Pages

Ads 468x60px

Wednesday, April 29, 2015

Watu wenye ulemavu wa kusikia Viziwi waipongeza Benki ya CRDB



Watu wenye ulemavu wa kusikia yaani Viziwi wameupongeza uongozi wa Benki ya CRDB mkoa wa Mbeya kwa  kuwapatia elimu ya ufunguaji  na utunzaji wa pesa katika akaunti za Benki.
 Shukrani hizo zimetolewa  na mwenyekiti wa Viziwi mkoan hapa TUSSA MWALWEGA alipokua akiongea katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki hiyo katika ukumbi wa  Youth Center.
Tussa Mwalwega

“Kumekuwepo na dhana potofu kwa jamii ya watanzania kwamba sisi watu wanye ulemavu wa kusikia tupo tofauti na wengine na kwamba yapo mambo ambayo haya tuhusu kitu ambacho si kweli sisi ni sawa na watu wengine na tunastahili kuchukuliwa kama hao kwani ulemavu hatukupenda kuwanao i ila tunaushukuru uongozi wa benki hii kwa namna ambavyo wamekubali  na kuona umuhumu wa kutoa elimu hii kwetu”  amesema Mwalwega.

Kwa upande wake STEPHAN MWAIPOPO ambaye alikuwa mkufunzi wa semina hiyo amewataka walemavu hao kujitokeza kwa wingi katika kufungua akaunti katika benki hiyo .

Mwaipopo amesema kuwa watawapunguzia gharama za kufungua   kutoka elfu ishilini hadi elfu kumi tu, kwa kuw a kunafaida nyingi  ikiwepo utunzaji wa pesa zao pamoja na mikopo midogo yenye riba nafuu itakayowawezesha kuendeleza  biashara zao ndogondogo zitakazo wafanya wajikwamue kiuchumi.

Naye meneja wa benki hiyo BENSON FRED amesema zoezi hilo lilikua gumu kutokana kushindwa kuelewana kutokana na kutokua na uelewa wa lugha ya alama ambayo wanatumia walemavu hao  lakini kwa sasa wamepata mtu mwenye ujuzi wa kutafsili lugha hiyo iameahidi kuendesha semina hiyo kwa wilaya zote za mkoa wa Mbeya ili kuwahamsisha kufungua akaunti katika benki yeke.

Meneja wa Benki ya CRDG Benson Fred  mwenye koti jeusi katika akiongea na watu wenye ulemavu wa kusikia VIZIWI kwa kutafsiliwa na mtaalamu wa Rugha ya alama FARAJA MBWILO katika semina hiyo



Mkufunzi wa Semina STEPHAN MWAIPOPO kutoka CRDB aliepo kushoto akifundishwa na kutafsiliwa na mkalimani Faraja MBWILO






      Wanasemina kutoka wilaya mbalimbali za mkoa wa Mbeya wakiwa katika mafunzo
         Lupi Mwaisaka Afisa Jinsia CHAVITA makao makuu akiongea jambo katika semina
                                                                        Fadhili kwale

                                                              Isdory Mwashimaha
                                Tussa Mwalwega mwenyekiti wa CHAVITA Mkoa wa mbeya
                                                                       Gwantwa Mugha
                                                               Severin Lwenagira
                                                              Tunganege Jackson
                                     Washiliki wa semina wakiuliza maswali baada ya mafunzo


0 comments:

Post a Comment