaa na wachezaji wangu
kuangali nini kimetokea kwakuwa hii ni mechi ya pili tunapoteza tukiwa nyumbani
kitu ambacho hakijazoeleka Tutakaa chini Tujipange tuone cha kufanya” Amesma
mwambusi
Nae kocha
wa Mtibwa Suger Mecky mexime amekiri kuwa mechi anazo kutana nazo ni ngumu lakini
wamejipanga vizuri amewasifia wachezaji wake kuwa wana hali ya kushinda nakwamba
nafasi waliyopata wamezitumia vizuri na
ndio maana wamepata matokeo hayo.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment