Pages

Ads 468x60px

Friday, March 6, 2015

Viongozi wa chama cha bodaboda mkoani Mbeya wagomea zoezi la kubadili namba mpya.




Wadai tozo la kodi yake ni kubwa na ni mzigo mzito kwao hawana uwezo wa kuubeba.
 MWENEKITI WA BODABODA MKOA WA MBEYA VICENT MWASHOMA AKITOA TAMKO MBELE YA WAANDISHI WA HABARI NA VIONGOZI WA VITUO MBALIMBALI KATIKA UKUMBI WA COFE GARDEN
 KATIBU MSUMBS MDESA AKISOMA TAMKO MBEYA YA WANACHAMA NA WAANDISHI WA HABARI





 BAADHI YA VIONGOZI WA BODABODA WAKIWASIKILIZA VIONGOZI WAO









 UJUMBE WAO KUPITA MABANGO WAKIONESHA KWA WAANDISHI WA HABARI


Soma hapa

Na Charles Abraham:



Viongozi wa chama cha bodaboda mkoani Mbeya wagomea zoezi la kubadili namba mpya.
Wadai kodi yake ni kubwa na ni mzigo mzito kwao hawana uwezo wa kuubeba
Chama cha bodaboda mkoani Mbeya wametoa tamko la kuto endelea kulipa kodi za kubadili namba mpya linalo tegea kumalizika mach 31/ 2015 kwa mujibu wa mamraka ya mapato Tanzania (TRA) na kwamba endapo hawatabadili kwa muda huo basi watalipa gharama hizo pamoja na faini

Wakizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ulifanyika katika ukumbi wa cofi garden uliopo jijini hapa mwenyekiti wa chama hicho VICENT MWASHOMA amesema hawawezi kutoa gharama hizo kwakua serikali haijatoa elimu  vizuri  kwa waendesha bodaboda kwani  ni tofauti na ukienda kulipia

“Ndugu waandishi Serikali  ilikua na dhamila nzuri katika kuendesha zoezi hili la kubadilisha kutoka namba za vibao vya njano kwenda vyeupe hii ingerahisisha usimamizi na utawala kwa pikipiki zetu lakini pia kuzipata zilizoibiwa hii ilikua ni nia njema, Tuliambiwa tutalipa shilingi elfu kumi tu, sasa ni tofauti na ukienda kulipa  tunalipishwa kiasi cha laki moja hadi laki tano kitu ambacho hatuwezi kumudu” amesema Mwashona

Kwa upande wake katibu wa chama hicho MSUMBA MDESA amesema kuanzia leo wamesitisha zoezi la usajili wa namba mpya za pikipiki  kwa kuiambia Serikali hawapo tayali kwa utaratibu waliouanzisha wa ulipishwaji wa gharama za usajili wa vyombo vyetu kwakua tunajua tunaonewa .

“Nataka kusema kuanzia sasa hatutalipa gharama hizo ili kulipia namba mpya kwakuwa kwani anaepaswa kulipa ni muuza duka anapo ingiza chombo nchini anatakiwa atozwe hiyo kodi ya lakini si mtumiaji wa mwisho ambae ni kijana wa kitanzania aliyekosa ajira na kuchukua mkopo ili kujiajiri iSerikali inakuja kumkandamiza kwa kumtwisha mzigo mzito wa kodi kubwa hata kabla ajaanza kurejesha mkopo. Amesema Mdesa.

Ameongeza kuwa anaiomba serikali iliangalie upya swala hili na kutengeza mazingira mazuri kwa vijana  wanaotafuta namna ya kujiajiri  wasiweke mazingira ya kutaka tuandamane.

MWISHO





 

0 comments:

Post a Comment