Mtendaji mkuu wa Ofisi ya Rais, usimamizi wa utekelezaji wamiradi (PDB) Bwana Omari Issa, leo amekabidhi rasmi taarifa ya mkakati wa kuboresha sektaya afya chini ya BRN kwajumuia ya wahisani wa maendeleo. Makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi za PDB ambapo jumuiya yawahisani ilipatafursa ya kusikiliza kwa kina namna BRN inavyofanya kazi yakuleta matumaini mapya kwa watanzania kupitia sekta za kipaumbele.
Sekta ya afyaimekuwa ikijaribukuboresha utendaji
wake lakini kuingia katika BRN kutaleta tija Zaidi. BRN
inaamini katika misingi mikuu ambayo ni kuweka vipaumbele, kuwa na adabu ya utekelezaji,uwajibikaji
na uaminifu, ufuatiliaji wa kina na wamara kwa mara na Mawasiliano
thabiti kati ya watoa huduma nawapokea huduma. Hizi ni nguzo muhimu zitakazo tufikisha katika dira ya maendeleo ya taifa ya
Mwaka 2025.
Awamu ya kwanza ya BRN iliziangazia sekta sita ambazo ni Kilimo,
Elimu, Maji, Uchukuzi,
Nishati na ukusanyaji wa mapato ambapo sekta za Afya na Uboreshaji wa mazingira ya Biashara zimeanza rasmi
Mwaka huu. Sekta sitaza mwanzo zimedhihirisha mafanikio anuwai ambayo yaliwavutia jopo
la wataalamu wamaendeleo wakiongozwa na Rais Mstaafu wa Botswana Bw Mogae.
Ripoti kamili ya utekelezaji wa BRN kwa Mwaka wa kwanza
itazinduliwa rasmi mape mamwezi Machi Mwaka huu.
Sekta ya afya inakusudia kutekeleza vipaumbele
vine ambavyo ni mosi;
ugawanyaji sawia wa wa huduma wa afya wenye ujuzi takikana kuanzia ngazi ya chini ya afya ya msingi,
pili;
utoaji huduma wenye ubora wa nyota tatu katika ngazi zote, tatu; upatikanaji wa dawa na bidhaa muhimu za afya katika ngazi zote, nne; kuimarisha afya ya uzazi nausalama wa
mama na mtoto ilikupunguza vifo vya kundi hili muhimu kwa angalau asilimia 60ifikapo
Mwaka 2018.
Jumuiya ya wahisani wamepongeza uamuzi wa kuiingiza sekta ya afya katika
BRN na wa kithibisha utayari wao wakufanikisha mkakati huu, wametoa wito kwa wizara ya afya,
PDB,
Sekta binafsi na jamii ya kitanzania kwa ujumla kuhakikisha kuwa mkakati huu utafanikiwa.
Malengo haya yote yanahitaji juhudi kubwa na ya pamoja kutoka kwa jamii,
wizara na taasisi zake zote hadi ngazi ya kijiji, wahisani wa maendeleo na sekta binafsi. “tusingoje nani aanze, sote tuwajibike,
kila mmoja ajitazame kama anawajibika ipasavyo.
Dira ya maendeleo ya Taifa tunayotaka itupeleke kuwa nchi yenye uchumi wa kati haiwezi kufikiwa tusipofanya kazi kwa pamoja bila kunyoosheana vidole.
BRN ni treni iliyoanza safari tayari, kila mmoja anawajibika kuingia kwa wakati na kwania
Chanya,
ukichelewa ukakuta imeondoka bado unafursa ya kuikimbilia kituo kinachofuata ilitwende pamoja”
Bw Omari Issa ametoa wito huo kwa wahisani wa maendeleo najamii kwaujumla.
……………………………………………..xxxxxx………………………………………………..
Annastazia
Rugaba, PDB habari, Februari 2015
Mtendaji Mkuuwa PDB Bw. Omari Issa
akielezea umuhimu wa sekta ya Afya kuingia BRN
kuungana na sekta nyingine zilizotangulia zinazoendelea kuzaa matunda
Bw. Omari Issa
akimkabidhi mwakilishi wa wahisani wa maendeleo mkakati wa sektayaAfya chini ya BRN
Bw Issa na Dr. Sudha Sharma wa UNICEF
Tanzania ambae ana wawakilisha jumuiya ya wahisani wa maendeleo baada ya makabidhiano
Mwakilishi wa jumuiya ya wahisani akipongeza uamuzi waserikari kuiweka sekta ya afya katika
BRN
Naibu Katibu mkuu wa wizara ya afya Bw Michael
akiwashukuru PDB
kwaku simamia vizuri mchakato wa kuchagua vipaumbele vya sekta yaafya chini ya BRN
Mmoja wa wahisani akisisitiza suala la
uwajibikaji katika sekta ya afya
Bi. Sharon Crommer Mkuu wa USAID Tanzania
akisisitiza ushiriki wa sekta Binafsi katika kuboresha Sekta ya afya Nchini Tanzania
Mmoja wa wahisani akisisitiza umuhimu wa wizara ya afya kuwajibika ki
BRN katika maeneo mengine yasiyo ya kipaumbele katika BRN
Dr Oberline Kisanga wa kitengo cha
mageuzi katika wizara ya afya akifafanua ushiriki wa TAMISEMI
katika mkakati huuwa afya chini ya BRN
Bw Mugisha na Dr Linda wa PDB wakifurahia sehemu ya makabidhiano ya mkakati wa afya chini ya
BRN
Sehemu ya washiriki watukio hili wakiwa katika ukumbi wamkutano wa
PDB
0 comments:
Post a Comment