Pages

Ads 468x60px

Monday, April 20, 2015

Haruna mwanauta awaza kutia nia ya kugombea ubunge na kumrithi Victor Mwambalaswa Chunya kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)



Imeelezwa kuwa  wilaya ya Chunya  ina rasilimali nyingi ambazo zinaweza kuwaondoa wananchi wake kwenye umaskini  pia kuifanya  wilaya hiyo kuwa tajiri  na kuwa nufaisha wananchi  wake.
 Hayo yamebainishwa na HARUNA MWANAUTA  ambaye ni mfanya biashara mkubwa katika sekta ya utarii na uwindaji wa wanyama poli katika kitalu cha Rungwa mwamagembe kilichopo  Lupa wilayani humo.

Mwanauta ameyasema  hayo wakati akizungumza na mwandishi wa habari  kuwa wilaya hiyo inayo dhahabu nyingi na wachimbaji wakubwa ambao wanaweza kuinufisha kwa kodi zao na pia kuwaunganisha wachimbaji wadogo ili waweze kukopesheka na  kununua vifaa vya kuchimbia  
HARUNA MWANAUTA
madini

Amesema swala la wilaya hiyo pamoja na wananchi wake kuitwa masikini yeye anapingana nalo,  nakumesema kuwa nikuwakosea wananchi wake  kwani  wanayo migodi ya Dahabu pamoja na kilimo cha Tumbaku ambacho kinaweza kuwa kwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini uliokithili .

 “Chunya inahitaji kiongozi mwenye ushirikiano na  wananchi katika kuwajengea uwezo wa kujikwamua katika umasikini uliopo , Kwani imegawanyika katika makundi mawili makuu kiuchumi ikiwepo Dhahabu na kilimo cha Tumbaku lazima apatikane kiongozi atakae wezesha sekta hizi mbili ziwanufaishe wananchi wa chunya” amesema Mwanauta.

 chunya ina ardhi yenye Rutuba inayo kubali kilimo cha aina yoyote, wananchi  waatumie  maafisa ugani kulima kilimo chenye tija na kutumia fursa ya uwanja wa Ndege wa songwe kuuza nje ya nchi mazao yao
  
Aidha  mwanauta amekua akiiangalia wilaya hiyo kwa mtazamo wakipekee na kuona fursa iliyo nayo ya dhahabu pamoja na kilimo kinaweza kuwanufaisha  kisha kuondokana dhana iliyo jengeka kwamba wilaya hiyo ni masikini pamoja na wakazi wake,  ameamua  kujitosa  kugombe nafasi ya ubunge muda utakapofika na kumrithi Victor Mwambalaswa aliyepo sasa

0 comments:

Post a Comment