Pages

Ads 468x60px

Friday, October 17, 2014

Viongozi wa dini na vyama vya siasi wametakiwa kuilinda amani mkoani Mbeya







      Mkuu a wilaya ya Mbeya Norman Sigalla akiongea na viongozi wa dini na siasa





            Viongozi wa Dini, Siasa na kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya mbeya









                          Wadau wakichangi maoni katika mkutano huo

                                                Habari kamili



Viongozi wa dini na vyama vya siasi wametakiwa kuilinda amani mkoani Mbeya
Kwakua Mbeya ilikuwepo kabla ya taasisi hizo



Hayo yame jili katika mkutano wa viongozi wa dini, siasa na kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Mbeya mjini uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo jijin hapa

Akiongea katika kikao hicho mkuu wa wilaya ya Mbeya Norman sigalla amewataka viongozi  hao kuchukua hatua ya kuilinda amani ya wilaya na mkoa kwa ujumla kwakua Mbeya ilikuwepo kabla ya taasisi hizo kuwepo.

“Ndugu zangu nawaomba kuilinda amani ya wilaya kwa dhati kwakua dini na siasa si muhimu kuliko Mbeya yetu, kwakua ipo kabla hata ya dini na vyama vya siasa kwa hiyo ni muhimu kuendesha dini na siasa kwa uangalifu mkubwa ili kusitokee kuihatalisha amani yetu” amesema Sigalla

Ameongeza kua machafuko ya dini yanatokea sana huku Afrika, lakini ziliko anzia dini hizo hawagombani huwezi kuona Uarabuni au Ulaya watu wanagombana kuhusu dini yao jiulize ni kwanini waanzilishi hawapigani ila wapokeaji hupigana ujue ipo shida katika uelewa wao.

Pia Sigalla amewataka viongozi hao kujiuliza kitu chochote wanacho kifanya kina manufaa gani kwa jamii ya watanzania na kinalaeta maendeleo gani kwao ukiona unapamga maandamano unaona kabisa hayana umuhimu kwa maendeleo yao ni bora sana ukayaacha.

Kwa upanda wake makamu wa Shekhe wa mkoa Abdull Azizi amewataka vingozi wote kuchunga sana ulimi kwakua ndicho chanzo kikubwa cha mafarakano mahali popote duniani kwani huchochea na kusababisha machafuko, hata hinyo amempongeza mkuu wa wilaya hiyo kwa kuwa na utaratibu wa kukutana nao mara kwa mara.

Kwa upande wa mmoja  viongozi wa siasa Yasini mlotwa mwenyekiti wa chama cha wananchi (CUF) wilaya ya mbeya ameishauri serikali kuchunguza tenda zinatolewa huchukuliwa na mawakala feki wengine wakiwa watumishi wa serikari ambao hushinda na kufuja pesa za walipa kodi bila manufaa yao.

Mkutano huo ni mkakati wa mkuu wa wilaya ya Mbeya na wadau hao  waliojiwekea ili kukutana kila baada ya miezi sita kwa lengo la kutathimini muenendo wa amani katika wilaya na mkoa wa Mbeya.

0 comments:

Post a Comment