Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abass Kandoro akiongea na wana mkutano uliofanyika katika ukumbe wa Mtenda Soweto
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mtenda Kyela Rice co. LTD George Mtenda
Mwenyekiti wa bod Stela Mtagwaba akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi
Kwa niaba ya wakulima Oden Simkwai kutoka wilayani Momba akisoma Risala
Baadhi ya wakulima waliohudhulia mafuzo hayo
Burudani kutoka kikundi cha Awilo kilimfanya mkuu wa mkoa kushuka jukwani na kumtunza mtoto aliekua kivutio kwa wana mkutano
Wajumbe katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro
Mchele Safi wa kyela kutoka kampuni ya usindikaji na uuzaji ya Mtenda Kyela Rice co (LTD)
SOMA HAPA
NA, Charles Abraham
Kandoro azindua muungano wa makampuni matatu katika sekta ya kilimo na kuyataka yawe na mikataba itakayowanufaisha wakulima Nchini.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mtenda Kyela Rice co. LTD George Mtenda
Mwenyekiti wa bod Stela Mtagwaba akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi
Kwa niaba ya wakulima Oden Simkwai kutoka wilayani Momba akisoma Risala
Baadhi ya wakulima waliohudhulia mafuzo hayo
Burudani kutoka kikundi cha Awilo kilimfanya mkuu wa mkoa kushuka jukwani na kumtunza mtoto aliekua kivutio kwa wana mkutano
Wajumbe katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro
Mchele Safi wa kyela kutoka kampuni ya usindikaji na uuzaji ya Mtenda Kyela Rice co (LTD)
SOMA HAPA
NA, Charles Abraham
Kandoro azindua muungano wa makampuni matatu katika sekta ya kilimo na kuyataka yawe na mikataba itakayowanufaisha wakulima Nchini.
Katika kutekeleza
kauli mbiu ya kilimo kwanza, makampuni
matatu yameunganisha nguvu ya pamoja ili kuimarisha na kuwasaidia wakulima kukuza kipato na uchumi katika sekta hiyo.
Shilikisho
hilo lililozinduliwa likiambatana na mafunzo ya kilimo bora cha mpunga kwa wakulima
limeziunganisha kampuni ya Mtenda Kyela
rice co. LTD, Tanseed International na Yara (MTAYArF)
Akiongea
katika uzinduzi huo Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro ameyataka makampuni
yaweze kuwanufaisha wakulima katika mikataba watakayo kua wakiingia nao isiwe
ya kuwakandamiza na hivyo kushindwa kunufaika na misaada pamoja na mafunzo
mnayo wapatia.
“Nawapongeza
sana wakurugenzi wa kampuni hizi tatu kwa kuchukua uamuzi wa kuunganisha nguvu
ya pamoja katika kuendeleza shughuri za kilimo nchini, ninawaomba kupitia
makampuni yenu muwasaidie wakulima kujiunga katika vikundi ili nao wawe na
nguvu ya kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo cha kisasa” Amesema Kandoro
Ameongeza kuwa
pamoja na umoja huo na kwa manufaa kwa kuwasidia wakulima kwa kuangalia mikataba
ikae vizuri isiwe ya kuwandamiza bali iwe yenye kuwasaidia ili kujikwamua
kiuchumi na kuleta maendeleo katika familia zao, pamoja na hayo serikali imekuwa
ikitoa mchango wake kwa kwajengea miundo mbinu bora.
Kwa upande
wake mmoja wawakulima Odeni Simkwai toka msangano Wilaya Momba amepongeza sana
kampuni ya Mtenda rice kwa mchango wake na misaada kwa wakulima kwani limewanufiasha
kwa pembejeo na bei nzuri kwa ununuzi wa mazao yao.
Awali akisoma
Risara kwa mgeni rasmi Stela Mtagwaba mwenyekiti wa bodi hiyo amesema lengo la
shilikisho hilo ni kupambana na changamoto wanazokutana nazo ikiwa ni ukosefu
wa masoko ya uhakika, uzalishaji mdogo na ubora usiolidhisha.
“Ni vizuri
ukajua lengo la shilikisho hili utakalolizindua hivi punde japo kwa ufupi, kampuni
hizi tatu pamoja na wakulima wa mpunga zimebaini vikwazo katika kilimo cha mpunga
ikiwa ni kutojua mbinu za kilimo cha kisasa, pamoja na kutotumia mbegu bora,
pia hawajui sayansi ya udongo,
Ameongeza
kuwa kwa kuona hayo kampuni ya ununuaji wa mpunga, usindikaji na uuzaji wa
mchele Mtenda Kyela rice, kampuni ya mbegu bora Tanseed International, Kampuni
ya mbolea ya Yara na wakulima wa mpunga wa Kyela,Mbarali na Momba wameamua
kuunda umoja huu ili kuunganisha nguvu ya pamoja katika kuleta maendeleo yao.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment