WAZIRI wa Maliasili na Utalii,
Lazaro Nyalandu, amemaliza mgogoro wa ardhi uliodumu karibu miaka 10 wilayani
Mbarali, mkoani Mbeya.
Mgogoro huo unahusisha wakazi wa vijiji 21 waliotakiwa kuondolewa kwa madai ya kuvamia eneo la Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
Mgogoro huo unahusisha wakazi wa vijiji 21 waliotakiwa kuondolewa kwa madai ya kuvamia eneo la Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
Nyalandu, ambaye yuko ziarani mkoani
Mbeya, jana alizungumza na wananchi na kuwahakikishia
kuwa Serikali haiwezi
kuwaacha wakiangamia.
Akizungumza katika mkutano na waandashi wa habari uliofanyika katika hotel ya Hill View jijini hapa alisema wananchi wanaoishi vijiji hivyo hawatahamishwa.
![]() |
Waziri Lazaro Nyarandu |
Akizungumza katika mkutano na waandashi wa habari uliofanyika katika hotel ya Hill View jijini hapa alisema wananchi wanaoishi vijiji hivyo hawatahamishwa.
Alisema uamuzi huo ni utekelezaji wa
maelekezo ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kuitaka Serikali
kuhakikisha inamaliza mgogoro huo.
Alisema kwa muda mrefu mgogoro huo umekuwa ukitafutiwa ufumbuzi wa kudumu na umefika wakati ni lazima mambo yafikie mwisho ili wananchi waendelee na shughuli zao za maendeleo.
Alisema kwa muda mrefu mgogoro huo umekuwa ukitafutiwa ufumbuzi wa kudumu na umefika wakati ni lazima mambo yafikie mwisho ili wananchi waendelee na shughuli zao za maendeleo.
“Naomba niseme kuwa vijiji
vinavyotakiwa kuhama vitaendelea kuwepo na ninaagiza kufanyika kwa ukaguzi wa
mpaka katika GN 28 ili kuhakikisha haki inatendeka katika suala hili. Huu
mgogoro ni lazima ufike mwisho na uamuzi huu una baraka zote za Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda,” alisema Nyalandu.
Alisema maeneo yenye mgogoro mengi ndiyo kilimbilio na uchumi wa wananchi wa
Mbarali kutokana na kuendesha shughuli za kilimo na makazi, hivyo Serikali
haiwezi kuchukua uamuzi utakaokuwa na madhara kwa wananchi wake.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM
Wilaya ya Mbarali, Mathayo Mwangomo, alisema mgogoro huo umeleta mpasuko mkubwa
na kusababisha wananchi kukosa imani na baadhi ya viongozi.
Naye, Mbunge wa Mbarali, Modestus Kilufi, alisema mgogoro huo umedumu kwa miaka
mingi na ilikuwa ni lazima mwafaka ufikiwe ili kuleta amani na utulivu ulioanza
kutoweka.
Waziri Lazao Nyarandu akiongea na baadhi ya Waandishi wa Habari Hill view Hateli jijini Mbeya
0 comments:
Post a Comment