Pages

Ads 468x60px

Wednesday, February 18, 2015

Kuingia kwa sekta ya afya katika BRN kunaleta matumaini mapya


Mtendaji mkuu wa Ofisi ya Rais, usimamizi wa utekelezaji wamiradi (PDB) Bwana Omari Issa, leo amekabidhi rasmi taarifa ya mkakati wa kuboresha sektaya afya chini ya BRN kwajumuia ya wahisani wa maendeleo. Makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi za PDB ambapo jumuiya yawahisani ilipatafursa ya kusikiliza kwa kina namna BRN inavyofanya kazi yakuleta matumaini mapya kwa watanzania kupitia sekta za kipaumbele.

Sekta ya afyaimekuwa ikijaribukuboresha utendaji wake lakini kuingia katika BRN kutaleta tija Zaidi. BRN inaamini katika misingi mikuu ambayo ni kuweka vipaumbele, kuwa na adabu ya utekelezaji,uwajibikaji
 na uaminifu, ufuatiliaji wa kina na wamara kwa mara na Mawasiliano thabiti kati ya watoa huduma nawapokea huduma. Hizi ni  nguzo muhimu zitakazo  tufikisha katika dira ya maendeleo ya taifa ya Mwaka 2025.

Awamu ya kwanza ya BRN iliziangazia sekta sita ambazo ni Kilimo, Elimu, Maji, Uchukuzi, Nishati na ukusanyaji wa mapato ambapo sekta za Afya na Uboreshaji wa mazingira ya Biashara zimeanza rasmi Mwaka huu. Sekta sitaza mwanzo zimedhihirisha mafanikio anuwai ambayo yaliwavutia jopo la wataalamu wamaendeleo wakiongozwa na Rais Mstaafu wa Botswana Bw Mogae. Ripoti kamili ya utekelezaji wa BRN kwa Mwaka wa kwanza itazinduliwa rasmi mape mamwezi Machi Mwaka huu.

Sekta ya afya inakusudia kutekeleza vipaumbele vine ambavyo ni mosi; ugawanyaji sawia wa wa huduma wa afya wenye ujuzi takikana kuanzia ngazi ya chini ya afya ya msingi, pili; utoaji huduma wenye ubora wa nyota tatu katika ngazi zote, tatu; upatikanaji wa dawa na bidhaa muhimu za afya katika ngazi zote, nne; kuimarisha afya ya uzazi nausalama wa mama na mtoto ilikupunguza vifo vya kundi hili muhimu kwa angalau asilimia 60ifikapo Mwaka 2018.

Jumuiya ya wahisani wamepongeza uamuzi wa kuiingiza sekta ya afya katika BRN na wa kithibisha utayari wao wakufanikisha mkakati huu, wametoa wito kwa wizara ya afya, PDB, Sekta binafsi na jamii ya kitanzania kwa ujumla kuhakikisha kuwa mkakati huu utafanikiwa.

Malengo haya yote yanahitaji juhudi kubwa na ya pamoja kutoka kwa jamii, wizara na taasisi zake zote hadi ngazi ya kijiji, wahisani wa maendeleo na sekta binafsi. “tusingoje nani aanze, sote tuwajibike, kila mmoja ajitazame kama anawajibika ipasavyo. Dira ya maendeleo ya Taifa tunayotaka  itupeleke kuwa nchi yenye uchumi wa kati haiwezi kufikiwa tusipofanya kazi kwa pamoja bila kunyoosheana vidole. BRN ni treni iliyoanza safari tayari, kila mmoja anawajibika kuingia kwa wakati na kwania Chanya, ukichelewa ukakuta imeondoka bado unafursa ya kuikimbilia kituo kinachofuata ilitwende pamoja” Bw Omari Issa ametoa wito huo kwa wahisani wa maendeleo najamii kwaujumla.

……………………………………………..xxxxxx………………………………………………..



Annastazia Rugaba, PDB habari, Februari 2015



Mtendaji Mkuuwa PDB Bw. Omari Issa akielezea umuhimu wa sekta ya Afya kuingia BRN kuungana na sekta nyingine zilizotangulia zinazoendelea kuzaa matunda

 

Bw. Omari Issa akimkabidhi mwakilishi wa wahisani wa maendeleo mkakati wa sektayaAfya chini ya BRN





Bw Issa na Dr. Sudha Sharma wa UNICEF Tanzania ambae ana wawakilisha jumuiya ya wahisani wa maendeleo baada ya makabidhiano








Mwakilishi wa jumuiya ya wahisani akipongeza uamuzi waserikari kuiweka sekta ya afya katika BRN



Naibu Katibu mkuu wa wizara ya afya Bw Michael akiwashukuru PDB kwaku simamia vizuri mchakato wa kuchagua vipaumbele vya sekta  yaafya chini ya BRN






Mmoja wa wahisani akisisitiza suala la uwajibikaji katika sekta ya afya





Bi. Sharon Crommer Mkuu wa USAID Tanzania akisisitiza ushiriki wa sekta Binafsi katika kuboresha Sekta ya afya Nchini Tanzania





Mmoja wa wahisani akisisitiza umuhimu wa wizara ya afya kuwajibika ki BRN katika maeneo mengine yasiyo ya kipaumbele katika BRN



Dr Oberline Kisanga wa kitengo cha mageuzi katika wizara ya afya akifafanua ushiriki wa TAMISEMI katika mkakati huuwa afya chini ya BRN



Bw Mugisha na Dr Linda wa PDB wakifurahia sehemu ya makabidhiano ya mkakati wa afya chini ya BRN

 

Sehemu ya washiriki watukio hili wakiwa katika ukumbi wamkutano wa  PDB


0 comments:

Post a Comment