Pages

Ads 468x60px

Wednesday, October 1, 2014

Ukatili wa kijinsia bado ni tatizo kubwa nchini Tanzania



Wazee wanyanyaswa na kunyang`anywa milki zao huko matema wilayani Kyela
Mbeya Moraviani Town choir watembelea na kujionea kisha kuwapatia misaada mbalimbali


Waimbaji wa nyimbo za injili mkoni mbeya Town choir wakiwa na wenyeji wao tayali kwa kuwatembelea wazee



 Bibi amelala chini ishara ya kushukuru baada ya kupewa zawadi na wanakwaya hao, Bibi huyu ameachwa na wajukuu wanne na watoto wake waliofariki wakiwa wanantegemea na hana kipato chochote
           Vijana hao wakiondoka kwenda kaya nyingine






Bibi huyu hana ndugu yoyote wakumsaidia na hiyo ndiyo nyumba yeke amejengewa na wasamalia wema haina choo wa jiko na maisha yanaendelea kijana mmoja yohana kajange amejitolea bati ili kuezeka ama kujenga upya nymba hiyo.

Baadhi ya waimbaji watokwa na machozi walishindwa kuvumilia waliyokua wakiyaona jinsi wazee hawa wanavyopata tabu katika maisha yao 
                                        Ziara inaendelea



Bibi huyu ana mtoto mmjoa lakini amemtelekeza kwamba amewahi mtukana hivyo hampi msada wowote na anasumbuliwa na kifua kikuu hivyo anahudumiwa na wasamalia wema.

Hiyo ni nyumba ya bibi hawa wawili ni mtu na mdogo wake wamefukuzwa kutoka katika miji ya waume zao baada ya kufa hivyo wamerudi nyumbani kwao na kujengeawa kibanda hicho ambacho hujihifadhi.









Hii ni nyumba ya bibi huyo hapo juu ambae tulimkuta amelala chini ya kivuli cha mti akiwa hana mtu wa kumsaidia







Huyu anaumwa kavimba miguu na hana  mtu wa kumtuma amletee hata maji ya kunywa


                            Ziara bado inaendelea





         Zaidi ya kaya 25 zilipewa msaada na waimbaji hao

















                           Baada a ziara mambo kunoga




Ziara ya siku mbili sasa ni wakati wa maandalizi ya kulejea jijini

                                 Soma habari hapa



Ukatili wa kijinsia bado ni tatizo kubwa nchini Tanzania
Wazee wanyanyaswa na kunyang`anywa milki zao huko matema wilayani Kyela

Pamoja na mashirika malimbali yesiyo ya kiserikali nchini yanayo pinga na kutoa elimu ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia hari hiyo bado ni kitendawili katika jamii ya watanzania.

Hali hiyo imegundulika baada ya kikundi maarufu cha uimbaji wa nyimbo za Injili Nchini Mbeya moraviani town choir cha kanisa la moraviani ushirika wa mbaeya mjini kufanya ziara huko matema.

Kikundi hicho kimefanya ziara ya kuwatembelea wazee wanaoishi mazingira magumu katika kijiji cha matema kilichopo wilayani Kyela na kukuta hali hiyo inayo pelekea majonzi mazito.

Akiongea mwenyeji wao Mchungaji Zabroni Mwakalasi wa kanisa la (KKKT) matema amesema wazee hao wametelekezwa na familia zao, na wengine kutokana na mila za eneo hilo zime wafanya wajikute wametengwa bila msada wowote

“Hawa wazee wameachwa na familia zao kwa imani tofauti ikiwepo kufukuzwa katika miji yao baada ya mume kufa ndugu wanaobaki huwafukuza ili kumiliki mazao yaliyopo katika mashamba hayo likiwepo zao la kokoa ambalo limeku na kipato kikubwa kwa jamii ya watu wa kyela” amesema mwakalasi

Kwa upande wao mmoja wa wazee hao amewashukuru sana Vijana hao kwa moyo waliouonesha kwao kwani yeye amekata tama ya kuishi kwa kudhani hana ndugu wakumfariji

“Asanteni sana kwa kututembelea sisi wazee ninamshukuru Mungu aliewaleta kwetu kwani tulidhani hatuna ndugu tena kumbe tunao tena ni wengi katika kristo yesu” aliongea huku akitokwa na machozi ya uchungu.

Vijana wa Kanisa la moraviani ushirika wa Mbeya mjini walifanya ziara hiyo ya siku mbili mwishoni mwa wiki hii katika fukwe za ziwa nyasa (matema) kwa lengo la kupanga mpango mkakati wa maendeleo yao kwa mwaka 2014-2015

Katika ziara hiyo pia walipata nafasi ya kutembelea wazee wanaoishi mazingira magumu ambapo walitoa misaada mbalimbali ikiwepo Sukari, chumv, sabuni, mafuta ya kupakaa na box la viberit.

Kiongozi wa ziara hiyo John mwambola ametoa wito kwa vikundi vingine na watu binafsi kutembelea watu wenye uhitaji kama hawa kwani wanahitaji sana faraja na misada ya hali na mali kwa mazingira waliyojikuta  wakiiishi bla kupanga.

Mwambola maongeza kua kwakufanya hivyo ni kutimia amri kuu tuliyo achiwa na  bwana wetu yesu kristo alipokua akiondoka hapa duniani yani (UPENDO)




0 comments:

Post a Comment