Pages

Ads 468x60px

Monday, April 27, 2015

Wakuu wa wilaya ya Rungwe na Kyele wa watimua LHRC



Maafisa wa kituo cha haki za binadamu(LHRC)  watimuliwa na wakuu wa wilaya ya Rungwe na Kyela baada ya kushindwa kujibu maswali yenye utata,hayo yamebainishwa na ZAINABU MBUSSI mkuu wa wilaya ya Rungwe alipokua akiongea na mwandishi wa habari hizi kujibu tuhuma zilizotolewa kwake kuwafukuza maafisa hao katika wilaya yake.
William Kahale

“ niliwasimamisha kuendelea na zoezi la kuendesha mdahalo na wananchi wa wilaya yangu kutokana na wao kushindwa kujibu baadhi ya maswali yangu kitu ambacho kilinitia shaka juu ya elimu wanayotaka kuipeleka kwa Wananchi wa Rungwe huenda haitakuwa sahihi.

Mwassa Jingi

Hali hiyo imejitokeza baada ya mmoja wa maafisa hao WILLIAM KAHALE katika mkutano na waandishi wa habari mkoa wa Mbeya uliofanyika katika ofisi za Mbeya Press Club zilizopo Soweto jijini hapa na kutoa shutuma kwa wakuu wa wilaya hao kuzuia kufanya midaharo ya katiba pendekezwa katika wilaya zao bila kupewa sababu za msingi.

“Nataka kuongea changamoto ambazo tumekutana nazo katika wilaya mbili katika utoaji wa elimu ya katiba mpya kwa niaba ya Tume ya uchaguzi kwa mujibu wa sheria kama tulivyopewa mamlaka kinyume na katiba ya jamhuri ya Tanzania ibara ya 18 na 21 ibara ndogo ya pili kwa kua tumepewa huo uhuru, Sheria ya kura ya maoni imeikaribisha Tume kutoa elimu ya uraia Tume imetupa majukumu asasi za kiraia kutoa  elimu kwa niaba yake, wametuzia kwa makusudi na kuvunja sheria
ya uchaguzi” amesema KIHALE
 
Awali Katika hali ya mchakato wa kuunda katiba mpya Sheria ya kura ya maoni  imeipa mamlaka Tume ya uchaguzi  kukaribisha Asasi za kiraia kutoa elimu ya uraia na kuziruhusu asasi za kiraia zaidi ya miatatu (300)  kutoa  elimu hiyo kikiwepo kituo cha sheria na haki za binadamu

                    Grace Mgonja Constitutional Trainer Sociologist (LHRC) akiongea na waandishi wa habari




                               Baadhi ya wananchi wa habari wakisikiliza kwa makini ndani ya mkutano huo.

                            Vailety Jailo kutoka Sweety Fm Radio akiongea jambo katika mkutano

0 comments:

Post a Comment